‘Mpeni Sioi ubunge mumfute machozi’

mkirua vunjo

Member
Nov 11, 2011
25
5
Mwandishi Wetu, Arumeru
WANANCHI wa Jimbo la Arumeru Mashariki, wameombwa kumchagua mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CCM, Sioi Sumari ili kumfuta machozi yaliyotokana na kifo cha baba yake mzazi, Jeremiah Sumari ambaye alikuwa Mbunge wa Jimbo hilo.

Mbali na hilo wananchi hao wameelezwa kuwa kwa kufanya hivyo, watakuwa wamejipatia baraka kwa Mungu kwani watamwezesha Sioi kupata mshahara utakaomwezesha kuendesha familia aliyoachiwa na baba yake.

Mwito huo ulitolewa juzi katika Kijiji cha Migadini, Kata ya Mororoni na Mbunge wa Mtera(CCM), Livingstone Lusinde alipokuwa akimnadi mgombea huyo katika kampeni za uchaguzi mdogo zinazoendelea jimboni humo.

Lusinde alisema wananchi hao wanastahili kuwa na moyo wa huruma kwa kumchagua kwa kura nyingi ili ajipatie mshahara wa kumwezesha kumudu familia aliyoachiwa na marehemu baba yake, ikiwa ni moja ya njia ya kumfuta machozi.

"Mkimchagua Sioi mtapata baraka za Mungu kwa vile mtakuwa mmewezesha kutokea kwa mambo matatu… kwanza kura zenu zitamfuta machozi ya kufiwa na baba yake, pili mtamwezesha kupata mshahara utakaomwezesha kulea familia yake ambayo sasa haina baba," alisema Lusinde.

Pia aliwaambia wananchi hao kwamba kumchagua Sioi kuwa mbunge wa jimbo hilo ni kumfurahisha Rais Jakaya Kikwete kwa kuwa huyo ndiye chaguo lake na ndiye aliyeongoza vikao vya Kamati Kuu iliyokutana mara mbili kupitisha jina lake kuwa mgombea wakati wa mchakato wa kura za maoni.

Alisema katika kura hizo za maoni zilizofanyika mara mbili, zote Sioi alionekana kushinda na kuibuka kidedea.

"Njia pekee ya kumfurahisha Rais ni kumchagua Sioi kwa kuwa ni chaguo lake, hakika mtamfurahisha na Sioi ataweza kutekeleza vyema ilani ya chama," alisema Lusinde.

Kwa upande wake, Sioi alisema anayaelewa vyema matatizo yanayoikabili Kata ya Maroroni ikiwemo ukosefu wa mashamba ya uhakika, maji, barabara na zahanati hivyo akichaguliwa, atayatatua matatizo hayo mara moja.

"Nawaombeni sana mnichague kuwa mbunge wenu ili kwa pamoja tuweze kushirikiana kutatua kero hizi ambazo kimsingi zote nazifahamu vyema na nafahamu pia hatua za kuchukua ili kuhakikisha tunaondokana nazo," alisema Sioi.

Shabiki wa Chadema
Katika tukio jingine hekima na busara za Mratibu Mkuu wa kampeni za CCM, Mwigulu Nchemba zilitumika kuepusha maafa kwa mwanachama mmoja wa Chadema, aliyevalia sare za chama hicho baada ya kufika kwenye mkutano wa CCM katika Kata ya Kikatiti.

Wakati Mwigulu akihutubia mkutano huo, mwanachama huyo wa Chadema, ghafla alivamia mkutano huo na kuanza kupiga mayowe huku akitamka maneno ya "Peoples Power" (Nguvu ya umma).

Hatua hiyo iliwakera wafuasi wa CCM ambao waliamua kumtia adabu kabla ya Mwigulu kuingilia kati kuwazuia akiwataka wamwache kwani alikuwa anapaswa kufundishwa sera za CCM.
 
Mwandishi Wetu, Arumeru
WANANCHI wa Jimbo la Arumeru Mashariki, wameombwa kumchagua mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CCM, Sioi Sumari ili kumfuta machozi yaliyotokana na kifo cha baba yake mzazi, Jeremiah Sumari ambaye alikuwa Mbunge wa Jimbo hilo.

Mbali na hilo wananchi hao wameelezwa kuwa kwa kufanya hivyo, watakuwa wamejipatia baraka kwa Mungu kwani watamwezesha Sioi kupata mshahara utakaomwezesha kuendesha familia aliyoachiwa na baba yake.

Mwito huo ulitolewa juzi katika Kijiji cha Migadini, Kata ya Mororoni na Mbunge wa Mtera(CCM), Livingstone Lusinde alipokuwa akimnadi mgombea huyo katika kampeni za uchaguzi mdogo zinazoendelea jimboni humo.

Lusinde alisema wananchi hao wanastahili kuwa na moyo wa huruma kwa kumchagua kwa kura nyingi ili ajipatie mshahara wa kumwezesha kumudu familia aliyoachiwa na marehemu baba yake, ikiwa ni moja ya njia ya kumfuta machozi.

“Mkimchagua Sioi mtapata baraka za Mungu kwa vile mtakuwa mmewezesha kutokea kwa mambo matatu… kwanza kura zenu zitamfuta machozi ya kufiwa na baba yake, pili mtamwezesha kupata mshahara utakaomwezesha kulea familia yake ambayo sasa haina baba,” alisema Lusinde.

Pia aliwaambia wananchi hao kwamba kumchagua Sioi kuwa mbunge wa jimbo hilo ni kumfurahisha Rais Jakaya Kikwete kwa kuwa huyo ndiye chaguo lake na ndiye aliyeongoza vikao vya Kamati Kuu iliyokutana mara mbili kupitisha jina lake kuwa mgombea wakati wa mchakato wa kura za maoni.

Alisema katika kura hizo za maoni zilizofanyika mara mbili, zote Sioi alionekana kushinda na kuibuka kidedea.

“Njia pekee ya kumfurahisha Rais ni kumchagua Sioi kwa kuwa ni chaguo lake, hakika mtamfurahisha na Sioi ataweza kutekeleza vyema ilani ya chama,” alisema Lusinde.

Kwa upande wake, Sioi alisema anayaelewa vyema matatizo yanayoikabili Kata ya Maroroni ikiwemo ukosefu wa mashamba ya uhakika, maji, barabara na zahanati hivyo akichaguliwa, atayatatua matatizo hayo mara moja.

“Nawaombeni sana mnichague kuwa mbunge wenu ili kwa pamoja tuweze kushirikiana kutatua kero hizi ambazo kimsingi zote nazifahamu vyema na nafahamu pia hatua za kuchukua ili kuhakikisha tunaondokana nazo,” alisema Sioi.

Shabiki wa Chadema
Katika tukio jingine hekima na busara za Mratibu Mkuu wa kampeni za CCM, Mwigulu Nchemba zilitumika kuepusha maafa kwa mwanachama mmoja wa Chadema, aliyevalia sare za chama hicho baada ya kufika kwenye mkutano wa CCM katika Kata ya Kikatiti.

Wakati Mwigulu akihutubia mkutano huo, mwanachama huyo wa Chadema, ghafla alivamia mkutano huo na kuanza kupiga mayowe huku akitamka maneno ya "Peoples Power" (Nguvu ya umma).

Hatua hiyo iliwakera wafuasi wa CCM ambao waliamua kumtia adabu kabla ya Mwigulu kuingilia kati kuwazuia akiwataka wamwache kwani alikuwa anapaswa kufundishwa sera za CCM.

Duh! Mbunge anawaza mshahara tu? kwahiyo wanamchagua ili aweze kukimu mahitaji yake ya kimaisha!
 
Lusinde alisema wananchi hao wanastahili kuwa na moyo wa huruma kwa kumchagua kwa kura nyingi ili ajipatie mshahara wa kumwezesha kumudu familia aliyoachiwa na marehemu baba yake, ikiwa ni moja ya njia ya kumfuta machozi.

"Mkimchagua Sioi mtapata baraka za Mungu kwa vile mtakuwa mmewezesha kutokea kwa mambo matatu… kwanza kura zenu zitamfuta machozi ya kufiwa na baba yake, pili mtamwezesha kupata mshahara utakaomwezesha kulea familia yake ambayo sasa haina baba," alisema Lusinde.

Pia aliwaambia wananchi hao kwamba kumchagua Sioi kuwa mbunge wa jimbo hilo ni kumfurahisha Rais Jakaya Kikwete kwa kuwa huyo ndiye chaguo lake na ndiye aliyeongoza vikao vya Kamati Kuu iliyokutana mara mbili kupitisha jina lake kuwa mgombea wakati wa mchakato wa kura za maoni.

Hebu someni tena hicho kipande kwenye blue. Naona kama kuna hila ya kumhujumy Sioi, au Lucinde anaugua ugonjwa ambao bado haujajulikana!
 
Ubunge si fadhila wala kufutana machozi.Hawa CCM kwani wanakula nini hawa wenzetu?!
 
Duuu Mh. Lusinde kweli sera zimekwisha kabisa huko CCM....... Kura za kumfuta machozi????? agrrrrrrrrr..
 
Hotuba hii ingefana sana siku ya sikukiu ya R.I.P akili ya Job Lusinde!
 
Kama mtu anatakiwa kuchaguliwa ili akapate mshahara wa kujikimu yeye na familia yake basi haina maana. Hivi haya matatizo ya huko arumeru mashariki amabyo CCm wanayahubiri sasa na kuahidi kuyatatua kupitia Sioi yalikuwa hayaonekani miaka yote wao wakiwa wanaongoza hilo jimbo? Kwa kweli ukiambiwa kitu jaribu kuchanganya na za kwako!!
 
Mwandishi Wetu, Arumeru
WANANCHI wa Jimbo la Arumeru Mashariki, wameombwa kumchagua mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CCM, Sioi Sumari ili kumfuta machozi yaliyotokana na kifo cha baba yake mzazi, Jeremiah Sumari ambaye alikuwa Mbunge wa Jimbo hilo.

Mbali na hilo wananchi hao wameelezwa kuwa kwa kufanya hivyo, watakuwa wamejipatia baraka kwa Mungu kwani watamwezesha Sioi kupata mshahara utakaomwezesha kuendesha familia aliyoachiwa na baba yake.

Mwito huo ulitolewa juzi katika Kijiji cha Migadini, Kata ya Mororoni na Mbunge wa Mtera(CCM), Livingstone Lusinde alipokuwa akimnadi mgombea huyo katika kampeni za uchaguzi mdogo zinazoendelea jimboni humo.

Lusinde alisema wananchi hao wanastahili kuwa na moyo wa huruma kwa kumchagua kwa kura nyingi ili ajipatie mshahara wa kumwezesha kumudu familia aliyoachiwa na marehemu baba yake, ikiwa ni moja ya njia ya kumfuta machozi.

“Mkimchagua Sioi mtapata baraka za Mungu kwa vile mtakuwa mmewezesha kutokea kwa mambo matatu… kwanza kura zenu zitamfuta machozi ya kufiwa na baba yake, pili mtamwezesha kupata mshahara utakaomwezesha kulea familia yake ambayo sasa haina baba,” alisema Lusinde.

Pia aliwaambia wananchi hao kwamba kumchagua Sioi kuwa mbunge wa jimbo hilo ni kumfurahisha Rais Jakaya Kikwete kwa kuwa huyo ndiye chaguo lake na ndiye aliyeongoza vikao vya Kamati Kuu iliyokutana mara mbili kupitisha jina lake kuwa mgombea wakati wa mchakato wa kura za maoni.

Alisema katika kura hizo za maoni zilizofanyika mara mbili, zote Sioi alionekana kushinda na kuibuka kidedea.

“Njia pekee ya kumfurahisha Rais ni kumchagua Sioi kwa kuwa ni chaguo lake, hakika mtamfurahisha na Sioi ataweza kutekeleza vyema ilani ya chama,” alisema Lusinde.

Kwa upande wake, Sioi alisema anayaelewa vyema matatizo yanayoikabili Kata ya Maroroni ikiwemo ukosefu wa mashamba ya uhakika, maji, barabara na zahanati hivyo akichaguliwa, atayatatua matatizo hayo mara moja.

“Nawaombeni sana mnichague kuwa mbunge wenu ili kwa pamoja tuweze kushirikiana kutatua kero hizi ambazo kimsingi zote nazifahamu vyema na nafahamu pia hatua za kuchukua ili kuhakikisha tunaondokana nazo,” alisema Sioi.

Shabiki wa Chadema
Katika tukio jingine hekima na busara za Mratibu Mkuu wa kampeni za CCM, Mwigulu Nchemba zilitumika kuepusha maafa kwa mwanachama mmoja wa Chadema, aliyevalia sare za chama hicho baada ya kufika kwenye mkutano wa CCM katika Kata ya Kikatiti.

Wakati Mwigulu akihutubia mkutano huo, mwanachama huyo wa Chadema, ghafla alivamia mkutano huo na kuanza kupiga mayowe huku akitamka maneno ya "Peoples Power" (Nguvu ya umma).

Hatua hiyo iliwakera wafuasi wa CCM ambao waliamua kumtia adabu kabla ya Mwigulu kuingilia kati kuwazuia akiwataka wamwache kwani alikuwa anapaswa kufundishwa sera za CCM.

Hawa jamaa wameishiwa la kuzungumza mbele ya wananchi, ina maana Mtanzania atakayefariki akiwa kwenye utumishi wa umma nafasi yake apewe mtoto ili aweze kuendelea kutunza familia hiyo? Job Lusinde alikuwa balozi lakini kijana wake anayesema maneno hayo hajapewa nafasi hiyo, matokeo yake yeye alimg'oa baba yake Mzee John Malecela kwenye nafasi ya ubunge akaichukua yeye na sijui familia ya baba yake aliyefanya kampeini kumuondoa kwenye nafasi hiyo anaionaje aulizwe Lusinde.
Kama familia ni ya katibu mkuu akifariki mtoto apewe nafasi hiyo ili atunze familia yao? acheni kupotosha umma wa Arumeru Mashariki nyie CCM ongea yenye mantiki. Angalia penye wekundu
 
CCM kweli wameishiwa. Nikiwa mdogo sikuwahi kuona kiongozi wa CCM mwenye uwezo mdogo wa kuzungumza kama LUSINDE. Huku ni kuwatukana hata watu waliomsaidia kumchakachua Mzee Malecela hili yeye apate nafasi. maskini chama hichi Kikongwe
 
Very goo CCM, sasa hamfichi ujinga wenu. Kwa hiyo ubunge sasa umekuwa fadhila kwa mtu kupewa ili afute machozi ya kufiwa na baba yake, loh!

Ngoja na mimi niende UN nikadai kurithi ofisi ya marehemu baba yangu. Kumbe ndio maisha simpo namna hii kama baba aliacha ofisi
 
Hotuba hii ingefana sana siku ya sikukuu ya wajinga R.I.P akili ya Job Lusinde
 
CCM kweli wameishiwa. Nikiwa mdogo sikuwahi kuona kiongozi wa CCM mwenye uwezo mdogo wa kuzungumza kama LUSINDE. Huku ni kuwatukana hata watu waliomsaidia kumchakachua Mzee Malecela hili yeye apate nafasi. maskini chama hichi Kikongwe

Uwezo wake wa kuzungumza sio mdogo, ni mkubwa hasa. Alichopungukiwa ni uwezo wa kufikiri, lkn hata hivyo sio shida sana ndani ya CCM. Siasa za CCM hazihitaji akili, ni mdomo na tumbo tu.
 
Very goo CCM, sasa hamfichi ujinga wenu. Kwa hiyo ubunge sasa umekuwa fadhila kwa mtu kupewa ili afute machozi ya kufiwa na baba yake, loh!

Ngoja na mimi niende UN nikadai kurithi ofisi ya marehemu baba yangu. Kumbe ndio maisha simpo namna hii kama baba aliacha ofisi

Sasa na wewe umekuja kumueleza nani humu JF mambo yako?
 
Mwandishi Wetu, Arumeru
WANANCHI wa Jimbo la Arumeru Mashariki, wameombwa kumchagua mgombea Ubunge wa Jimbo hilo kupitia CCM, Sioi Sumari ili kumfuta machozi yaliyotokana na kifo cha baba yake mzazi, Jeremiah Sumari ambaye alikuwa Mbunge wa Jimbo hilo.

Mbali na hilo wananchi hao wameelezwa kuwa kwa kufanya hivyo, watakuwa wamejipatia baraka kwa Mungu kwani watamwezesha Sioi kupata mshahara utakaomwezesha kuendesha familia aliyoachiwa na baba yake.

Mwito huo ulitolewa juzi katika Kijiji cha Migadini, Kata ya Mororoni na Mbunge wa Mtera(CCM), Livingstone Lusinde alipokuwa akimnadi mgombea huyo katika kampeni za uchaguzi mdogo zinazoendelea jimboni humo.

Lusinde alisema wananchi hao wanastahili kuwa na moyo wa huruma kwa kumchagua kwa kura nyingi ili ajipatie mshahara wa kumwezesha kumudu familia aliyoachiwa na marehemu baba yake, ikiwa ni moja ya njia ya kumfuta machozi.

"Mkimchagua Sioi mtapata baraka za Mungu kwa vile mtakuwa mmewezesha kutokea kwa mambo matatu… kwanza kura zenu zitamfuta machozi ya kufiwa na baba yake, pili mtamwezesha kupata mshahara utakaomwezesha kulea familia yake ambayo sasa haina baba," alisema Lusinde.

Pia aliwaambia wananchi hao kwamba kumchagua Sioi kuwa mbunge wa jimbo hilo ni kumfurahisha Rais Jakaya Kikwete kwa kuwa huyo ndiye chaguo lake na ndiye aliyeongoza vikao vya Kamati Kuu iliyokutana mara mbili kupitisha jina lake kuwa mgombea wakati wa mchakato wa kura za maoni.

Alisema katika kura hizo za maoni zilizofanyika mara mbili, zote Sioi alionekana kushinda na kuibuka kidedea.

"Njia pekee ya kumfurahisha Rais ni kumchagua Sioi kwa kuwa ni chaguo lake, hakika mtamfurahisha na Sioi ataweza kutekeleza vyema ilani ya chama," alisema Lusinde.

Kwa upande wake, Sioi alisema anayaelewa vyema matatizo yanayoikabili Kata ya Maroroni ikiwemo ukosefu wa mashamba ya uhakika, maji, barabara na zahanati hivyo akichaguliwa, atayatatua matatizo hayo mara moja.

"Nawaombeni sana mnichague kuwa mbunge wenu ili kwa pamoja tuweze kushirikiana kutatua kero hizi ambazo kimsingi zote nazifahamu vyema na nafahamu pia hatua za kuchukua ili kuhakikisha tunaondokana nazo," alisema Sioi.

Shabiki wa Chadema
Katika tukio jingine hekima na busara za Mratibu Mkuu wa kampeni za CCM, Mwigulu Nchemba zilitumika kuepusha maafa kwa mwanachama mmoja wa Chadema, aliyevalia sare za chama hicho baada ya kufika kwenye mkutano wa CCM katika Kata ya Kikatiti.

Wakati Mwigulu akihutubia mkutano huo, mwanachama huyo wa Chadema, ghafla alivamia mkutano huo na kuanza kupiga mayowe huku akitamka maneno ya "Peoples Power" (Nguvu ya umma).

Hatua hiyo iliwakera wafuasi wa CCM ambao waliamua kumtia adabu kabla ya Mwigulu kuingilia kati kuwazuia akiwataka wamwache kwani alikuwa anapaswa kufundishwa sera za CCM.
Kwa akili kama hii mtu ataache kusinzia Bungeni kweli??? Hawa ndiyo vijana wanaotegemwa na Magamba katika kuikomboa nchi hii, kazi kweli kweli.
 
Lakini hizi ndio hoja zilizobakia kwa CCM. Hata mkuu wao anaongea maneno yanayofanana na haya ni kwa vile watu hawayachambui kwa kina. Baada ya kupitishwa kwa Dr. Shein kugombea uraisi wa Zanzibar mwaka 2010 alisema haya, wengine mliokosa ni wadogo, wengine mna uwezo lakini kura hazikutosha, tutawapa kazi nyingine.... Hii sentensi ni ya KEPEANA. Lakini wakati wabunge wa CHADEMA walipotoka bungeni, alisema MAMBO YAO TUTAYAPITISHA SISI, POSHO TUTAZIPITISHA SISI, kwa hiyo lazima warudi kwa sababu wanatuhitaji, hii kauli ukiichambua kiundani haina UWAJIBIKAJI ndani yake bali ULAJI
 
WANANCHI WA ARUMERU WATAMCHAGUA SIOI IKIWA BABA YAKE ALIWALETEA MAENDELEO KATIKA JIMBO AMBALO LINAONEKANA KUWA NA KERO NYINGI AMBAZO ZIMESHINDWA KUPATA UFUMBUZI KAMA AMBAVYO AHADI ZA JAKAYA ZILIVYOSHINDWA KUTATULIWA.KIMSINGI WANANCHI WANA KILA SABABU YA KUTAFAKARI SANA ,NA SI KUCHAGUA ETI KUPATA MSHAHARA WA KUSUSTAIN FAMILIA.ACTUALLY THEY ARE WELLOFF.:scared::lock1:
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom