‘Mpeni Sioi ubunge mumfute machozi’

Ni sawa na kusema world bank nipeni ajira mnifute machozi ya baba yangu alokuwa akifanya kazi hapo,na mniwezeshe kutunza familia kubwa alotuachia..mtakuwa mnampendeza Mungu sana world bank!
 
hapo wa arumeru wasahau maendeleo...kwa maana hela yote ya jimbo na mshahara ni
kwa ajili ya kulea familia ya sumari
 
Wakuu, msishangae Lusinde akawa tayari ametumiwa salamu za pongezi na wakuu wake! maana yeye ndiyo ameonekana mwenye busara ya kutumwa frontline ya chama chake!! Naamini waliobaki nyuma ni hoi zaidi kibusara kuliko huyo Lusinde!
 
Hebu someni tena hicho kipande kwenye blue. Naona kama kuna hila ya kumhujumy Sioi, au Lucinde anaugua ugonjwa ambao bado haujajulikana!


Lusinde haugui ndivyo alivyo jina lake ni LIVINGSTONE maana yake jiwe linaloishi, sasa jiwe lina akili? sasa wanatufumbua macho hawa magamba kuwa huwa wanagombea ili wapate hela za kusaidia familia zao, wapuuzi hawa, huwa wanapiga magoti kuomba kura kwa kujifanya wanataka kusaidia wananchi kumbe ni wananchi wa kwenye familia zao, full of sh..t
 
Aende zake huko..kwanza hii biashara ya kurithishana viti hii imetoka wapi..hii si nchi ya kifalme,au kuna kiziz wamechimbia kwahiyo wanataka kukizuia wengine wasijue kuna nini...mtoto anataka rithi matakataka ya baba ili nini..TUJIULIZE
 
Utashangaa sasa Sioi akishinda utamsikia Lusinde anasema "kama nisingewaambia wananchi wamfute machozi asingeshinda" subirini muone, argrrgggggrrrr
 
Mbunge mmoja wa jimbo moja la Mtera akimnadi SIOYI ktk uchaguzi mdogo ARUMERU kwa SERA MFIRISI kabisa eti Mh huyo anasema Wananchi wa Arumeru mashariki mchagueni SIOYI, kWANZA kama kifuta machozi kutokana na kifo cha babaye,PILI mchagueni ili aweze kupata msahara wa kuitunza familia aliyoachiwa na Marehemu babaye,na TATU mchagueni ili kumfurahisha Mh Kikwete.CCM hawana malengo mazuri na WAMERU,wanajali familia ya Marehemu tu na siyo WAMERU wapuuzeni. Wameru Chagueni Mbunge asiye na msongo wa mawazo ili mshirikiane na vema. SOURCE IS MWANANCHI NEWSPAPER,ON MONDAY,MARCH, 19TH 2012.
 
Nina masuala na uwezo wa wasimamizi wa kampeni za huyo Sumari. It appears kwamba motive pekee ya huyo bwana kugombea ni kupata mshahara wa kutunzia familia iliyoachwa na baba yake. Ni aibu kusikika kutoka katika midomo ya viongozi wa Chama chenye dhamana ya uongozi wa dola. Maana yake hapa ni kwamba kero za wananchi na uwakilishi wao ni secondary. Kwangu mimi, hiyo inatosha kumnyima kura mtu huyu.
 
Nina masuala na uwezo wa wasimamizi wa kampeni za huyo Sumari. It appears kwamba motive pekee ya huyo bwana kugombea ni kupata mshahara wa kutunzia familia iliyoachwa na baba yake. Ni aibu kusikika kutoka katika midomo ya viongozi wa Chama chenye dhamana ya uongozi wa dola. Maana yake hapa ni kwamba kero za wananchi na uwakilishi wao ni secondary. Kwangu mimi, hiyo inatosha kumnyima kura mtu huyu.
Nawaomba Wameru Sioyi wasimpe kura
 
Tatizo la wanaCCM hao hata hawawezi kusoma saikolojia ya watu wanaowasikiliza! Je walihisi kwamba wameru walimpenda sana Mzee Sumari?! hadi wawaombe kura za huruma?! au ndio kutapatapa?
 
Meneja kampeni mwenza, Vincent Nyerere, alisema kuwa yuko tayari kujitolea robota zima la vitambaa kwa ajili ya mgombea ubunge wa CCM anayetafuta ridhaa ya wananchi kupata nafasi hiyo nyeti kwa nia ya kufutwa machozi.
“Wananchi kura si kitambaa cha kufuta watu machozi, hivi hapa wangapi wamefiwa na baba zao, mama zao, shangazi zao, wajomba zao, kaka zao, dada zao na ndugu zao wengine wengi tu, lakini CCM na viongozi wake hawajaja hapa kuwaombea ubunge au uongozi wowote wa kuwafuta machozi…mbona hawajapewa ubunge?” alihoji.

Source :Tanzania Daima
 
Siasa chafu zaanza Arumeru
• Dk. Slaa ang'aka awataka polisi wachukue hatua haraka

na Mwandishi wetu

amka2.gif
SIASA chafu za kiharamia ambazo Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimehadharisha hivi karibuni, zimeanza kujidhihirisha baada ya kiongozi mmoja wa chama hicho, kutekwa na wanachama wanaodaiwa kuwa wafuasi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kisha kumpeleka msituni na kumfanyia unyama mkubwa.

Wafuasi hao wa CCM wanadaiwa kufanya unyama huo wakiongozwa na viongozi kadhaa wa mikoa ya Manyara na Kilimanjaro ambapo pia walimbana kiongozi huyo katika tawi la Magadirisho, Nuru Maeda, sehemu zake za siri.

Akisimulia kisa kizima cha kitendo hicho cha kutekwa nyara na mbele ya waandishi wa habari jana, Maeda ambaye alikuwa katika maumivu makali, alisema kuwa alikuwa akitoka kwa dada yake, na akiwa njiani alikutana na mwenyekiti wa kitongoji cha Magadirisho ambaye alimuuliza kuwa mkononi alikuwa amebeba nini.

"Nikamwambia nina daftari la wapiga kura, nilikuwa muwazi kwa sababu daftari la wapiga kura si tatizo na ni haki yangu kuwa nalo, yeye akasema kuwa hiyo ni moja ya nyaraka za serikali na kunitaka twende ofisini kwake; akampigia simu mtendaji wa kata, mtendaji yule akamjibu kuwa kama ana daftari hiyo ni haki yake kama kiongozi wala haina tatizo.

"Alipoona kuwa mtendaji hajampatia ushirikiano kama alivyotaka, akaniachia nikaenda nyumbani, kumbe huku nyuma kawapigia simu watu wa CCM," alisema na kuongeza:

"Ghafla nikiwa nyumbani nakunywa chai, wakaja watoto wanasema mwenyekiti wa kitongoji alikuwa ananiita, nikaenda; nilipofika ofisini, muda mfupi wakaja watu wa CCM ambao wengine nawafahamu kwani niliwahi kufanya nao kazi, alikuwepo katibu wa CCM mikoa ya (anaitaja)."

Alidai kuwa walimchukua pale na kumpeleka katika msitu kwenda kumtesa sana, wakampiga na kumminya sana sehemu zake za siri.

"Leo hapa kama isingekuwa kuwajua wale watu nilikuwa nakufa, mpaka sasa ingekuwa habari nyingine. Baadaye nikawaambia kuliko kunitesa wanipeleke kituo cha polisi; nilipofika hapo wakataka kuwa mbele, ndipo OCD akaamuru nipewe kipaumbele kusikilizwa ili ijulikane hasa nini kimetokea, hivi sasa narudi kituoni hapo tena," alisema Maeda.

Akizungumzia tukio hilo katika mkutano wa mwisho kwa siku ya jana kijiji cha Songoro, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Slaa, alionya kuwa matukio ya namna hiyo hayatavumilika tena, akitoa wito kwa Jeshi la Polisi kuchukua hatua za haraka bila kupendelea.

Akionekana kushangazwa, alisema ni hatari vitendo vya kihuni kama hivyo kufanywa na chama tawala tena na viongozi wakubwa wa chama hicho.

Dk. Slaa alisema ni ajabu kuwa baada ya miaka yote ya kuwa madarakani CCM imeshindwa kuzungumza mafanikio ya sera zake kwa wananchi kwa vitendo badala yake inaanza kuomba nafasi za uwakilishi ikitaka ‘kuonewa huruma na kufutwa machozi'.

Akimnadi mgombea wa chama hicho, Joshua Nassari, katika maeneo mbalimbali ya kata za Kikwe, Nkoaranga na Songoro, Dk. Slaa aliwaambia wananchi kuwa wakati wa uchaguzi si wakati wa kufanya propaganda, kueneza majungu na umbea bali ni mahali pa vyama kushindana kwa sera na hoja.

Dk. Slaa aliwaambia wananchi kuwa endapo watamchagua Nassari watakuwa amepata mtu wa kufanya kazi iliyowahi kufanywa na aliyekuwa mmoja wa wapigania uhuru wa Tanganyika, hayati Japhet Kirilo, aliyekwenda kupigania ardhi ya Wameru huko Umoja wa Mataifa (UN).

Naye, Nassari aliwaambia wananchi kuwa chini ya uongozi makini wa CHADEMA, atakwenda bungeni na halmashauri kuisimamia, kuiagiza na kuiwajibisha serikali kwa kuhoji masuala mbalimbali.

Kwa upande wake, meneja kampeni mwenza, Vincent Nyerere, alisema kuwa yuko tayari kujitolea robota zima la vitambaa kwa ajili ya mgombea ubunge wa CCM anayetafuta ridhaa ya wananchi kupata nafasi hiyo nyeti kwa nia ya kufutwa machozi.

"Wananchi kura si kitambaa cha kufuta watu machozi, hivi hapa wangapi wamefiwa na baba zao, mama zao, shangazi zao, wajomba zao, kaka zao, dada zao na ndugu zao wengine wengi tu, lakini CCM na viongozi wake hawajaja hapa kuwaombea ubunge au uongozi wowote wa kuwafuta machozi…mbona hawajapewa ubunge?" alihoji.

 
jamani mtu anasimama jukwaani na kusema,wana arumeru mchagueni sioi sumary kuwa mbunge wenu kwa sababu 3 muhimu
1.mkimchagua,mtakuwa mmemfuta machozi ya kuondokewa na baba yake marehem sumary
2.mkimchagua,mtakuwa mmempa ajira ili aweze kuihudumia familia iliyoachwa na baba yake.
3.mkimchagua,mtakuwa 'mmemfurahisha' jk maana ndie aliesimamia mchakato wa kumsimamisha agombee ubunge arumeru.
JE WANANCHI WA ARUMERU WAMEWEKWA WAPI KTK KUTATUA MATATIZO YAO YA KIJAMII,KIUCHUMI NA KITAMADUNI?MAANA KTK SABABU ZOTE 3,HAKUNA NAFASI YA MWANANCHI.
JE DHAMIRA YA WANACCM IKO WAPI,KWAO AU KWA WANANCHI?
yaani sisi wa arumeru tumpe ubunge ili tumfute machozi???????????????? these are fool minds!
NAWASILISHA!
 
Ama kweli ccm nikundi la Mafya na kujipatia uchindi wakekunatokana na ukungu wa kiza yani udanganyifu wa ahadi nyingi wasizowezakuzitekeleza, ubenaji, kutumia vikoso vya polisi na nguvu kupita kiasi ,kutumia pesa nyingi za wavuja jacho huku nchi ikikabiliwa na matatizo makubwana migomo.

Kawaida ukiaza foul inamana mpira umekunamia? Kwa hio ccmwamechoka kwahio Watanzania niwajibu wetu kuipunzicha ili chadema ishikeusukani, ccm inanuka kwa viongozi kujilimbikizia mamali huku wavuja jachowakihaha na migomo isio kwicha.
 
jAMANII UBUNGE SIYO RAMBIRAMBI, LUSINDE INGEFAA ZAIDI AKIPELEKWA MILEMBE KUCHUNGUZWA AKILI KAMA IPO SAWA!!!!!!!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom