Mpwa wangu anatafuta mume wa kuzaa naye!

Mh jamani kwa kweli nampa pole sana, But kama anataka kupandikiza, Hospital ipo masaki nadhani awe na kiasi cha dola 3000 tu ili apandikizwe mbegu na apate mtoto . Kuhusu mbegu sijui kama wanazo pale au unaenda na mwanaume wa mbegu.

duh pesa yote hiyo mbegu inaweza kuwa safi wadudu awajashambulia ,je ardh ikiwa mbaya na mbegu ikagoma kuchpuka watarudsha japo nusu
 
Naomba unipm nimuunganishe na kaka yangu mmoja alikuja hapa ofisini akaanza kumielezea tatizo kama hilo yeye
ni mtu mzima na hivyo anapokutana na hawa mabinti huwa anaona kama wadogo zake.
kama utaweza itakua vizuri .
Tukubali kwamba kuna kipindi kinafika unaona kwamba muda umeenda na suala kama hili linakua tatizo hasa kwa familia zetu za kiafrika,tusaidiane pale inapowezekana .
 
Mungu aliyemuumba atampa Mume kwa sababu ahadi za Mungu ni kweli na Amen, anachotakiwa ni kuwa mwaminifu kwa Mungu na majukumu aliyodhaminiwa. Kuhusu kumpata mwanamume wa kuzaa naye huo sio mpango wa Kimungu huo ni mpango mbadala ambao utamfanya atimize haja zake za kimwili zaidi na si za Kimungu. Pia kama ni mtu mwenye kazi zake ni kwanini amekubali kukaa na wazazi wake kufikia leo na hata kujihisi kukataliwa??? Hapo ameamua kuwa mtumwa hata wa fikra zake anatakiwa ajitegemee na kufanya maendeleo yake binafsi na katika kazi ya Mungu na Mungu angempa Mume sawasawa na neno lake. Asitafute mwanamume Mungu atampa kwa wakati wake lakini amtumikie Mungu.

Asante
 
Usipate Taaabu ndugu yangu. hebu nipe contact zake na utamuona anatema mate na kuchagua vyakula muda si mrefu.

Ni mtaalamu kwa wale woote wanaotaka watoto. nna watoto kama 18 sasa ambao nimewatoa kama tiba kwa wanaotaka kuzalishwa. Nipatie mapema maana sasa hivi sina mtu ambae amenibook
 
duh pesa yote hiyo mbegu inaweza kuwa safi wadudu awajashambulia ,je ardh ikiwa mbaya na mbegu ikagoma kuchpuka watarudsha japo nusu

Siku ukiamua kwenda utapata majibu yote hayo kabla hujatoa vijisent vyako!
 
Ni mtoto wa kaka yangu, na amezaliwa na kukulia Dar, mimi sikuwa karibu naye na ni msiri sana. Nimekuwa nikizungumza naye mara kwa mara lakini sio muwazi na hiyo ilitokana na yeye kujiwekea mipaka.

Amesoma hapa nchini na nje ya nchi katika moja ya nchi za Scandinavia na sasa ni mwajiriwa serikalini. Sina uhakika sana umri wake lakini naamini ana zaidi ya miaka 40. Hivi karibuni nilishikwa na udadisi na katika mazungumzo na shemeji yangu,(mama yake) alinijulisha kwamba hata yeye na kaka yangu wanashangaa binti yao kutoolewa au hata kupata mtoto. Anakiri kwamba hawajawahi kumuona na mwanaume na hana mashoga wanaofika hapo nyumbani.

Nilimdadisi iwapo waliwahi kumuuliza kuhusu kuolewa, shemeji akanijibu kwamba waliwahi kumuuliza na akajibu kwa kifupi kwamba hajapata mume na kipata atawajulisha. Lakini tangu siku hiyo akawa hana raha na akawaambia wadogo zake kwamba wazazi wamememchoka na sasa wanamnyanyasa. (anao wadogo zake wawili wa kike ambao wameshaolewa na kuzaa)

Nilitoa wazo kwamba wamshauri japo apate mtoto, ushauri ambao aliukubali kwa mikono miwili, lakini ni nani wa kuzaa naye?

Nimeshauri hatua ya kwanza ahame hapo nyumbani akapange mbali na nyumbani ili awe huru na hapo atakuwa na fursa ya kupata mwanaume japo wa kuzaa naye. Amekubali na sasa anatafuta nyumba ya kupanga.

Lakini yuko worried kama atapata mwanaume mwaminifu ambaye sio mume wa mtu japo wa kuzaa naye tu basi. Ila swali lake aliuliza iwapo hapa nchini kuna uwezekano wa kufanyiwa IFV badala ya njia ya kujamiiana. Hilo sina uhakika nalo na ndio maana nimekuja hapa kutafuta ushauri..
King'asti , BADILI TABIA , gfsonwin , Yummy , nyumba kubwa , Nehondo , MwanajamiiOne , marrykate , AshaDii , NATA , FirstLady1 , TaiJike , na wengineo ambao sijawataja, naomba msaada wenu ili nimsaidie mpwa wangu[/QUOT

Mwambie aende Nairobi wanafanya hiyo IFV (USD 4000). Kwake itakuwa nzuri sana kwa sababu hakuna usumbufu, mara baba hajaja kuona mtoto, matumizi nk. Anakufa na mwanae kwa shida na raha.
 
Usipate Taaabu ndugu yangu. hebu nipe contact zake na utamuona anatema mate na kuchagua vyakula muda si mrefu.

Ni mtaalamu kwa wale woote wanaotaka watoto. nna watoto kama 18 sasa ambao nimewatoa kama tiba kwa wanaotaka kuzalishwa. Nipatie mapema maana sasa hivi sina mtu ambae amenibook

m nimeshapanda dau achana nae tafathal
 
ninahisi huyo nduguyo ana Turner syndrome.....na ndio maana anapendekeza nji ya IFV badala ya kujamiiana
 
Tegelezeni,naamini umepata ushauri wa kutosha,la kufanya sasa ni ku print thread nzima umpe mpwa asome page hadi page kisha uone ata react vipi.
All the best.
 
Nilitoa wazo kwamba wamshauri japo apate mtoto, ushauri ambao aliukubali kwa mikono miwili, lakini ni nani wa kuzaa naye?

Nimeshauri hatua ya kwanza ahame hapo nyumbani akapange mbali na nyumbani ili awe huru na hapo atakuwa na fursa ya kupata mwanaume japo wa kuzaa naye. Amekubali na sasa anatafuta nyumba ya kupanga.

Lakini yuko worried kama atapata mwanaume mwaminifu ambaye sio mume wa mtu japo wa kuzaa naye tu basi. Ila swali lake aliuliza iwapo hapa nchini kuna uwezekano wa kufanyiwa IFV badala ya njia ya kujamiiana. Hilo sina uhakika nalo na ndio maana nimekuja hapa kutafuta ushauri..

Nimeona kuna centre moja inayojitangaza kuwa wanafanya IVF, ukitoka Mwenge kwenda Kawe kwa barabara ya mkato inayopita karibu kwa kanisa la Mama Rwakatare, ukikaribia barabara ya Old Bagamoyo. Naona ni wapya. Wameandika kwenye kibao kwenda pale ni kwa appointment tu. Kama upo nchi za nje niambie nikupe contacts zao (ie itabidi niende pale tena) . Advice yangu ni kuwa akipendelea njia hii, ni bora ajue sperm donor wake, Si vyema mtoto kuzaliwa asijue baba yake ni nani.
 
Miaka 40, lazima alishafanya ngono. Najua ni siri yake, tena na watu wengi sana. Tatizo la huyo, anataka apate mtu wa kada yake kitu ambacho huwa hakisound kwenye mapenzi/mahusiano.

Ushauri wangu ni kuwa, amtafute yule aliyezini naye kwa mara ya kwanza, na kama ameshaoa, atafute aliyefuatia ambaye hajaoa wazae watoto
 
nimeona kuna centre moja inayojitangaza kuwa wanafanya ivf, ukitoka mwenge kwenda kawe kwa barabara ya mkato inayopita karibu kwa kanisa la mama rwakatare, ukikaribia barabara ya old bagamoyo. Naona ni wapya. Wameandika kwenye kibao kwenda pale ni kwa appointment tu. Kama upo nchi za nje niambie nikupe contacts zao (ie itabidi niende pale tena) . Advice yangu ni kuwa akipendelea njia hii, ni bora ajue sperm donor wake, si vyema mtoto kuzaliwa asijue baba yake ni nani.

ndo nini?
 
Inaonekana mtu sio kamili bila kuwa na matokeo ya kupenda au kupendwa

Hata penseli ukiiweka katika glass iliyojaa maji nusu inaonekana kama (penseli) imepinda.

Usiamini kila kitu kwa sababu tu "inaonekana".

Na matokeo ya kupenda na kupendwa si lazima yawe mtoto, ingekuwa hivyo wagumba wasingependwa.
 
Mie niko tayari ila twende kwa wakili tukatengeneze mkataba. yeye anahitaji mtoto nami ninamahitaji yangu pia kama tukienda sawa tunafunga biashara
 
Mi naweza kumsaidia kwa njia ya kujamiiana tena bila cost yoyote yeye aniPM tu,Tena sirudii mara mbili only once
 
Back
Top Bottom