Mrabaha au mrahaba?

dazu

JF-Expert Member
Feb 26, 2011
365
76
Wanajamvi naomba ufafanuzi, kipi kiswahili sahihi, kumaanisha ile token tunayopewa na wawekezaji wetu hasa kwenye madini: Mrahaba au mrabaha?
 
Mrahaba ndiyo sahihi ila MRABAHA sina uhakika kama ni sahihi.
 
Sahihi ni mrabaha. Inasemekana kuwa hili ni tatizo linalowakuta baadhi ya watu katika lugha zote wanaobadilisha nafasi ya tamshi katika neno. Kwa mfano, maralia badala ya malaria.
 
Hili neno lina utata sana, mimi nijuavyo sahihi ni 'mrabaha' (nadhani ikitokana na neno la kiarabu, 'murabahah') lakini kuna wengine wanasema sahihi ni 'mrahaba'. Iliwahi kusemwa bungeni hivi:
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende kwenye maeneo machache ambayo nayafahamu vizuri ili niweze kuboresha Bajeti hii.

Kwanza nije kwenye mchango wa madini kwenye Pato la Taifa. Naungana na wenzangu kwamba mchango wake ni kidogo sana na matatizo ni Mikataba tuliyonayo. Kwanza labda nisahihishe neno moja tu ambalo linatumiwa hapa ndani ya Bunge, hakuna neno mrahaba kwenye Kiswahili, Kiswahili sanifu ni mrabaha, naomba mwangalie kwenye Kamusi zenu. Watu wote naona wanasema mrahaba, mrahaba nadhani hicho ni Kisukuma.
(Kicheko/Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mrabaha au royalty ya asilimia tatu ni ndogo sana. Namshauri Waziri wa Madini na Waziri wa Fedha, kaeni mpange royalty mpya, mrahaba mpya. (Makofi)

MBUNGE FULANI: Mbona wewe mwenyewe unasema mrahaba?


MHE. YETE S. MWALYEGO: Mrabaha mpya. Unajua mazoea tena. Napendekeza asilimia kumi ili tuweze kuongeza pato la Taifa. (Makofi/Kicheko)



Mheshimiwa Naibu Spika, pia limezungumzwa suala la lugha ya Kiswahili kwamba, tusiishie kutoa nyaraka na maelekezo bali tuchukue hatua madhubuti za kuhakikisha kwamba kauli za Serikali zinatekelezwa. Nataka niliahidi Bunge lako Tukufu kwamba sisi katika Wizara tumejiandaa kauli ile imepelekwa kwa Waziri wa TAMISEMI na yeye amepeleka kwa Halmashauri zote zilizopo chini ya TAMISEMI, tumepeleka kwa Waziri wa Utumishi na yeye pia ameshatoa maagizo kwa Ofisi zote za Serikali kuhakikisha kwamba zinatekelezwa lakini ushauri uliotolewa na Bunge tutaufuatilia na tutajitahidi kuhakikisha kwamba maelekezo haya yanatekelezwa ikiwa ni pamoja na kuona kwamba, tunatumia Kiswahili sanifu, saa kumi badala ya masaa kumi, mrabaha badala ya mrahaba na kadhalika. (Makofi)


Nimeona hata google translation inachanganya hayo maneno mawili hivi: Mrahaba=Royalty , Mrabaha = Royalties!
 
Back
Top Bottom