Mradi wa Digital Broadcasting TBC

Tanzania!!
I cant you!!
is there a place where a group of people sit and look at the whole picture? get it in their heads and set priprorities? hata sidhani,

Priorities are there can't u see; we watu wamesafiri mpaka China......... we vipi wewe!!!:angry:
 
... Jamani huko juu mbona wengine mnaponda?? kama TBC yetu ina channel alizotaja Charity kama BBC, AlJaazera, Channel 10, Citizen (kenya), Setanta (sports) na kadhalika nadhani kwa shs alfu 9 tu sio mbaya kiasi hicho! Ndio Mwanzo. labda niulize tu kama kuna channel yenye Sitcoms kama ile iliyowahi kuwa ITV ya EBN ambayo sijui iliishia wapi iliyokuwa na Sitcoms kama The Parkers, Everybody Loves Raymond, Daimon nakadhalika! Halafu huu ushamba nao, jamani nauliza msinicheke. Hivi hii Decorder unaweza kuifunga mwenyewe bila kulazimika kutafuta fundi na haina haja ya Dishi la nje????

Asa ulitaka tuunge mkono kitu hafifu? Ona we mwenyewe ushaanza kuulizia unazopendaga
 
watoto wanaipenda kwani channel zao za watoto ni nzuri (kwangu) kuliko zilizokuwapo DSTV ($30,000)

Nadhani ulimaanisha $30 na kwa DST cartoon unapata Cartoon Network ; Kidsco, Boomerang na nyingine! 4 channels out of two; well mie mpaka ifike huku mkoaani na nihakikishe operation yake from a subscriber; kwangu mpira sio priority; aaafu vipi kuhusu parental guidance?
 
sasa hivi chaneli zimeongezeka jamani zinafika 50 na kitu na ukiwa na antena ya nje unapata local chanels
 
Gharama nafikiri watu wengi wamekwisha eleza huko nyuma, jaribu kusoma waliotangulia. Ila ni nzuri hasa kama huna uwezo wa mambo makubwa kama DSTV, hutajutia pesa yako. Tatizo tunalolipata kwa sasa ni kuwa bado wanaonekana wapo kwenye aidha majaribio au bado wako kwenye instalation. Maana mara matangazo yanakatika, au wanaanza ku-search upya!. Napenda zaidi chanel zao za watoto (cartoons), ni nzuri sana.
 
kwa sisi kcc wakianza kulipia ndio watakuwa wametufuta kiaina hata mkuu wa kaya akitukoromea hatutamuona ,lkn tutatozwaje kuona wakati tbc inaendeshwa kwa kodi zetu tunazokatwa kwenye vijimshahara vyetu
 
hao wanawaibia tu,kama ni mradi wa DIGITAL TV hakuna haja ya kununua decoder you just need A DIGITAL TV na antennae nzuri unapata free digital channels,otherwise labda hio ni subscription tv kama DSTV sio national tv ninavyojua TBC NI NATIONAL TV sasa kwanini ulipie na iko run na kodi za wananchi??
 
Kiukweli huo mpango wao unahitajika kuboreshwa ili hiyo digital broadcasting iwe bora maana kwa sasa bora analog isiyokwamakwama. digital inakwamama hadi unachoka kutazama. cha msingi kama vipi waongeze minara ili upatikanaji wa mawimbi uwe bora zaidi
 
drphone rejea posts za mwanzoni mwa topiki!

naambiwa mikoani decorder wanaziuza hata kabla ya kuwasha mitambo yenyewe! Mlioko Mwanza na Arusha tuhabarisheni.
 
Hizo channel nyingi zilizomo kwenye hiyo decoder yao kama hizo za watoto mnazosema ni free to air hivyo wale wenye madishi ya FTA hawana haja na hiyo decoder ya kulipia maana kila kitu chao ni cha Free to air pengine urahisi wao ni kuwa ukiwa na decoder tu inatosha huitaji matangazo ya dish la nje kuwa na wewe unalo. ha ha ha.
 
Kiukweli huo mpango wao unahitajika kuboreshwa ili hiyo digital broadcasting iwe bora maana kwa sasa bora analog isiyokwamakwama. digital inakwamama hadi unachoka kutazama. cha msingi kama vipi waongeze minara ili upatikanaji wa mawimbi uwe bora zaidi
Hivi wananchi haswa watanzania masikini watahitajika kuwa na decoda ngapi ili waweze kuona stations locat/za hapa nyumbani walizokuwa wanaziona mwanzo? Maana kila watu wanajiunga kivyao na wanatoa decoda kianaaina/kivyao.
 
Hivi hili swala la kila kampuni au TV station kuwa na decoda yake na kumfanya mwananchi kununua na kulipia Decoda lukuki inakuwaje hebu tufafanulieni jamani.
 
Hivi wananchi haswa watanzania masikini watahitajika kuwa na decoda ngapi ili waweze kuona stations locat/za hapa nyumbani walizokuwa wanaziona mwanzo? Maana kila watu wanajiunga kivyao na wanatoa decoda kianaaina/kivyao.

kuna mazungumzo yanaendelea baina ya hawa wamiliki wa vituo vya tv kuona kuwa wanatumia mfumo mmoja wa digital kurusha matangazo
 
kuna mazungumzo yanaendelea baina ya hawa wamiliki wa vituo vya tv kuona kuwa wanatumia mfumo mmoja wa digital kurusha matangazo
Bora iwe hivyo, maana wasipofanya hivyo tutapata taabu kuwa na decorder nyingi!
 
Kwa current gossip nilizopata ni kuwa hawa jamaa wa itv wana bifu na tbc, so huo muafaka ni adimu kidogo. Pia star tv naona wako kivyaovyao sana. Pia watakaojiunga na star media ni pamoja na tv clouds, mlimani tv, c2c, tbc 2. Utakuwa na haja gani tena ya tv zingine?
 
Mradi huu ni mkubwa sana kwa budget yetu ya 6trilion ambayo 35% ni michango kutoka nje there is no way kwa serikali kuwekeza ili wastahili hizo 65% shares. Tunashindwa kujenga shule na zahanani za kutosheleza nchini, maji safi na salama bado ni ndoto kwa wengi, Umeme na barabara ndiyo usiseme.
Kutokana na hali kama hakuna njia nyingine zaidi ya kuruhusu wawekezaji kuwa na hisa zaidi. Pengine cha msingi ni kuwe na kipengele kwenye mkataba wa kukubaliana kuwa katika siku za usoni serikali inaweza kununua hisa hizo.
Watu wa dar wameanza kufaidi huduma hii ambayo ninadhani iko kwa majaribio kwa gharama ya aprx sh300 kwa siku. Ninadhani gharama [shs70,000] kwa decoder zitapungua kadiri ya coverage itakavyoongezeka. Mradi huu ukifanikiwa basi hata elimu kwa njia ya TV itakuwa rahisi zaidi.
Mimi nadhani tuache tabia ya kuwa pessimists kwa kila jambo kwani matokeo yake ni kudumaza fikra za kuthubutu kufanya mambo makubwa yenye manufaa kwa nchi yetu
 
Kwa current gossip nilizopata ni kuwa hawa jamaa wa itv wana bifu na tbc, so huo muafaka ni adimu kidogo. Pia star tv naona wako kivyaovyao sana. Pia watakaojiunga na star media ni pamoja na tv clouds, mlimani tv, c2c, tbc 2. Utakuwa na haja gani tena ya tv zingine?
Hizo TV stesheni zote zitakazojiunga na Star Media bado hazina ubora unaotakiwa, kuna ulazima wa kuwepo ITV na Star TV.
 
Back
Top Bottom