Mphamvu
JF-Expert Member
- Jan 28, 2011
- 10,702
- 3,288
Hii ni dhahiri kuwa kuna ufujaji mkubwa wa pesa za wanachuo wa UDSM, Kampasi ya Mlimani kupitia taasisi yao ya uwakilishi, DARUSO.
Bajeti ya DARUSO iliyokuwa Mil. 78 imekuwa supplied na mil. 26 toka Utawala wa Chuo. Baada ya Viongozi wa Colleges kuchukua 25% ya fedha iliyopo kama katiba inavyosema, kikabaki kiwango ambacho kila taasisi ingepewa 22% ya bajeti yao yote.
Cha ajabu, wadau muhimu walioshiriki katika mchakato wa kuandaa bajeti hawakushirikishwa katika mchakato wa ugawaji wa fedha hiyo ambayo ilikuwa haitoshi, shughuli ikafanywa na Waziri wa Fedha na Cabinet peke yao.
pili, yakaidhinishwa malipo ya Tsh. 700'000 kwa mtu anayedaiwa kuwa ametengeneza tovuti ya DARUSO, tovuti yenyewe ni daruso.udsm.ac.tz ambayo imekuwako tangu enzi za Kipara, na sio tovuti bali ni 'link' kwenye tovuti ya chuo na hakukuwa na mpango wa tovuti kwenye vitabu vya bajeti vya DARUSO.
Mpaka sasa, BUNGE la DARUSO limelazimika kufanya shughuli zake kwa nakisi kutokana na madudu ya Baraza la Mawaziri.
Nitawajuza zaidi kadiri nitakavyopata taarifa.
Bajeti ya DARUSO iliyokuwa Mil. 78 imekuwa supplied na mil. 26 toka Utawala wa Chuo. Baada ya Viongozi wa Colleges kuchukua 25% ya fedha iliyopo kama katiba inavyosema, kikabaki kiwango ambacho kila taasisi ingepewa 22% ya bajeti yao yote.
Cha ajabu, wadau muhimu walioshiriki katika mchakato wa kuandaa bajeti hawakushirikishwa katika mchakato wa ugawaji wa fedha hiyo ambayo ilikuwa haitoshi, shughuli ikafanywa na Waziri wa Fedha na Cabinet peke yao.
pili, yakaidhinishwa malipo ya Tsh. 700'000 kwa mtu anayedaiwa kuwa ametengeneza tovuti ya DARUSO, tovuti yenyewe ni daruso.udsm.ac.tz ambayo imekuwako tangu enzi za Kipara, na sio tovuti bali ni 'link' kwenye tovuti ya chuo na hakukuwa na mpango wa tovuti kwenye vitabu vya bajeti vya DARUSO.
Mpaka sasa, BUNGE la DARUSO limelazimika kufanya shughuli zake kwa nakisi kutokana na madudu ya Baraza la Mawaziri.
Nitawajuza zaidi kadiri nitakavyopata taarifa.