Yericko Nyerere
JF-Expert Member
- Dec 22, 2010
- 16,987
- 20,270
Hali ndani ya ccm imezidi kuwa mbaya na ambayo haijawahi kutokea tangu kuundwa kwa chama hiki tangu mwaka 1977,
WAHAFIDHINA ndani ya ccm wameapa kuwa hawapo tayari kuona ccm ikishindwa Uchaguzi ujao, na wapo tayari kufia miguuni kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Tz,
Taarifa za ndani na zakuaminika zinasema mpasuko wenye kutishia hata usalama wa nchi yetu,umeanzaa baada ya Lowassa kulazimishwa na wanausalama kuhudhuria UGAWAJI wa ng'ombe pale Monduli ulioratibiwa na kusimamiwa na Rais Jakaya Kikwete!
Kimsingi inasemekana Lowasa alishaapa kutokaa meza moja na JK, hivyo kitendo cha kulazimishwa kuwepo na kuamuliwa kutoa kauli ya kumsifu jk imemkera sana yeye na wanamtandao wake ndani ya ccm na wamepanga kufanya UASI mkubwa ndai ya CHAMA na ikibidi wanasema (nje ya chama)!
Wakati hilo likijiri kambi ya Samweli Sita nayo imechukizwa sana na hatua ya JK kukaribiana na Lowasa kwani wanasema kitendo cha JK kuwa (maadui) kilikuwa kikiwasaidia wao kujijenga kisiasa na kutimiza malengo yao ya Urais 2015
Hawa nao wanatafakari hatua za kuchukua na inatajwa kuna vikao vya siri vimekuwa vikifanyika Tabora na Masaki vikiratibiwa na wanamtandao wa Sitta!
Kundi lingine ni la Waziri Membe,
Kwanza Membe amekasirishwa sana kuona wanaccm wanamchafua huku mwenyekiti jk akiacha tu hizo rafu bila kupuliza kipyenga, amefika mbali na kusema sasa anajibu mapigo,
Wakati kundi la mwishoo ni la vijana, likiongozwa na Januari Makamba, Emanuel Nchimbi, Nape Nauye nk
Hawa wamestushwa sana na mwenyekiti kuwageuka nakuanza kuwa karibu na Lowasa wakati alishawaahidi kuwa sasa ni zamu ya vijana,
Hili nalo linajiapiza kuwa bora chama kife lakini sio kuongozwa na wazee kwakuwa wameongoza kwa miaka 50 lakini nchi inakuwa kwa kurudi nyuma,
Wakati kundi hili likisema kwa manung'uniko, linaonekana kama linasalitiana kwakuwa baadhi yao wameanza kupingana na kudharauliana wao kwa wao, na wengi wakimtupia lawama Januari na Nape kwa wamekuwa wakijipendekeza kwa Mwenyeti badala ya kujenga umoja wao!
Wadadisi wa siasa za ccm wanasema kuwa hali iliyopo haiwezi kutatulika bila juhudi za vyama marafiki vya nje, kama ANC afrika Kusini, PLO cha Palestina, Frelimo cha Msumbiji,nk
Haya ndugu zangu mungu aepushilie mbali Chama hiki kife bila kurusha miguu maana kitatuingiza kwenye matatizo makubwa!
WAHAFIDHINA ndani ya ccm wameapa kuwa hawapo tayari kuona ccm ikishindwa Uchaguzi ujao, na wapo tayari kufia miguuni kwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Tz,
Taarifa za ndani na zakuaminika zinasema mpasuko wenye kutishia hata usalama wa nchi yetu,umeanzaa baada ya Lowassa kulazimishwa na wanausalama kuhudhuria UGAWAJI wa ng'ombe pale Monduli ulioratibiwa na kusimamiwa na Rais Jakaya Kikwete!
Kimsingi inasemekana Lowasa alishaapa kutokaa meza moja na JK, hivyo kitendo cha kulazimishwa kuwepo na kuamuliwa kutoa kauli ya kumsifu jk imemkera sana yeye na wanamtandao wake ndani ya ccm na wamepanga kufanya UASI mkubwa ndai ya CHAMA na ikibidi wanasema (nje ya chama)!
Wakati hilo likijiri kambi ya Samweli Sita nayo imechukizwa sana na hatua ya JK kukaribiana na Lowasa kwani wanasema kitendo cha JK kuwa (maadui) kilikuwa kikiwasaidia wao kujijenga kisiasa na kutimiza malengo yao ya Urais 2015
Hawa nao wanatafakari hatua za kuchukua na inatajwa kuna vikao vya siri vimekuwa vikifanyika Tabora na Masaki vikiratibiwa na wanamtandao wa Sitta!
Kundi lingine ni la Waziri Membe,
Kwanza Membe amekasirishwa sana kuona wanaccm wanamchafua huku mwenyekiti jk akiacha tu hizo rafu bila kupuliza kipyenga, amefika mbali na kusema sasa anajibu mapigo,
Wakati kundi la mwishoo ni la vijana, likiongozwa na Januari Makamba, Emanuel Nchimbi, Nape Nauye nk
Hawa wamestushwa sana na mwenyekiti kuwageuka nakuanza kuwa karibu na Lowasa wakati alishawaahidi kuwa sasa ni zamu ya vijana,
Hili nalo linajiapiza kuwa bora chama kife lakini sio kuongozwa na wazee kwakuwa wameongoza kwa miaka 50 lakini nchi inakuwa kwa kurudi nyuma,
Wakati kundi hili likisema kwa manung'uniko, linaonekana kama linasalitiana kwakuwa baadhi yao wameanza kupingana na kudharauliana wao kwa wao, na wengi wakimtupia lawama Januari na Nape kwa wamekuwa wakijipendekeza kwa Mwenyeti badala ya kujenga umoja wao!
Wadadisi wa siasa za ccm wanasema kuwa hali iliyopo haiwezi kutatulika bila juhudi za vyama marafiki vya nje, kama ANC afrika Kusini, PLO cha Palestina, Frelimo cha Msumbiji,nk
Haya ndugu zangu mungu aepushilie mbali Chama hiki kife bila kurusha miguu maana kitatuingiza kwenye matatizo makubwa!