Tegelezeni
JF-Expert Member
- Dec 31, 2009
- 268
- 124
Ushauri mzuri sana huu. Kama kuna ndugu yake ambaye ni memba humu JF, basi au-print huu uzi na kumpelekea. utamsaidia kujitizama upya.Kama utafanikiwa kutoka kwenye janga hili, nakusihi uwe balozi mwema wa kuwashawishi hata wenzako wenye umri kama wako waone faida za kuwa watulivu, na kuishi maisha ya uadilifu na kutii maonyo ya wazazi, viongozi wa dini na jamii kwa ujumla. Maisha ya mahangaiko yana hatari nyingi na balaa nyingi, watu wengi ambao wameshindwa kutulia na kuendesha maisha ya kiistaarabu wamejikuta wakijiingiza kwenye shida na majanga ambayo huenda yasingekuwa na sababu yatokee, hili ni muhimu sana ulizingatie maana ''mtoto wa tajiri akionywa mtoto wa maskini tega sikio" pia unaelewa wazi kuwa "mchuma janga hula na wakwao". Pole sana dada yangu, ningekuandikia mengi ila naona nisikuchoshe upumzike kwani hili nililokukuta kwa vyovyote litakuwa limekuvunja sana moyo na kukutia simanzi, kwa vyovyote vikao vya bunge lisilo rasmi kichwani kwako litakuwa likikuyumbisha kwa maoni na kukutaka utoe miongozo itakayosaidia kuondokana na hii dhahma, jitie moyo, inawezekana wanadamu wasitake kukuelewa ila nakuhakikishia hapo ulipo ukimwita mola wako kwa uaminifu yeye atakuelewa tu na anaweza kabisa kukuepusha na janga hili pole sana Lulu.