usimchangie, na kwa nini akuombe mchango? anataka kuona feelings zako zikoje...ki ukweli nadhani bado utakuwa unampenda (speaking from experience)...huyo hana lolote anataka kukuumiza....mpotezee
Msitudanganye bado mnapendana sana na wewe una ka wivu ndio maana hutakikuchanga. Changa tu uwe nae karibu na mwanandoa wake akumaki vizuri siku ya arusi........na baadae aje akutoe meno umenielewa?.Wakuu.
Niliwahi kutoa sredi hapa kwamba nilikuwa na mpenzi wangu ambaye alikuwa wa kwanza nilikutana naye nikiwa chuo tukaachana siku ya wapendanao..Jamaa yangu huyu anatarajia kufunga pingu za maisha mwezi wa tano mwaka huu.Siku chache zilizopita alinipigia simu na kuniambia kwamba anatarajia kufunga pingu za maisha na kuniomba nimchangie ili kufanikisha harusi yake.ikumbukwe kwamba hatkumalizana vizuri na huyu jamaa ingawa amekuwa akilazmisha mara nyingi kwamba tuwe best friends,hili alilisema hata wakati tunaachana lakini kwangu mimi niliona ni upuuzi,sikujisikia kuwa karibu naye hasa kirafiki ingawa tumekuwa tukiwasiliana kwa njia ya simu mara moja moja kila mtu akimkukmbuka mwenzake.Nilimueleza bila kuficha kwamba sitamchangia hata senti moja kwani sijisikii kufanya hivyo.Ikumbukwe kuwa tuliachana tukiwa hatujagombana hata kidogo wala kuwa na makosa ya kupelekea kuachana.
Naombeni ushauri nafanya vibaya kutomchangia?
Nyani ungeweka hivi changia ili siku akiboreka na huyo mke wake basi ye ndo litakuwa chaguo ingawa sitapenda huyu binti arudishe tena majeshi huko ambako alipata majeraha ya moyo.Namshauri tu mie ndo niwe kimbilio lake.Wewe changia tu bana...huwezi jua....anaweza akakupa tena ummege siku akiboreka na huyo mumewe mpya
Wakuu.
Niliwahi kutoa sredi hapa kwamba nilikuwa na mpenzi wangu ambaye alikuwa wa kwanza nilikutana naye nikiwa chuo tukaachana siku ya wapendanao..Jamaa yangu huyu anatarajia kufunga pingu za maisha mwezi wa tano mwaka huu.Siku chache zilizopita alinipigia simu na kuniambia kwamba anatarajia kufunga pingu za maisha na kuniomba nimchangie ili kufanikisha harusi yake.ikumbukwe kwamba hatkumalizana vizuri na huyu jamaa ingawa amekuwa akilazmisha mara nyingi kwamba tuwe best friends,hili alilisema hata wakati tunaachana lakini kwangu mimi niliona ni upuuzi,sikujisikia kuwa karibu naye hasa kirafiki ingawa tumekuwa tukiwasiliana kwa njia ya simu mara moja moja kila mtu akimkukmbuka mwenzake.Nilimueleza bila kuficha kwamba sitamchangia hata senti moja kwani sijisikii kufanya hivyo.Ikumbukwe kuwa tuliachana tukiwa hatujagombana hata kidogo wala kuwa na makosa ya kupelekea kuachana.
Naombeni ushauri nafanya vibaya kutomchangia?
Pia anaweza kumchangia na aisende tu,sidhani hata kama kuna haja ya kuomba ushauri katika hili.......Hasa ukizingatia waliachana kwa amani
Uamuzi uko mikononi mwako!!!Great thoughts umepewa...choose wisely!1.
yeye kaomba umchangie-kama una uwezo wa kuchanga, mchangie kwa msingi wa ombi lake na kulingana na uwezo wako, usije ukalaza watu wa nyumbani mwako na njaa kwa sababu ya kuchangia harusi hii, kumbuka kila aombaye hupokea, je tukiwasaidia wale tu walio wapenzi wetu, tutapata ama kustahili thawabu gani ya ziada? mafarisayo na wenye dhambi na watu wa mataifa nao hawafanyi hivyohivyo? hakika haki yetu lazima ipite haki ya mafarisayo, watoza ushuru na wenye dhambi, vinginevyo hatuwezi kuurithi ufalme wa Mungu.
2.
ushinde ubaya kwa wema-kwa kuwa unakiri kuwa hukumkosea, lakini bado Mungu anampa fursa na ujasiri wa kukutafuta na kuomba umuunge mkono au umsaidie, kumbuka unapaswa kuushinda ubaya kwa wema. kwa wema wako atatambua kosa lake la kumkataa mke mwema na pamoja na kuwa huna tena nafasi kwake, lakini atayasimulia matendo yako makuu siku zote za maisha yake na kufanyika baraka mlangoni mwako maisha yake yote na hivyo Mungu kutukuzwa kupitia maisha yako.
3.
kushiriki ama kutoshiriki harusi nashauri usikilize dhamiri yako inataka nini. mimi ningeshauri ushiriki kama na nafasi na usiwe kwazo katika shughuli yao ile kwa namna yoyote bali ufanyike baraka. si mbele yake bali mbele za Baba yetu aliye mbinguni. atakapoziona baraka kupitia kwako, atamshukuru Mungu na kumuinua siku zote za maisha yake na ataamini kuwa kweli wewe ni mtoto wa Mungu kwani unakata mashauri kwa jinsi ya Mungu na si kwa jinsi za wanadamu. kumbuka tena mpendwa kuwa haki yako mbele za Mungu lazima ipite haki ya afarisayo na wenye dhambi ili kustahili thawabu
Nakubaliana na wewe.Sikuhukumu, ila wewe dada unaonekana bado unam-mind jamaa. Achana naye bana. Huna sababu hata ya kuwasiliana naye. nakushauri usimchangie hata thumuni. Ujue pepo wake mwovu anakunyemelea. Ukimwendekeza kidogo tu unajikuta umekuwa mke wa pili au nyumba ndogo yake. Achana naye huyo. Si riziki yako. Usikubali kubembelezwa kama mtoto mchanga kupewa pipi, bazoka, sukari gulu; sijui nini! Kata bomba la mawasiliano ya kawaida, labda bakisha sala tu: mwombee kwa Mungu. Kazi kwako mamaa!
An eye for an eye makes the whole world blind!Nakubaliana na wewe.
Naona wachangiaji wanapuuzia ukweli kwamba mleta mada hayupo comfortable na huyu muoaji kutokana na experience yake mwenyewe, kwamba alicheza na feelings zake na kumuacha kwenye mataa siku ya wapendanao. This guy is an a$$hole, he couldn't find a better day ya ku-break up.
Ningekuwa mie he wouldn't see aint no nickel from me.
Ukimchangia au usipomchangia, yote ni sawa. It has to come from the heart. Labda yeye anakutest tu. But to show you are so over him and that he is yesterday's news - mchangie.
Personal or shared experience Preta?usimchangie, na kwa nini akuombe mchango? anataka kuona feelings zako zikoje...ki ukweli nadhani bado utakuwa unampenda (speaking from experience)...huyo hana lolote anataka kukuumiza....mpotezee