OSOKONI
JF-Expert Member
- Oct 20, 2011
- 10,965
- 5,336
Kukimbilia kujiuzulu siyo suluhu sana ya tatizo. Kwasababu kama ni hivyo, watu wanaweza kuharibu mambo kwa maksudi wakitegemea watajiuzulu na kukaa pembeni."
Alieleza kwamba hadi jana jioni, hakuwa na uamuzi wowote kuhusu hilo na alikuwa akiendelea na majukumu yake kama kawaida huku akisisitiza;
"Unajua mtu anaweza kufikiria zaidi kujiuzulu kama atakuwa amefanya au amesababisha kitu na yeye mwenyewe nafsi yake ikathibitisha hilo. "
Alisema binafsi, ameguswa na mgomo huo wa madaktari ambao umeathiri huduma za afya nchini, huku baadhi ya watu wakipata madhara zaidi ya maradhi.
Lakini, alipoulizwa kwamba kutokana na hali hiyo, haoni kwamba alipaswa kuwajibika kwa kujiuzulu kama sehemu ya kuumizwa na madhara yaliyowapata Watanzania kutokana na Wizara yake alijibu; "Naomba ni reserve(nihifadhi) kauli yangu katika hilo. Lakini, nani wanataka nijiuzulu, ni wewe (mwandishi) au nani? Maana sijasikia hilo unalosema. Nikisikia nitaamua."
Alifafanua kwamba kuwajibika wakati mwingine baadhi ya watu wamekuwa wakitafsiri dhana hiyo tofauti .
"Kwa mfano, mimi nimeguswa sana na mgomo wa madaktari, nawapenda sana Watanzania, sasa hapo kuna tofauti kidogo."
Dk Mponda alisema ndiyo maana alikuwa akifanya jitihada zote kuhakikisha anakutana na madaktari hao kuhakikisha mgomo huo unamalizika, lakini bahati mbaya juhudi hizo hazikufanikiwa haraka.
"Kwakweli nimeguswa sana na mgomo huo wa madaktari, ndiyo maana nimekuwa nikifanya kila jitihada kuhakikisha unamalizika, lakini bahati mbaya hilo halikutokea. Kwa hiyo, nimeumia sana," alisisitiza Dk Mponda, baada ya kuulizwa tena kwamba kama ameguswa ni kwanini asiwabijike kwa kujiuzulu hata kama hakutenda kosa.
Alisema anatambua umuhimu na dhana ya uwajibikaji, lakini akasisitiza kuwa "Siwezi kusema zaidi kwa sasa. Wakati ukifika nitaweza kuzungumza."
Alieleza kwamba hadi jana jioni, hakuwa na uamuzi wowote kuhusu hilo na alikuwa akiendelea na majukumu yake kama kawaida huku akisisitiza;
"Unajua mtu anaweza kufikiria zaidi kujiuzulu kama atakuwa amefanya au amesababisha kitu na yeye mwenyewe nafsi yake ikathibitisha hilo. "
Alisema binafsi, ameguswa na mgomo huo wa madaktari ambao umeathiri huduma za afya nchini, huku baadhi ya watu wakipata madhara zaidi ya maradhi.
Lakini, alipoulizwa kwamba kutokana na hali hiyo, haoni kwamba alipaswa kuwajibika kwa kujiuzulu kama sehemu ya kuumizwa na madhara yaliyowapata Watanzania kutokana na Wizara yake alijibu; "Naomba ni reserve(nihifadhi) kauli yangu katika hilo. Lakini, nani wanataka nijiuzulu, ni wewe (mwandishi) au nani? Maana sijasikia hilo unalosema. Nikisikia nitaamua."
Alifafanua kwamba kuwajibika wakati mwingine baadhi ya watu wamekuwa wakitafsiri dhana hiyo tofauti .
"Kwa mfano, mimi nimeguswa sana na mgomo wa madaktari, nawapenda sana Watanzania, sasa hapo kuna tofauti kidogo."
Dk Mponda alisema ndiyo maana alikuwa akifanya jitihada zote kuhakikisha anakutana na madaktari hao kuhakikisha mgomo huo unamalizika, lakini bahati mbaya juhudi hizo hazikufanikiwa haraka.
"Kwakweli nimeguswa sana na mgomo huo wa madaktari, ndiyo maana nimekuwa nikifanya kila jitihada kuhakikisha unamalizika, lakini bahati mbaya hilo halikutokea. Kwa hiyo, nimeumia sana," alisisitiza Dk Mponda, baada ya kuulizwa tena kwamba kama ameguswa ni kwanini asiwabijike kwa kujiuzulu hata kama hakutenda kosa.
Alisema anatambua umuhimu na dhana ya uwajibikaji, lakini akasisitiza kuwa "Siwezi kusema zaidi kwa sasa. Wakati ukifika nitaweza kuzungumza."