Mponda: Nitajiuzulu kuepusha vifo na si shinikizo la madaktari!

nasikitika kuwa mmoja wa watanzania wa miaka hamsini ya uhuru,bora ningezaliwa 1910 nikapigana vita vya dunia nikashiriki kuikomboa nchi halafu nikafa 1967.

ningeungana na akina che guavaranmartin luther king,tito okelo,patrice lumumba katika historia.
ila kuzaliwa miaka hii sijui historia ita kaaje na hawa magamba?
 
mponda angejiuzulu wiki kadhaa zilopita ingefaa zaidi. vipi lucy yeye bado anajivinjari?
 
Linalonishangaza ni hili la viongozi vilaza kumchukulia kila anayedai haki yake kuwa amehamasishwa kisiasa!!!!!!!!
 
Waziri wa Afya Dr Haji Mponda amesema yeye atajiuzulu ili kuokoa roho za watanzania ambao wataathirika na mgomo mpya wa madaktari na si kwa shinikizo! Hayo aliyasema jana usiku kwenye kikao cha dharura cha baraza la mawaziri cha kujadili mgomo mpya wa Madaktari na Manesi! Hata hivyo Mponda ametoa rai kwamba watanzania wawe makini sana na jinsi watu wanavyotumia migogoro kwa maslahi yao binafsi huku wakisababisha maafa makubwa kwa raia wasio na hatia. Na kusema kuwa kama wana taaruma wakiingia kwenye ushabiki wa siasa nchi itaingia kwenye mgogoro mkubwa na kudhoofisha ustawi wa taifa letu!

Maneno ya hekima.

Matatizo ya Wizara ya Afya hayajaanza awamu ya Mponda kinachoonekana hapa ni kwamba Mponda amerithi matatizo lakini anaonekana ndiye mwanzilishi wake.


Prof David Mwakyusa ni prof katika fani ya tiba ni nani alijua angeweza kushindwa kuleta mabadiliko ya sekta ya Afya?

Tuna safari ndefu ya kutafuta chanzo cha kweli cha matatizo yanayoikumba wizara ya Afya na ndipo tutajinasua na migogoro hii.
 
Kama ni kujiuzulu ili kuepusha vifo mbona kwenye mgomo wa kwanza hakujiuzulu
 
Twende mbele turudi nyuma; hivi Dr. Mponda akijiuzulu kuna uhakika gani kwamba sekta ya afya itaboreshwa? Au ni kwamba tu ajiuzulu kuondoa kiwingu? Akija mwingine na sekta ya afya isiiboreke naye ataambiwa ajiuzulu? Watumiaji wa umeme tutamtaka waziri wa nishati ajiuzulu kwa kuwa sekta ya nishati si nzuri; itafuatia waziri wa elimu; kisha kwa kuwa kuna watoto wa mitaani wengi basi waziri wa watoto na jinsia naye atatakiwa ajiuzulu? Nadhani suala si waziri suala ni mfumo.
 
Kama ndivyo, kimbelembele cha nini! Tunawezaje kukuchukulia wewe kama reliable source bila kutaja au kuweka hata nakala ya gazeti kama umeitoa huko!! Wewe hujiulizi kwa nini threads zingine haziulizwi chanzo na yako inaulizwa na zaidi ya mtu mmoja!!! Wewe bweg e kweli!!

Tomaso!
 
mpaka ashinikizwe ndo ajiuzulu, alikuwa wapi mda wooote huo. jamni WaTZ tuwe na huruma basi hat kidogo tu inatosha.
 
Hii inji ina matatizo makubwa sana, kinachomfanya Mponda asijiuzuru hadi leo ni security. Akitoka tu uwazirini kuanzia kesho ni njaa tu kwa kuwa hajawahi kuishi kwa kujitegemea, zaidi ya kuitegemea serikali toka azaliwe. Arudi kugombea posho za ubunge atuachie ofisi yetu
 
Kama ni kocha basi kikwete ni arsenal wenger.....mpaka arsenak ishuke daraja ndio atanunua wachezaji......
 
Mzizi vipi kuhusu Lucy Nkya nae atafuata nyayo za boss wake au atakomaa? Ikiwa hicyo Dr. Haji Mponda atakuwa amejijengea heshima mbele ya jamii ya watanzania.
 
Huu mgomo wa Madaktari naona utanukia East Africa kwa ujumla! Nimeona Kenya nao Madaktari ngoma ni droo kati yao na Serikali yao jana!
 
Niandike inasemekana wakati muhusika ndio amesema hivyo? We vipi? Au ndio mmezoea udaku! Kama wewe ni Tomaso basi subiri hadi mwisho umuone Mponda anatangaza kwenye TV kwa macho yako kesho!

Udaku unapoletwa kwa great thinkers.
 
Twende mbele turudi nyuma; hivi Dr. Mponda akijiuzulu kuna uhakika gani kwamba sekta ya afya itaboreshwa? Au ni kwamba tu ajiuzulu kuondoa kiwingu? Akija mwingine na sekta ya afya isiiboreke naye ataambiwa ajiuzulu? Watumiaji wa umeme tutamtaka waziri wa nishati ajiuzulu kwa kuwa sekta ya nishati si nzuri; itafuatia waziri wa elimu; kisha kwa kuwa kuna watoto wa mitaani wengi basi waziri wa watoto na jinsia naye atatakiwa ajiuzulu? Nadhani suala si waziri suala ni mfumo.

Mkuu Kimbunga sasa ni nani wa kuongoza hiyo safari? Imefika hali sasa kila mtu kwa umoja wake aamue kuwa sehemu ya mabadiliko!
 
Back
Top Bottom