Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Mpendazoe afichua njama mpya
na Mwandishi wetu
ALIYEKUWA mgombea ubunge jimbo la Segerea kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Fred Mpendazoe, ameeleza kufanyiwa njama zenye lengo la kumhusisha na biashara ya madawa ya kulevya ili kudhoofisha harakati za kisiasa.
Mpendazoe ambaye amefungua kesi mahakama kuu Dar es Salaam kupinga matokeo ya uchaguzi wa ubunge wa jimbo hilo yaliyompa ushindi Makongoro Mahanga (CCM), jana aliiambia Tanzania Daima kwamba mwishoni mwa mwaka jana alipata taarifa kutoka kwa mmoja wa Wasamaria wema kwamba upo mpango wa kumpandikizia kesi ya kufanya biashara ya madawa ya kulevya ili imdhohofishe kisiasa.
Alisema wiki moja baada ya kupewa taarifa hiyo ambayo hakuitilia maanani, aliweza kutengua mtego uliosukwa na watu wanne (majina tunayahifadhi) waliojaribu kumuomba asaidie kununua madawa ya kuhifadhia chakula huku lengo lao likiwa ni kumtegeshea madawa ya kulevya.
Akisimulia sakata hilo Mpendazoe alisema alipigiwa simu na mtu mmoja aliyedai anafanya kazi Kigoma katika shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) na kumuomba amsaidie kununua madawa ya kuhifadhia chakula jijini Dar es Salaam.
"Alisema malipo yote wangefanya wao lakini mimi niwasiliane kwanza na msambazaji wao aliyepo hapa Dar anionyeshe sample halafu wao watakuja kulipia madawa yote ambayo jumla yake yangegharimu milioni 150 na kwamba wangenipa kamisheni ya milioni 25. Akanipa na namba ya simu ya huyo msambazaji.
"Msambazaji wao alisema yupo tayari kumtuma dereva wake aniletee sampuli Ubungo Plaza na sampuli moja ina thamani ya milioni tatu lakini chaajabu yeye alikuwa tayari niletewe bure wakati hata hatujaonana zaidi ya kuzungumza kwa simu tu. Huyo dereva wake alipokuja akataka tuelekee moja kwa moja kwenye gari langu ili aweke hayo madawa nikamwambia asubiri kwanza...nikampigia tena bosi wake na kumuomba aje kwanza angalau tufahamiane.
Hakuja na dereva wake akaondoka na madawa kabla hata sijayakagua. Tangu siku hiyo nikipiga namba ya huyo muuzaji wa madawa ya vyakula haipatikani na nikipiga ya yule wa Kigoma aliyenituma nimsaidie kuyanunua nayo haipatikani...wote wanajuana" alisema Mpendazoe ambaye amewasilisha maelezo hayo kwa jeshi la polisi ili lifanye uchunguzi.
Kabla ya sakata hilo, Mpendazoe alieleza kufanyiwa njama nyingine ya kudaiwa kutumia gari la wizi ambalo hata hivyo alithibitisha ni gari lake.
na Mwandishi wetu
Mpendazoe ambaye amefungua kesi mahakama kuu Dar es Salaam kupinga matokeo ya uchaguzi wa ubunge wa jimbo hilo yaliyompa ushindi Makongoro Mahanga (CCM), jana aliiambia Tanzania Daima kwamba mwishoni mwa mwaka jana alipata taarifa kutoka kwa mmoja wa Wasamaria wema kwamba upo mpango wa kumpandikizia kesi ya kufanya biashara ya madawa ya kulevya ili imdhohofishe kisiasa.
Alisema wiki moja baada ya kupewa taarifa hiyo ambayo hakuitilia maanani, aliweza kutengua mtego uliosukwa na watu wanne (majina tunayahifadhi) waliojaribu kumuomba asaidie kununua madawa ya kuhifadhia chakula huku lengo lao likiwa ni kumtegeshea madawa ya kulevya.
Akisimulia sakata hilo Mpendazoe alisema alipigiwa simu na mtu mmoja aliyedai anafanya kazi Kigoma katika shirika la umoja wa mataifa la kuhudumia wakimbizi (UNHCR) na kumuomba amsaidie kununua madawa ya kuhifadhia chakula jijini Dar es Salaam.
"Alisema malipo yote wangefanya wao lakini mimi niwasiliane kwanza na msambazaji wao aliyepo hapa Dar anionyeshe sample halafu wao watakuja kulipia madawa yote ambayo jumla yake yangegharimu milioni 150 na kwamba wangenipa kamisheni ya milioni 25. Akanipa na namba ya simu ya huyo msambazaji.
"Msambazaji wao alisema yupo tayari kumtuma dereva wake aniletee sampuli Ubungo Plaza na sampuli moja ina thamani ya milioni tatu lakini chaajabu yeye alikuwa tayari niletewe bure wakati hata hatujaonana zaidi ya kuzungumza kwa simu tu. Huyo dereva wake alipokuja akataka tuelekee moja kwa moja kwenye gari langu ili aweke hayo madawa nikamwambia asubiri kwanza...nikampigia tena bosi wake na kumuomba aje kwanza angalau tufahamiane.
Hakuja na dereva wake akaondoka na madawa kabla hata sijayakagua. Tangu siku hiyo nikipiga namba ya huyo muuzaji wa madawa ya vyakula haipatikani na nikipiga ya yule wa Kigoma aliyenituma nimsaidie kuyanunua nayo haipatikani...wote wanajuana" alisema Mpendazoe ambaye amewasilisha maelezo hayo kwa jeshi la polisi ili lifanye uchunguzi.
Kabla ya sakata hilo, Mpendazoe alieleza kufanyiwa njama nyingine ya kudaiwa kutumia gari la wizi ambalo hata hivyo alithibitisha ni gari lake.