Mponye mpenzi wako kwa kumtendea haki

mtishbieliya

Senior Member
Oct 16, 2014
130
116
TAFADHALI KUWA NA HURUMA.

Sio sawa kabisa kuingia katika mahusiano na mtu na kumfanya atengeneze hisia za kukupenda wewe, kumfanya mtu aamini kuwa wewe ni wa tofauti na wale wote ambao wamekwisha muumiza kihisia hapo mwanzo.

Anakuamini na anakukabidhi moyo, mapenzi na mwili wake, anakutegemea wewe, anapanga kesho yake pamoja na wewe, ana sucrifice kile kidogo alicho nacho kwa ajili yako.

Anajivunia kuwa na wewe kiasi cha kukutambulisha kwa familia yake na marafiki zake wote wa mbali na wa karibu, anabadilisha tabia yake kwa ajili yako, anaacha tabia zake fulani kwa ajili yako.

Muda mwingine anapoteza kazi fulani kukufuata wewe huko unakoishi kwa ajili ya wewe, anakuwa na maadui kwa ajili yako na anatukanwa na watu kwa ajili yako.

Wewe kwa ujinga wako au kwa ujinga juu ya jambo la kipumbavu, unamuacha yeye au unamtelekeza au unamuumiza kihisia, haumpendi tena. Unasahau ni yepi amepitia au mlipitia pamoja. Umesahau ahadi nono ulizomueleza hapo mwanzo, umesahau kila kitu kabisa

Unaanza kumuona ni mpumbavu na ni mbaya kiasi gani, unaanza kumuita majina ya ajabu ajabu na kumtukana matusi ya nguoni, unakana mbele yake na kumwambia watoto si wako

Sio sawa ndugu yangu, inaumiza mno, ni maumivu makali sana moyoni, moyo unavuja damu, maumivu hayaponi kirahisi. Unaweza kuwa umefanya hivyo kwa kuwa na wewe ulifanyiwa hivyo kipindi cha nyuma na watu wengine ila sio busara kumfanyia mwenzako ambae hana hatia.

Unaweza ukachukulia kama ni mchezo fulani. Ila amini me nakwambia MUNGU hana furaha na hicho ulichokifanya na wewe pia.

Tafadhali sana nimejifunza kamwe usimfanye mtu akupende katika mahusiano wakati unajua kwamba haumpendi na hautadumu nae siku zote. Kamwe usimpumbaze mtu au kumtumia kwa faida zako.

Kuwa na huruma na huo moyo wa mpenzi wako uliojaa mapenzi na ambao hauna hatia masikini ya Mungu. Bila shaka unanisoma hapa, nenda ukamwambie ukweli kuhusu mustakabari wa mahusiano yenu. Nenda tafadhali, mueleze ukweli! Usimfiche, usiendelee kumdanganya na kumpa ahadi kedekede wakati unaona kabisa hilo jambo haliwzekani.!

Onyesha hekima yako angalau mara moja tu sasa hivi na Mungu atakubariki.

Dah inauma sana!

Share

Mwl Tweve Hezron
 
Ukiona unafanya hivyo jichunguze utakuwa ni mgeni ktk ulimwengu wa mapenzi.kwenye usiingize miguu yote kwa kupima urefu wa bahari utazama utapolea huko uwe chakula y samaki.dishwaaaa
 
TAFADHALI KUWA NA HURUMA.

Sio sawa kabisa kuingia katika mahusiano na mtu na kumfanya atengeneze hisia za kukupenda wewe, kumfanya mtu aamini kuwa wewe ni wa tofauti na wale wote ambao wamekwisha muumiza kihisia hapo mwanzo.

Anakuamini na anakukabidhi moyo, mapenzi na mwili wake, anakutegemea wewe, anapanga kesho yake pamoja na wewe, ana sucrifice kile kidogo alicho nacho kwa ajili yako.

Anajivunia kuwa na wewe kiasi cha kukutambulisha kwa familia yake na marafiki zake wote wa mbali na wa karibu, anabadilisha tabia yake kwa ajili yako, anaacha tabia zake fulani kwa ajili yako.

Muda mwingine anapoteza kazi fulani kukufuata wewe huko unakoishi kwa ajili ya wewe, anakuwa na maadui kwa ajili yako na anatukanwa na watu kwa ajili yako.

Wewe kwa ujinga wako au kwa ujinga juu ya jambo la kipumbavu, unamuacha yeye au unamtelekeza au unamuumiza kihisia, haumpendi tena. Unasahau ni yepi amepitia au mlipitia pamoja. Umesahau ahadi nono ulizomueleza hapo mwanzo, umesahau kila kitu kabisa

Unaanza kumuona ni mpumbavu na ni mbaya kiasi gani, unaanza kumuita majina ya ajabu ajabu na kumtukana matusi ya nguoni, unakana mbele yake na kumwambia watoto si wako

Sio sawa ndugu yangu, inaumiza mno, ni maumivu makali sana moyoni, moyo unavuja damu, maumivu hayaponi kirahisi. Unaweza kuwa umefanya hivyo kwa kuwa na wewe ulifanyiwa hivyo kipindi cha nyuma na watu wengine ila sio busara kumfanyia mwenzako ambae hana hatia.

Unaweza ukachukulia kama ni mchezo fulani. Ila amini me nakwambia MUNGU hana furaha na hicho ulichokifanya na wewe pia.

Tafadhali sana nimejifunza kamwe usimfanye mtu akupende katika mahusiano wakati unajua kwamba haumpendi na hautadumu nae siku zote. Kamwe usimpumbaze mtu au kumtumia kwa faida zako.

Kuwa na huruma na huo moyo wa mpenzi wako uliojaa mapenzi na ambao hauna hatia masikini ya Mungu. Bila shaka unanisoma hapa, nenda ukamwambie ukweli kuhusu mustakabari wa mahusiano yenu. Nenda tafadhali, mueleze ukweli! Usimfiche, usiendelee kumdanganya na kumpa ahadi kedekede wakati unaona kabisa hilo jambo haliwzekani.!

Onyesha hekima yako angalau mara moja tu sasa hivi na Mungu atakubariki.

Dah inauma sana!

Share

Mwl Tweve Hezron
Nadhani kupenda kusiwekezwe eneo moja, penda vingi vingi kama hela, chakula, magari n.k
 
Yaani kupenda hela, gari na chakula ufananishe na kumpenda bae umpendae? Mbado hujawahi penda Wewe!!!
Unamwambia bae,"nakupenda kama soda ", kwa sehemu kubwa hivyo ndo ambavyo wanaume wengi wanapenda unaweza kupendwa kama gari hata ukiumwa anaweza asije kukuona ila gari likichubuliwa rangi kidogo anapatwa na high bp.
 
Back
Top Bottom