MP's wife condemns US embassy over visa refusal

Mtanzania, Asante kwa mtizamo wako lakini napenda kusema kwamba maelekezo yangu ni sahihi kabisa. Na masuala yote ya immigrationa nowdays yanashughulikiwa na USCIS( zamani INA). Unaweza soma hapa kuhusu masuala yote kuhusu namna mtu anavyoweza kupoteza status yake kama Legal Permanent Reisdent aka Green Card Holder. Natumaini itakupa mwanga kidogo. :Now That You Are A Permanent Resident

Shadow,

Asante kwa link. Nimeiangalia na naona iko clear na inafanana kabisa na kwa nchi za Europe. Wache niweke hapa chini ili kila mtu asome:

You may be found to have abandoned your permanent resident status if you:

-Move to another country intending to live there permanently.
-Remain outside of the US for more than one year without obtaining a reentry permit or returning resident visa.
-However in determining whether your status has been abandoned any length of absence from the US may be considered, even if it is less than one year.
-Remain outside of the US for more than two years after issuance of a reentry permit without obtaining a returning resident visa.
-However in determining whether your status has been abandoned any length of absence from the US may be considered, even if it is less than one year.
-Fail to file income tax returns while living outside of the US for any period.
Declare yourself a "nonimmigrant" on your tax returns.


Kwa mfano kama huyo mama alirudi TZ kimoja na bwanake, automatically alipoteza hiyo green card status. Kama anataka kurudi USA kwa muda mfupi lazima aombe visa. Kama anataka kurudi kuishi kimoja USA angeweza kuomba returning resident visa na kama bado ana uhusiano na USA wanaweza kumrudishia. Uhusiano huo ni pamoja na kuwa na familia kule, nyumba nk.

Kwa watu walio wengi, wanachofanya ni kuendelea kujifanya wanaishi USA kumbe wamerudi kwao na wanatembelea USA mara moja moja. Watu wengi wanafanikiwa kwa kutumia njia hiyo. Ila tatizo lake unaweza kuingia matatizoni kwa kushindwa kulipa kodi au kushindwa kutimiza sheria zingine za nchi. Hapo ndio ukweli hujulikana na jambo dogo hugeuka kubwa.

Kwa mawazo yangu mimi naona huyo mama kwa kujua sheria aliachia hiyo green card bwanake alipopata ubunge. Ukiwa mwanasiasa au familia ya mtu anayetaka kuwa mwanasiasa inabidi uwe mwangalifu sana na haya mambo. Usije ukaishia kuwa kama yule kijana wa Mathayo ambaye aliendelea kupata mshahara kule Botswana hata baada ya kuondoka.

Hata ukiendelea kuwa na green card na mpakani wakagundua umerudi kwenu kimoja, wanaweza kuku deport hapo hapo kwa kukosa visa.

Ushauri ambao watu wengi wenye case kama huyu mama wanapewa kwenye hizi forums za immigration ni kwamba omba visa ili mkukwepa usummbufu mpakani.


Susuviri, kuhusu mahali pa kuombea, inatakiwa iwe pale ambapo unaishi. Kama unaishi hapo kwa muda mfupi ni kweli wanakuambia ukaombee kwenu. Lakini kama una haki ya kuishi hapo kwa muda mrefu, kwa mfano una visa ya kuolewa, una PR, hapo ni main residence yako nk. unaruhusiwa kuombea kwenye nchi hiyo hiyo. Huyo jamaa yako atakuwa alikuwa na visa ya muda mfupi au mwanafunzi na labda alikuwa naomba kwenda USA kwa visa ya muda mrefu, hapo watakuambia nenda kaombee kwenu.

Kwa case ya huyu mama naamini alikuwa na haki ya kuombea Dar au Nairobi. Labda kwasababu ya kuwa Arusha akaona aende Nairobi kwao na confidence kubwa, akakutana na vichaa hao wa ubalozi.

Cases kama hizi jamani ziko nyingi sana na huwa inaudhi sana. Huyu mama angelikuwa na muda angeweza ku appeal na kushinda lakini case yake ndio hivyo, kashindwa kwenda kumuona mtoto wake dakika za mwisho. Inasikitisha sana.

Wacha tusubiri ubalozi watasema nini.
 
Mtanzania

Unawezaje kuishi USA kwa kufuata sheria "green card" miaka 20 halafu "uamue" kurudi Tanzania "moja kwa moja" kwa maana ya kwamba hata mtoto wako akiwa icu ushindwe kuingia kwenda kumuona..!!?? Hili mimi haliniingii akilini...

Mkuu Yebo Yebo,

Inawezekana kabisa, huyu mama sio wa kwanza wala hatakuwa wa mwisho. Kama unataka kukwepa usumbufu huo basi omba uraia. Green card inakusaidia tu kama unaishi muda wote
kwenye hiyo nchi.

Ukiamua kurudi kwenu kwa muda mrefu kutumia green card ni risky.

Ukiwa na muda uwe unatembelea hapa: Immigrationboards.com :: Index

na unaweza kujifunza mengi na kuzuia usumbufu. Wakati mzuri wa kununua insurance ni wakati huihitaji.
 
Wale siyo wajinga aisee. They know better than you think you do! Lazima kuna tatizo hapo. Kwanza, hata ukiwa national wa wapi, VISA unaweza omba popote penye Embassy. Namshangaa huyu kukimbia Dar na kusema ati kwa kuwa ni Kenyan ndiyo akaenda kule?! Huyo mtoto wake ni raia wa wapi? USA, Kenya au Tanzania? I she legally staying in USA? Halafu, hai-click kichwani, mke wa mbunge wa huku Tanzania then anadai yeye ni Kenyan National..,,?!

Lazima kuna fool play anijua yeye mwenyewe kwa kina. Tusirukie issues. Wale jamaa wako makini sana, ingawaje unaweza wachanganya kirahisi sana.

Mkuu,
nakusikia sana..na ndio nikasema there is more than what we have been told as reasons for the refusal.I was being polite here maana i didnt want to say much more than what I wanted to.
Pili -- kenyan married to a former TZ MP......OFCOURSE KUNA KITU!
 
Maiti ya mtoto wa mbunge yazua mzozo (Tanzania Daima)
na Ramadhani Siwayombe, Arusha

MAZISHI ya Angela Mrema, mtoto wa Mbunge wa Arusha Mjini, Felix Christopher Mrema, aliyefariki dunia wiki mbili zilizopita nchini Marekani, yamekwama kwa siku ya 16 sasa kutokana na mvutano wa wazazi.

Mazishi ya mtoto huyo aliyefariki dunia Desemba 17, yamekwama baada ya kuibuka kwa mvutano wa kifamilia kati ya mbunge huyo na mtalaka wake, Milcah, mama mzazi wa marehemu.

Akizungumza na Tanzania Daima jana mjini hapa, mama wa marehemu alikiri kuwa hadi sasa mazishi ya binti yake yamekwama kutokana na mvutano huo wa kifamilia.

Alisema anashangazwa na uamuzi wa mzazi mwenzake (Mrema) kukataa kurejesha maiti ya binti yao na kufanya mazishi nchini na badala yake anataka azikwe Marekani ili mkewe wa sasa, asichukie.

‘Mpaka sasa licha ya kufiwa na mwanangu, siruhusiwi kufika nyumbani kwa Felix ambaye ni mzazi mwenzangu na kuamriwa wageni wanaotaka kunipa pole wafike katika nyumba ya kupanga ninayoishi, eneo la Haile Selassie huku yeye akiwa anaendelea na msiba nyumbani kwake, kwa kweli huko ni kutonitendea haki kama binadamu na mzazi,"' alilalama mama huyo.

‘Nimeshangazwa sana na hali hii inaonyesha mzazi mwenzangu ambaye kisheria za dini bado ni mume wangu kwa kuwa tulifunga ndoa kanisani, kukubali mawazo yanayochelewesha mazishi ya mtoto wetu," alisema Milcah.

Milcah aliendelea kusema kuwa mtoto wao lazima azikwe nchini, kwani haoni sababu za kutosafirisha mwili wa marehemu wakati fedha za kusafirisha mwili huo zipo.

Aidha, alibainisha kuwa baada ya kukataa mwanawe azikwe Marekani, hivi sasa mzozo unaoendelea kati yake na Mrema ni wapi mahala pa kufanyia mazishi.

Alipopigiwa simu na Tanzania Daima kuzungumzia tatizo hilo, mbunge huyo alikataa kuzungumzia kwa undani mzozo huo, kwa madai kuwa ni mambo ya kifamilia, hivyo hapaswi kuzungumza kwenye vyombo vya habari.

Alikiri kuwa hadi sasa mazishi hayajafanyika na kuongeza kwamba wakati utakapofika jamii itajua.

"Ndugu yangu hayo ni mambo ya kifamilia…hivi sasa tupo katika msiba, nina majonzi makubwa, hivyo siwezi kuzungumzia masuala hayo magazetini kwani ni mambo ya ndani ya familia," alisema Mbunge Felix.

Mtoto huyo wa mbunge wa Arusha Mjini, Angela Mrema, alifariki nchini Marekani Desemba 17 mwaka jana akiwa katika chumba cha upasuaji, baada ya kupata ajali ya gari Desemba 7 mjini Arusha.

Katika ajali hiyo, Angela alivunjika nyonga na mguu na kulazimika kufanyiwa upasuaji wa mwanzo na kuwekewa chuma. Alifariki dunia wakati akifanyiwa upasuaji wa pili nchini Marekani.
 
Mkewe wa sasa ni wa taifa gani? Mmarekani? Inawezekana kweli jamaa alimchomea mama watoto wake ubalozini kuwa si mkewe? Kama ni kweli haya yanayoandikwa basi amejidhalilisha. Ugomvi wake na mzazi mwenzake haustahili kuingizwa kwenye msiba wa mtoto wao!

Amandla......
 
Fundi,

Hao ndio wanasiasa wetu, wanashindwa kutatua matatizo yao ya ndani, je wataweza vipi kutatua matatizo ya Watanzania?
 
Mi sioni la kushangaza hapo, wanajiona miungu watu hao....Mbona kukukatalia ni kitu cha kawaida tu......mimi nasuggest kuwe na some sort of refund kama wakikukatalia visa, then tuwaone kama watakuwa kama walivyo sasa...sitoshangaa pia kama walimpakia na matusi on her way out.....
 
Mi sioni la kushangaza hapo, wanajiona miungu watu hao....Mbona kukukatalia ni kitu cha kawaida tu......mimi nasuggest kuwe na some sort of refund kama wakikukatalia visa, then tuwaone kama watakuwa kama walivyo sasa...sitoshangaa pia kama walimpakia na matusi on her way out.....

Zamani ilikuwa unalipia viza inapokubaliwa. Wakashtuka. Sasa unatanguliza mpango. Na kila appeal na mpango wake! Ukiangalia tunavyogombea kwenda kwao, huu ni mradi mzuri. Na safi zaidi ni kwamba hawalzimiki kutoa sababu ya kukutalia viza!

Hivi baba wa marehemu aliwahi kwenda kumtazama mwanae? Kama hakuwahi, itakuwaje adai azikwe alikofia (kama ni kweli)? Kama bajeti inagomba basi heri wamchome, wagawane majivu! Huku kulumbana kutawafanya wengi wakose imani na mheshimiwa.
 
guyz, slow down and get it, she is an ex-wife, that explains it all. So huyo mama ni kivyake in real life.
 
Hivi mbona watu wanashindwa kumaliza mambo ya kifamilia kwa busara?! Soon aibu itawakuta pale mambo yatakapoanza kuwekwa hadharani na kufaidisha hata wale wasiohusika.Inahuzunisha hasa unapoona kiongozi kama huyu bwana mwenye kujua hata sheria zinasema nini kuhusu talaka, wajibu na stahili aki behave kama layman!Mengi yatafichuliwa!
 
Hivi mbona watu wanashindwa kumaliza mambo ya kifamilia kwa busara?! Soon aibu itawakuta pale mambo yatakapoanza kuwekwa hadharani na kufaidisha hata wale wasiohusika.Inahuzunisha hasa unapoona kiongozi kama huyu bwana mwenye kujua hata sheria zinasema nini kuhusu talaka, wajibu na stahili aki behave kama layman!Mengi yatafichuliwa!

Ukificha maradhi, msiba utakuumbua. Sasa hii familia walishindwa kufikia muafaka wa kuakikisha marehemu anapumzishwa kwa amani. Pili, hakuna chama cha watanzania walioko huko California na maeneo ya karibu kusaidia katika kusafirisha mwili wa huyu marehemu kwenda kwa mama yake? Au kwa sababu ni mtoto wa kigogo? je tuite ni kunyanyapaa?
 
Ukificha maradhi, msiba utakuumbua. Sasa hii familia walishindwa kufikia muafaka wa kuakikisha marehemu anapumzishwa kwa amani. Pili, hakuna chama cha watanzania walioko huko California na maeneo ya karibu kusaidia katika kusafirisha mwili wa huyu marehemu kwenda kwa mama yake? Au kwa sababu ni mtoto wa kigogo? je tuite ni kunyanyapaa?
Unaponogewa na "mambo ya nyumba ndogo uzeeni"..makubwa yatakupata tu!
Inabidi utumie busara ku balance mambo vinginevyo dunia itakucheka.
 
Unaponogewa na "mambo ya nyumba ndogo uzeeni"..makubwa yatakupata tu!
Inabidi utumie busara ku balance mambo vinginevyo dunia itakucheka.

WoS, Inabadi tubadili mwenendo.. hizi 'nyumba ndogo' ni kama uzuri wa mkakasi lakini ndani kipande cha mti.
 
Back
Top Bottom