Mwanafunzi mwingine wa makamba. Angalia sana aisee,yeye mwenyewe anategemea lifti ya ndege ya mkulu na familia yake siku ya kukimbilia hukooo....(refer mambo ya Tunisia). Kindege chenyewe kidogoo,we haumo aisee...grow up!!!Baada ya sakata la kususia hotuba ya Rais Bungeni na mpasuko uliojitokeza huko, hivi sasa kuna mambo kadhaa ya ndani ya Chadema yanayo ashiri kuisambaratisha Chadema.
1) Kususia Hotuba ya Rais
Hili limetuonyeshaa ni jinsi gani Chadema inavyoendeshwa bila muelekeo, wakati wabunge wao wengi wa-kisusia hotuba ya Rais wengine wengi walisusia shinikizo la Mwenyekiti wao na kuamuwa kuto ingia kabisa bungeni siku hiyo. N awengine tukawaona, usiku huo kwenye hafla ya Rais ilhali viongozi wa Chadema walishinikiza wabunge wa Chadema wote wasiende huko.
2) Kugombea vyeo na nafasi za upendeleo.
Tumeona sakata la nafasi za upendeleo haswa za ubunge jinsi zilivyoleta mvutano ndani ya Chadema na kufikia wana Chademaa wengine kuwachia ngazi, hii ni dalili tosha kuwa utawala wa ndani wa Chadema una mapungufu makubwa.
Tukaona pia jinsi Zitto alivyopigwa chini na Mwenyekiti wake katika kuwania nafasi ya uongozi wa upinzani bungeni. Hali kadhalika tukaona Zitto alivyosulubiwa mpaka kulazwa hiospitali na kupigwa marufuku na uongozo wa Chadema kuwa asiongee na vyombo vya habari kuhusu Chadema kwani yeye si msemaji wa Chadema.
3) Sakata la Arusha:
Tumeona jinsi wengi wa viongozi wa Chadema kutokuhudhuria kwenye maadamano yaliyoshinikizwa na kushadidiwa na viongozi wachache wa Chadema. Na pia tukaona mvutano mkubwa ukitokea katika kutumia maiti kama njia ya kujipatia umaarufu Chadema, ni viongozi wachache wa Chadema walihudhuria "kuaga miili ya marehemu" hao.
Tukaona kuwa hata Fundikira ambae ni Mwenyekiti wa Wenyeviti wa Chadema mkoani Arusha kukataa kuhudhuria muago huo, akisingizia kuwa alikuwa na wageni nyumbani kwake. Wageni zaidi ya Mwenyekiti wake wa Taifaa na Katibu Mkuu wake na Kuaga "wahanga"? hilo ni la kujiuliza.
Ukitazama kwa juu juu utaona hayo si kama mambo ya kawaida, na ukiingia ndani kidooogo, utaona kuwa huo ni mpasuko na mtafuruku mkubwa ndani ya Chadema.
Wenye macho hawaambiwi tazama, na wenye masikio hawaambiwi...
Chama bora ni kile ambacho kinaziona kasoro zake na kuzifanyia kazi.
Hayo yoooote uliyoyasema kuhusu CCM hapa sio mahala pake, anzisha thread yake tutaijibu. Hapa tunaongelea mpasuko bdani ya Chadema, kubali au kataa, upo.
UVCCM jitahidini muokoe chama!Cdm kinawatesa...
Mwanafunzi mwingine wa makamba. Angalia sana aisee,yeye mwenyewe anategemea lifti ya ndege ya mkulu na familia yake siku ya kukimbilia hukooo....(refer mambo ya Tunisia). Kindege chenyewe kidogoo,we haumo aisee...grow up!!!
kwani hayo sio magazeti? Au ulitaka asome tanzania daima?Labda umesoma gazeti la Uhuru/Mtanzania/Habari Leo ndiyo ukafikia conclusion siwezi kukulaumu.
.....................Paid to defend your hegemonic party within pluralistic system........
...........antithetical to democracy
.....Utachoka mwisho wa siku, tumeshakichoka ki-CCM chako..............
waambie na hao wanaokulipa pia...tumewachoka na HADANGANYIKI MTU....Nyie bwabwajeni tu kama mnavuja....
Lbada ni makosa kuwaonyesha mapungufu? ambayo ni ya kweli tupu, watu wenye maana na mawazo wangema mnhhhh, huyu outsider kayaona haya, hebu tutazame namna ya kuyarekebisha.
Hayo ndi matatizo ya chadema kuanzia misukule mpaka viongozi, hamna kina cha kufikiri.
Ingekuwa "ukweli mtupu" wala usingekuwa na haja kutetea.Wewe sio outsider wala insider,you simply are a poor soul trying to serve your masters ili mkono uende kinywani.Hivi ukitakiwa "kufanya mengine" zaidi ya kutimiza maagizo ya kazi hapa JF,utakataa?Usiuze utu wako
Tangu lini CCM ikatoa mawazo yanayosaidia kukijenga CHADEMA? Zomba usipoteze muda kwa yasiyokuhusu na kutaka tuache mambo ya msingi kama Katiba Mpya na malipo haramu ya DOWANS na kujadili mpasuko hewa wa CHADEMA!
mimi nadhani umefika wakati wa kukubali makosa na kuanza kuyashughurikia mapema iwezekanavyo,sio kila jambo liwekwalo hapa juu ya chadema lina lengo la kuiyangusha ama kuichamba chadema,tuwe wenye kupima na kukubali na kuona ukweli kwa yale yatokeayo na ikiwezekana tuyatafutie dawa
kinacho nishangaza kwa chadema sisi ni kuwa hatukubali kuwa kuna tatizo na tunajifanya hatuoni yaliyotokea huu ni mwelekeo hasi kwa viongozi walio makini na walioive kisiasa
inamaanisha hata tukipewa nchi haya ndiyo majibu tutakayo kuwa tukiyatowa kwa wapiga kura wetu,kwani kila jambo linaloangukia kwetu chadema ilimradi tu limeonyesha kushindwa kwetu huwa hatuko tayari kukubaliana nalo na hata hatuko tayari kulitaftia uvumbuzi
zaidi ni kimtusi mtoa mada kana kwamba alichokitowa hakikufanyika ARUSHA.
Tubadilike kama kweli tunataka kuwaongozi WTZ tuondoe fikra hasi na mgando tulizonazo juu mada zote hasi kwa chadema,si kila siku CDM Tuko safi some times kunamatatizo na nilazima tuyakubali na kuyataftia ufumbuziiiii
MSEMA UKWELI HAPENDWI DAIMAAAAAA
mapinduziiii daimaaaa
Kumbe ndo mahala pako pa kupotezea muda hapa....aaaggghrrr!!!! IF YOU'VE GOT NOTHING TO DO PLEASE DON'T DO IT HERE!!! GO DO IT S'WHERE ELSE!! Nakushauri nenda pale Lumumba kuna kijiwe flani cha kahawa na majungu kitakufaa sana mtu kama wewe...Tena sana, hasa pale tunapoona kina sambaratika. Tutakosa hamasa. Kama vile Yanga wakiwa hawapo Simba nayo itasikitika na vice versa.
Chadema mkisambaratika, sijui tutampata nani wa kupoteza nae muda hapa JF.
kwani hayo sio magazeti? Au ulitaka asome tanzania daima?