Mr. President... Please don't do it. tomorrow..

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Mhe Rais,

Najua pressure ambayo unayo toka kwa GB na Brown hasa kuhusu suala la Zimbabwe. Wanatarajia support ya Tanzania likitolewa Azimio la Umoja wa Mataifa la kulaani Zimbabwe na matukio yote yaliyotokea baada ya uchaguzi na hasa kitendo cha kutotangaza matokeo.

Ninafahamu ni jinsi gani wakuu hawa wanajaribu kukujenga na kukupa ujiko kama alivyofanya Blair kwa Mkapa na hiyo kuinua profile yako kimataifa kuliko wakati mwingine wowote ule.

Ninafahamu baada ya US kumwaga Dola Milioni karibu 700 wanauwezo wa kuitisha wimbo itakuwa vigumu kuwakatalia. Nafahamu pia Uingereza na wenyewe wameandaa kimfuko kizuri tu kuendeleza ushirikiano na urafiki..

Yota haya nafahamu na nina uhakika na wewe unafahamu. Kwamba wakuu hawa katika suala la Zimbabwe wanataka nchi ya Kiafrika ambayo inaweza kumsimamia Mugabe na kumwambia ukweli bila woga na wao (US na UK) watakuwa tayari kusupport na kuanza kusema "even the AU, Tanzania or President of Tanzania" anaunga mkono. Najua watapamba kwa kutumia nafasi yetu ya historia ya ukombozi n.k na hivyo sauti ya Tanzania kuhusu Zimbabwe itakuwa na nguvu sana.

Sasa Mhe. Rais, hata kama unaamini unayotaka kusema au ambayo wanatarajia useme, naamini hapo siyo mahali pake. Wewe hapo UN piga maneno ya kidiplomasia lakini msimamo wa serikali yetu kuhusu Zimbabwe usisemwe hapo nenda ukausemee nyumbani kwenye Ikulu yetu. Hatutaki Rais wetu uonekane Kibaraka wa wakubwa! Ukisharudi nyumbani na kukutana na baraza lako la mawaziri basi ndio mchukue msimamo kama Taifa na kuamua kulaani hali ya kisiasa ZImbabwe.

Ombi langu ni hilo tu, usitumiwe na wakubwa kuwafanyia kazi yao chafu. Kama una jambo zito la kusema kuhusu Zimbabwe nenda kasemee katika Ikulu yetu pale Magogoni. Vinginevyo, Africa yaweza kukuona umenunuliwa!
 
Ombi langu ni hilo tu, usitumiwe na wakubwa kuwafanyia kazi yao chafu.


Nakubaliana na wewe MKJJ kwa hoja yote isipokuwa pale tu unaposema kwamba suala la kutia pressure issue ya Mugabe na Zimbabwe ni kazi chafu ya mataifa ya magharibi, natofautiana moja kwa moja na wewe kwenye hilo.

Mugabe is the shame of Africa. Mugabe amemfanya Tabo Mbeki kuwa kituko kwenye diplomasia ya kimataifa na hata nyumbani kwake South Africa. Kwa kifupi Mugabe amepoteza muelekeo na yupo tu kwa sababu zake binafsi na sio kwa ajili ya Zimbabwe anymore. Nadhani amepoteza uwezo wa kufikiri na kutenda rationally. Tumsaidie aondoke salama, ili Africa tupunguze aibu nyingine moja (baada ya Kenya) na tubaki na aibu za Somalia na Darfur kwa sasa.
 
Kama itasaidia kufanya Dikteta Mugabe aondoke aseme tuu chochote,na wewe mwanakijiji tuondolee unafiki wako hapo huku fact ziko wazi huyo mpuuzi mugabe ndio chanzo cha matatizo yote ya wazimbabwe weupe na weusi...almost a milion zimbabweans refugees,100,000 inflation,njaa na hataki kutangaza matokeo ya uchaguzi kwa sababu kashindwa lakini bado unamwona huyu jamaa wanaompinga ni vibaraka,naona umeanza kuishiwa wewe.
 
Koba, pinga hoja kwa hoja kulazimisha hoja kwa kuita watu majina hakuifanyi hoja yako kuwa na nguvu zaidi bali inaonesha udhaifu wako wa kujenga hoja! Of course, nisingetegemea kitu tofauti, ni kanzu tu imebadilika.

Nurujamii, labda sijaeleweka vizuri na nimeangalia hapo juu kama kuna mahali nimesema Mugabe anastahili kuwa Rais wa Zimbabwe (of course sisi ni nani kuwaamulia). Nilichosema ni kuwa, kama msimamo wa kumlaani Mugabe na kutaka matokeo yatangazwe nk ufanywe kwenye ardhi ya kwetu. Kwenda kumtukana mtu halafu umejificha kwa mtu mwenye nguvu hakukufanyi uonekane kuwa una nguvu.

Msimamo wa Tanzania kuhusu Zimbabwe utangazwe Tanzania, UN ni kwa wanadiplomasia na watu kupigiana kelele tu. Na tukisha chukua huo msimamo kuhusu Zimbabwe, hatuna budi kuchukua kuhusu Darfur na Iraq... na yote tutangazie toka ardhi yetu.
 
Mwanakijiji

Maneno hayo ni mazito na wengi hawawezi kuona maana yake kwani yana ujumbe mkali sana.


Kwa maoni yangu SADC wakutane ikiwezekana Dar within this week na watoe tamko la pamoja na kumthibiti huyu Mzee ambaye amepitwa na wakati. Yaani amechafua hali ya kisiasa ambayo ilikuwa imejengwa within SADC na sisi wote nchi za kiafrika tunaonekana punguani. Just imagine when they met in Lusaka what the hell were they talking about? Kama Mugabe hataki kutoka SADC wamng'oe PERIOD! Na hili litakuwa fundisho kwa wote within the region.
 
Dua.. you got it right.. sitaki Mugabe adindiwe US.. kama Tanzania ina ubavu wa kumuita Mugabe dikteta wamuitie nyumbani kwetu siyo kwa hawa jamaa!
 
Mkjj:
Katika mambo yoote, hili bado ninamwamini Kikwete bado anamsimamo. Sidhani kama zile pesa zitamrusha akili - hapana nadhani hawezi kununulika.

Hawa wanaomlaumu Mbeki hawajui walisemalo. Matatizo wanayoyapata Wazimbabwe ni makubwa, mengi yanamlalia Mugabe; lakini Waingereza na Waamerika hawaepi sehemu zao za lawama.
 
The Game has begun...

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

WAZIRI Mkuu wa Uingereza, Gordon Brown leo (Jumatano, Aprili 16, 2008), amemshutumu Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe, akimwita mwizi wa kura, kuhusiana na Uchaguzi Mkuu wa Zimbabwe uliofanyika Machi 29, mwaka huu.



Shutuma hizo za Brown zimetolewa kwenye siku ambako Uingereza na Marekani, kwa pamoja, zimeongeza kasi ya shinikizo lao kwa Serikali ya Rais Mugabe kuhusiana na uchaguzi mkuu huo.



Nchi hizo mbili zimetumia nafasi ya mkutano wa viongozi wakuu ulioitishwa kujadili jinsi Umoja wa Mataifa (UN) unavyoweza kushirikiana na Umoja wa Afrika (AU), katika kutatua migogoro ya Afrika, kuishambulia Serikali ya Mugabe ya Zimbabwe.



Waziri Mkuu Brown amekuwa wa kwanza kuzungumza katika kikao hicho cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwenye Makao Makuu ya UN mjini New York, Marekani.



“Uchaguzi ulioibiwa hauwezi kamwe na kwa njia yoyote ile kuwa uchaguzi wa kidemokrasia,” amesema Brown katika hotuba yake ya dakika tano kwenye kikao hicho.



Zimbabwe ambayo ilifanya uchaguzi mkuu Machi 29 mpaka sasa haijatangaza matokeo ya kura ya urais, siku 18 tokea kufanyika kwa uchaguzi huo, ingawa mpaka sasa matokeo ya serikali za mitaa, ya ubunge na ya seneta yamekwishatangazwa.



Brown ambaye nchi yake itakuwa Mwenyekiti wa Baraza la Usalama la UN mwezi ujao, hata hivyo, ametumia hotuba yake hiyo kutoa sifa kwa Jumuia ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) kwa juhudi zake katika kutafuta ufumbuzi wa tatizo la kisiasa la Zimbabwe.



“Lazima nielezee furaha yangu kwa jitihada zinazofanywa na SADC kutafuta ufumbuzi wa tatizo la Zimbabwe. Nafurahi zaidi kuwa jumuia hiyo itakutana tena mwishoni mwa wiki hii kujadili tena hali ya Zimbabwe



Naye Mwakilishi wa Kudumu wa Marekani katika UN, Balozi Zalmay Khalilzad ameishutumu Zimbabwe kwa kusema kuwa ni dhahiri kuwa wananchi wa Zimbabwe wamenyimwa nafasi ya mabadiliko hata kama walipiga kura wakitaka kuona mabadiliko katika uongozi na mwelekeo wa nchi yao.



“Ni siku 18 sasa tokea kufanyika kwa uchaguzi mkuu katika nchi hiyo, na mpaka sasa bado hakuna kauli yoyote juu ya matokeo ya kura ya urais. Ni dhahiri kuwa wananchi wa Zimbabwe wameibiwa,” amesema Balozi Khalilzad.



Balozi huyo ametoa mapendekezo matano ya jinsi ya kutimiza matakwa na utashi wa mabadiliko ya wananchi wa Zimbabwe, ikiwa ni pamoja na kuundwa kwa kundi la pamoja la UN na AU kutafuta njia ya kumaliza mgogoro huo.



Waziri Mkuu Brown amekuwa mmoja wa viongozi kadhaa wa serikali na nchi ambazo wamehudhuria mkutano wa leo uliotishwa na nchi ya Afrika Kusini ambayo ni mwenyekiti wa sasa wa Baraza la Usalama la UN.



Viongozi wengine ni Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri Mkuu wa Italia, Romano Prodi; Rais wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo; Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Joseph Kabila; Rais wa Somalia, Abdullahi Yusuf Ahmed; Waziri Mkuu wa Ethiopia, Meles Zenawi na Mwenyekiti wa Tume ya AU, Alpha Omar Konare.



Viongozi na wawakilishi wa nchi 42 wamezungumza katika kikao cha leo.



Mwisho.


Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais na Habari

NEW YORK.



17 Aprili, 2008
 
Kikao cha SADC kilichokaa Lusaka over the weekend kilitoa tamko gani, na nani alituwakilisha kwenye kile kikao?
 
Matokeo bado hayajatangazwa rasmi na chombo kinachohusika, hivyo mnategemea hawa jamaa SADC watafikia maamuzi gani?..
Nilisoma mahala kuwa Mbeki kabla hajaelekea Lusaka alipitia Harare na alikutanishwa na hiyo kamati ya kuhesabu kura...
Katika hilo yamekutwa matatizo mengi sana ambayo yalifanyika kinyume cha sheria za Upigaji kura na haikutajwa kama ni ZANU - PF waliocheza rafu ama MDC lakini kuna matatizo ambayo yanahitaji kurejebishwa kwanza.
Sasa hii iwe mchezo wa Mugabe ama nani kusitisha kutangazwa, hatuwezi kutoa hukumu zetu leo ikiwa hadi leo hii haijatangazwa mshindi kati yao.
Ni sawa na mtu kutaka kwenda simama mahakamani wakati kesi yako haijasomwa pamoja na kwamba imewasilishwa.. Tufanye subira Ukweli utakuja gundulika tu hata kama imani zetu zinatuambia Morgan ndiye mshindi..
What if Mugabe ndiye kaiba kura kibao kupitia foreign voters ambao hawaruhusiwi kulingana na sheria za Zimbabwe?..
 
Mwanakijiji still bado anaamini matatizo ya Zimbabwe ni weupe,na anafikiri JK kuongelea US ni ukibaraka,kweli umeishiwa wewe na siasa zako za kizamani..hilo zee lazima liondoke tuu hata kama ni wazungu wataliondoa itakuwa vizuri sana,yaani kutoa matokeo tuu limekataa na linawafanya wananchi wawe wakimbizi kwa njaa na udikteta wake,lakini sishangai maana kina mwanakijiji wanao mpa kichwa wapo wengi
 
Ombi langu ni hilo tu, usitumiwe na wakubwa kuwafanyia kazi yao chafu.


Nakubaliana na wewe MKJJ kwa hoja yote isipokuwa pale tu unaposema kwamba suala la kutia pressure issue ya Mugabe na Zimbabwe ni kazi chafu ya mataifa ya magharibi, natofautiana moja kwa moja na wewe kwenye hilo.

Mugabe is the shame of Africa. Mugabe amemfanya Tabo Mbeki kuwa kituko kwenye diplomasia ya kimataifa na hata nyumbani kwake South Africa. Kwa kifupi Mugabe amepoteza muelekeo na yupo tu kwa sababu zake binafsi na sio kwa ajili ya Zimbabwe anymore. Nadhani amepoteza uwezo wa kufikiri na kutenda rationally. Tumsaidie aondoke salama, ili Africa tupunguze aibu nyingine moja (baada ya Kenya) na tubaki na aibu za Somalia na Darfur kwa sasa.


Kweli Thabo Mbeki alionekana kituko kweli alipodai kuwa Hakuna Crisis in Zimbabwe, lakini cha kushangaza leo kabadili msimamo wake na kudai hakutakuwa na Amani Zimbabwe kama matokeo ya urais hayatatangazwa mapema. Hata wananchi wake wanamuona kituko. Si ajabu atampa Mugabe hifadhi ya kisiasa nchini kwake. Nafikiri atakuwa kamsaidia sana.
 
Mwanakijiji still bado anaamini matatizo ya Zimbabwe ni weupe,na anafikiri JK kuongelea US ni ukibaraka,kweli umeishiwa wewe na siasa zako za kizamani..hilo zee lazima liondoke tuu hata kama ni wazungu wataliondoa itakuwa vizuri sana,yaani kutoa matokeo tuu limekataa na linawafanya wananchi wawe wakimbizi kwa njaa na udikteta wake,lakini sishangai maana kina mwanakijiji wanao mpa kichwa wapo wengi

Heshima mbele mkuu.
Mimi nafikiri Mkjj yuko right kwa maana kuwa kuongelea kwenye ardhi yetu italeta sense zaidi kwa intergrity ya JK mwenyewe na nchi yetu pia. Kama unakumbuka issue ya Kenya baada ya kugundulika JK aliongea na bwana Kichaka kabla ya kwenda Kenya ilionekana JK went there kuwakilisha mawazo ya Bwana kichaka and nothing else.
Ni kweli kabisa kuwa Bwana kichaka na GB wanaitaji suport kutoka kwa mtu kama JK ili kuwakilisha ujumbe wao kwa Mugabe by any means kwa amani au kwa shari but this be done on our land.
 
Sadc didnt reach any aggreement kwa sababu statement yao ya mwisho was kuomba matokeo yatangazwe when convinient to do so na kuwaomba MDC wakubaliane na matokeo na wakubali kuwa na run off balot
 
Heshima mbele mkuu.
Mimi nafikiri Mkjj yuko right kwa maana kuwa kuongelea kwenye ardhi yetu italeta sense zaidi kwa intergrity ya JK mwenyewe na nchi yetu pia. Kama unakumbuka issue ya Kenya baada ya kugundulika JK aliongea na bwana Kichaka kabla ya kwenda Kenya ilionekana JK went there kuwakilisha mawazo ya Bwana kichaka and nothing else.
Ni kweli kabisa kuwa Bwana kichaka na GB wanaitaji suport kutoka kwa mtu kama JK ili kuwakilisha ujumbe wao kwa Mugabe by any means kwa amani au kwa shari but this be done on our land.

..nyie watu kama mnataka sense & intergrity mwambieni huyo dikteta aondoke sio kutuletea spin ya ajabu ajabu hapa,bora asemee huko huko kwa GW maana hata media itakamata kirahisi sana na kuwasha moto zaidi kuliko kuongelea swala zito kama hili kwenye media inayoishia Kimara.
 
Halafu jamani lazima tujiulize, kama Mugabe ni dikteta na ameiba kura na bado kashindwa, hii inaonyesha labda kura za haki zilikuwa 90% MDC na 10% Mugabe.

The guy has to go regardless kwa sababu wananchi wa Zimbabwe wanateseka sana.

Mugabe pse go in peace.

After Mugabe leaves, the land should also remain in the hands of Africans, maana UK na US wanataka wazungu wapewe back land, HELL NO!!!
 
Matokeo bado hayajatangazwa rasmi na chombo kinachohusika, hivyo mnategemea hawa jamaa SADC watafikia maamuzi gani?..
Nilisoma mahala kuwa Mbeki kabla hajaelekea Lusaka alipitia Harare na alikutanishwa na hiyo kamati ya kuhesabu kura...
Katika hilo yamekutwa matatizo mengi sana ambayo yalifanyika kinyume cha sheria za Upigaji kura na haikutajwa kama ni ZANU - PF waliocheza rafu ama MDC lakini kuna matatizo ambayo yanahitaji kurejebishwa kwanza.
Sasa hii iwe mchezo wa Mugabe ama nani kusitisha kutangazwa, hatuwezi kutoa hukumu zetu leo ikiwa hadi leo hii haijatangazwa mshindi kati yao.
Ni sawa na mtu kutaka kwenda simama mahakamani wakati kesi yako haijasomwa pamoja na kwamba imewasilishwa.. Tufanye subira Ukweli utakuja gundulika tu hata kama imani zetu zinatuambia Morgan ndiye mshindi..
What if Mugabe ndiye kaiba kura kibao kupitia foreign voters ambao hawaruhusiwi kulingana na sheria za Zimbabwe?..


The question is ni kwanini Mugabe atake re-count wakati hata matokeo yenyewe hayajulikani? Yeye anajua matokeo yalivyo ndio maana ameanza kusistiza recount, na ndio wenyewe walikuwa wanasistiza hata kuwepo kwa second round.
Ndugu watanzania lazima mkumbuke kuwa Mugabe is our shame, we put him to power, manokumbuka Historia mnaweza kukumbuka kuwa ni Nyerere ndio alimweka Madarakani Bob, kwa hiyo ujinga unaoendelea Zimbabwe tunastahili lawama kwa kiasi fulani, na kama ndio hivyo pia tunastahili kufanya kitu kuondoa hali hiyo.
I will be proud of JK if he will stand up and do what others have been afraid of doing!
 
I will be proud of JK if he will stand up and do what others have been afraid of doing!

Ni kweli kabisa imefika wakati wa kutuwaogopa hawa ma dikteta wanoshupalia kiti...mambo yanyoendelea Zimbwabwe ni shame kwetu sote wafrika..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom