vkeisy2006
JF-Expert Member
- Mar 26, 2010
- 229
- 99
Kuna kitu kinanichanganya sana, hakinihusu mimi lakini kinawahusu watu muhimu sana kwangu, nina marafiki wawili, na ni wamama wenye familia zao na nimajirani zangu, ss mmoja kati yako anatembea na mume wa mwenzie wakati wote wawili ni mashoga zangu, ila huyo anaeibiwa hajui kama huyu rafiki yangu mwingine anamchukuwa mumewe, na huwa anamchekea kabisa na kujifanya rafiki yake, wanaongea vizuri sana,
Nilishawahi kumuonya huyu rafiki yangu, kwanza ukizingatia sisi ni majirani, pili huyu akisha kuja kujuwa itaniweka mimi pabaya sana, naona bora hata asingeniweka wazi juu yahili maana linaniumiza sana, kwakuwa huyo mwanaume ameshanogewa na penzi la nje, ameshaanza kujisahau, anamtesa sana mkewe , anampiga sana, anatishia kumfukuza, kitu kidogo tu kwake linakuwa kubwa, huyo dada huwa akipigwa na kufukuzwa anakuja kwangu, akifika kwangu anajieleza sana, na kusema nahisi mume wangu ana mwanamke mwingine,
maana mwanzo hakuwa hivi, anachowaza ni sahihi na mimi nalijuwa hilo, kinachoniuma zaidi sikumoja alipigwa sana mumewe usiku, akakimbilia kwangu, akamkuta na huyu mwizi yuko kwangu, akaanza kutueleza, nilimuhurumia sana, nikamwambia vumilia tu! lakini huy mwenzangu ambae ndie muhusika wa tukio, akawa anamshauri aondoke, aliniudhi sana na huwa namsema sana, lakini hasikii, najuta kwanini nimelijuwa hili, bora ingekuwa siri yao tu!
sasa kumwambia kuwa chanzo ni fulani, nashindwa maana wote ni mashoga zangu, Sasa hebu nishaurini, nimwambie tu liwalo na liwe, au nitaitwa mmbea niwaache tu mwenzie huku pembeni anajifanya anampenda, inaninyima raha sana hii.
Nilishawahi kumuonya huyu rafiki yangu, kwanza ukizingatia sisi ni majirani, pili huyu akisha kuja kujuwa itaniweka mimi pabaya sana, naona bora hata asingeniweka wazi juu yahili maana linaniumiza sana, kwakuwa huyo mwanaume ameshanogewa na penzi la nje, ameshaanza kujisahau, anamtesa sana mkewe , anampiga sana, anatishia kumfukuza, kitu kidogo tu kwake linakuwa kubwa, huyo dada huwa akipigwa na kufukuzwa anakuja kwangu, akifika kwangu anajieleza sana, na kusema nahisi mume wangu ana mwanamke mwingine,
maana mwanzo hakuwa hivi, anachowaza ni sahihi na mimi nalijuwa hilo, kinachoniuma zaidi sikumoja alipigwa sana mumewe usiku, akakimbilia kwangu, akamkuta na huyu mwizi yuko kwangu, akaanza kutueleza, nilimuhurumia sana, nikamwambia vumilia tu! lakini huy mwenzangu ambae ndie muhusika wa tukio, akawa anamshauri aondoke, aliniudhi sana na huwa namsema sana, lakini hasikii, najuta kwanini nimelijuwa hili, bora ingekuwa siri yao tu!
sasa kumwambia kuwa chanzo ni fulani, nashindwa maana wote ni mashoga zangu, Sasa hebu nishaurini, nimwambie tu liwalo na liwe, au nitaitwa mmbea niwaache tu mwenzie huku pembeni anajifanya anampenda, inaninyima raha sana hii.