nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
HATIMAYE aliyekuwa mgombea ubunge wa jimbo la Segerea (CHADEMA), Fred Mpendazoe, amelipa sh milioni 15 katika Idara ya Fedha ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es salaam ikiwa ni dhamana ya kesi yake ya kupinga matokeo ya uchaguzi wa jimbo uliofanyika mwaka jana ambayo yalimtangaza Naibu Waziri wa Kazi na Ajira, Makongoro Mahanga (CCM), kuwa ndiye mbunge wa jimbo hilo.
Mbali na Dk. Mahanga wadaiwa wengine ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo.
Katika madai yake mlalamikaji ambaye ni Mpendazoe anaitaka Mahakama Kuu itengue ushindi wa Dk. Mahanga kwa kuwa taratibu za sheria ya uchaguzi ya mwaka 2010 hazikufuatwa.
Wakili wa Mpendazoe, Peter Kibatala, jana ndiye aliyekwenda idara hiyo ya fedha iliyoko ndani ya jengo la Mahakama ya Rufaa nchini kulipa kiasi hicho cha fedha na kuwaonyesha waandishi wa habari risiti ya malipo hayo.
Hii ndiyo risiti ya kiasi hicho cha fedha nilicholipa mahakamani kama dhamana ya kesi iliyofunguliwa na mteja wangu .na kwa kuwa tayari tumeishalipa baada ya kuupata uthibitisho wa malipo haya, Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ndiye atapanga tarehe ya kesi ya mteja wangu kuanza kusikilizwa rasmi kwani taratibu zote za kisheria tumeishazikamilisha, alisema wakili Peter Kibatala.
Machi nane mwaka huu, Jaji Profesa Ibrahimu Juma, alitupilia mbali pingamizi la wakili Jerome Msemwa anayewatetea wadaiwa, la kutaka mahakama hiyo imzuie Mpendazoe asiruhusiwe kuweka kiasi hicho cha fedha mahakamani kwa sababu muda wa kuwasilisha fedha hizo ulikuwa umeishapita.
Jaji Ibrahimu alitupilia mbali pingamizi hilo kwa kuwa halikuwa limekidhi matakwa ya kisheria na badala yake akalikubali ombi la Mpendazoe kuweka mahakama kiasi hicho cha fedha kama dhamana.
Mbali na Dk. Mahanga wadaiwa wengine ni Mwanasheria Mkuu wa Serikali na aliyekuwa msimamizi wa uchaguzi wa jimbo hilo.
Katika madai yake mlalamikaji ambaye ni Mpendazoe anaitaka Mahakama Kuu itengue ushindi wa Dk. Mahanga kwa kuwa taratibu za sheria ya uchaguzi ya mwaka 2010 hazikufuatwa.
Wakili wa Mpendazoe, Peter Kibatala, jana ndiye aliyekwenda idara hiyo ya fedha iliyoko ndani ya jengo la Mahakama ya Rufaa nchini kulipa kiasi hicho cha fedha na kuwaonyesha waandishi wa habari risiti ya malipo hayo.
Hii ndiyo risiti ya kiasi hicho cha fedha nilicholipa mahakamani kama dhamana ya kesi iliyofunguliwa na mteja wangu .na kwa kuwa tayari tumeishalipa baada ya kuupata uthibitisho wa malipo haya, Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, ndiye atapanga tarehe ya kesi ya mteja wangu kuanza kusikilizwa rasmi kwani taratibu zote za kisheria tumeishazikamilisha, alisema wakili Peter Kibatala.
Machi nane mwaka huu, Jaji Profesa Ibrahimu Juma, alitupilia mbali pingamizi la wakili Jerome Msemwa anayewatetea wadaiwa, la kutaka mahakama hiyo imzuie Mpendazoe asiruhusiwe kuweka kiasi hicho cha fedha mahakamani kwa sababu muda wa kuwasilisha fedha hizo ulikuwa umeishapita.
Jaji Ibrahimu alitupilia mbali pingamizi hilo kwa kuwa halikuwa limekidhi matakwa ya kisheria na badala yake akalikubali ombi la Mpendazoe kuweka mahakama kiasi hicho cha fedha kama dhamana.