Mpango wa siri wa kujenga taifa la wajinga

View attachment 1323
sijaelewa umekusudia kuua kivipi?

hawa wanafunzi wanafanya mitihani. na rangi ya njano level nyengine na hao wengine.

kurahisisha usimamizi wamewekwa pamoja, tatizo liko wapi?


kwani form four na form six si inakaribiana na hivyo wengi kwenye hall?


Nakubalina kabisa huu ni mpango wa siri wa SISIEMU wa kujenga Taifa la Wajinga.

Nani kakwambia wanafanya mtihani?

Sawa, kama wanafanya mtihani so what? Ndiyo wakae chini?

"kwani form four na form six si inakaribiana na hivyo wengi kwenye hall?" Hii sentensi haina maana yeyote.

Wana JF.
Kama mtu huwezi elewa kinachoendelea kwa kuiangalia picha hiyo, basi ni vigumu sana kuelewa kwamba Tanzania si nchi ya Viwanda.
Pia kwa mtaji huo ni vugumu kuelewa tofauti ya mshona Viatu(kilabata), mpinga rangi viatu na mtaalamu wa kufua chuma cha pua wa kule Korea ya kusini au Japan.
Pia kushindwa kuisoma na kuitafsiri picha hiyo ni dalili moja wapo kwamba somo kwamba Tanzania ni iko Dunia ya tatu katika mizania za maendeleo na nchi kama Sweden Japan na Amerika ziko dunia ya kwanza.
Ni masikitiko makubwa kabisa kuona mtu anaweza kunena maneno makuu katika imani ya dini kampeni za kisiasa na hata katika mkusanyiko wa harusi,lakini mtu huyo huyo hawezi kutambua dalili muhimu za udumavu wa elimu.
Mungu alitupa akili, lakini utashi wa kuzitumia akili katika namna nzuri alituachia wenyewe.
Kwa uhodari wa kutumia shoka wengine huamua kukata vichwa vya watu.
Kwa uhodari mahesabu wengine huamua kupika mahesabu na kuiba.
Kwa uhodari wa tiba na utatifi wengine huamua kuanzisha magonjwa mapya.
Kwa uhodari wa kuongea na kushawishi wengine huamua kuupeleka umma wote kwenye matatizo mkubwa ya kiuchumi.
Bado ni utashi wa bin adam kutumia akili aliyo pewa na Mungu katika mwelekeo ulio sahihi.

Katika nchi iliyopata uhuru zaidi ya miaka 47 iliyopita, mwanafunzi katika darasa la shule yeyote ile katika kijiji chochote kile hastahili kukaa chini wakati akifundishwa au akifanya mtihani au akisubiri mwalimu aingie darasani.
Miaka 47 ni mingi ya kutosha kupanga mipango sahihi ya elimu na kuacha upuuzi na utani kama huu tuuonao katika picha.

Juzi hapa tumeambiwa na Mzembe mmoja kwamba Tanzania INAPAA.
Leo hii shule iliyopo umbali wa chini ya Maili 5 kutoka Ofisi na nyumbani kwa Juha yule kuna Wanafunzi Jalo wamekaa chini darasani wakifundishwa.
Eti inapaa!

Kumradhi, nashindwa kuelewa maana ya kupaa ni nini?
MH yule pengine alifikia hatua ya kusema Inapaa kwa sababu yeye binafsi ametoka mbali na hakutegemea hata siku moja kufikia hapo alipo fikia.
Fikiria,Kutoka kufunga Lubega hadi kuvaa suti pande mbili na mjusi juu na zile suti za nipishe nijambe. Kubadili magari kama nguo za ndani, kumechisha gari na nguo nk.
MH huyu kweli aliona ni maendeleo makubwa yanayo patikana mawinguni tu kwa hiyo ni lazima Tanzania inapaa, asitambue kwamba yeye pekee anapaa akizungukwa na nzi wa kizungu.

Kama hatuwezi kuelewa matatizo ya elimu nchini Tanzania au tunaelewa na kuyapuuzia kwa sababu wadogo zatu wanasoma Bunge Primary school kuliko na madawati ya ziada, basi ni lazima tuelewe kwamba majadiriano juu ya mambo mengine yote yaliyo baki ni mazungumzo baada ya habari. Safari nyingine tukifungua enternet ni bora tulog kule whitehouse.com

Elimu ni Ufunguo wa maarifa yote duniani.
Ndiyo maana wenzetu wote wa dunia ya kwanza hawana mchezo wala ujinga katika masuala ya Elimu.
Wenzetu elimu wanaiangalia yote kwa ujumla wake, kuanzia kindergarten mpaka University.
Kuanzia kusoma Historia za utafiti wa zamani mpaka kufanya utafiti mpya hapa duniani na katika anga za juu.

Nina shangaa kuona mtu na akili zake timamu anashindwa kuelewa tatizo lililo wazi kabisa la watoto wa shule kukaa chini wakati wa kusoma.
Pengine mtu mwingine anaona tendo la wanafunzi kukaa chini wakiwa masomoni ni kawaida, hasa akizingatia jadi yake au utamaduni wa imani yake au vyote.
Lakini kwa utamaduni na imani hiyohiyo hata sijaona imani hiyo ya kukaa chini ikihamishiwa ikulu au kwenye Bunge.Kwenye maofisi yote kila mmoja nahusu utamaduni wa kukaa juu ya vipande vya miti kaa kima.

Ninashangaa kwa nini mtu mwenye akili timamu anashindwa kuelewa kwamba kuna jambo kubwa lisilo la kawaida linaendelea katika mfumo wa siasa na uchumi wa Tanzania endapo miaka 47 baada ya Uhuru watoto wa shule bado wana kaa chini sakafuni.

Tena si watoto wa shule za msingi tu, hata Univeristy of DSM wanafunzi wana kaa chini na wakati huo huo MH Kikwete anapita kila nchi kwa mbwembwe kuomba fedha za kujengea chuo kingine wakati tulicho nacho darasa moja lina watu 1000 katika chumba maalumu kwa wanafunzi 150.
Siyo tu wana kaa chini wengine wanachungulia madirishani wakiwa nje ya chumba cha darasa.

Tumeita mshauri toka Japan aje atushauri namna ya kuukata kama wao wajapan.
Ushauri wa mjapan huyu ukifanyiwa kazi watu wa kuja kuutekeleza kwa vitendo ni hao jamaa waliokaa chini. Sijui ni kwa kiwango gani watu waliosoma katika mazingira hayo ya kukaa chini watakuwa tayari kuyafanyia kazi maagizo ya huyu mjapan.

Kuna watu wanaandika maneno hapa mpaka unawahurumia, na hata kukufanya uamini kwamba pengine mawazo waliyo yaandika hayakutoka kwenye bongo zao ila yalitoka kwenye misuli ya mikono yao.

Sijui ni uwezo wa kufikiri umegonga Glass Ceiling au ni ushabiki wa kisiasa uliovuka mipaka?

Sijui ujasiri wa kutetea na kuona fahari kwamba wanafunzi katika picha wamekaa chini kinyume na madai ya viongozi wa chama na serikali unatoka wapi?

Hata ukiwa na Roho mbaya kuliko ibilisi mwenyewe, katika damu yako walau kutakuwa na chembe za ubinadamu.

Kukauka kisabuni na kushindwa kuona udhaifu wa chama tawala na serikali yake wa kushindwa kuimarisha elimu sambamba na mahitaji ya watanzania ni ugumu unao karibiana na uhaini.

Mtu asiyeona umuhimu wa shule kuwa na vyumba vya madarasa vya kutosha na kuhakikisha watoto wote wana madawati ya kukalia ni vema mtu huyu akubali kwamba kwake yeye fedha mfukoni ni bora kuliko elimu.
Laiti mtu huyo angejua kwamba Masheikh wa Saudia ndiyo wenye fedha nyingi kuliko lakini walio kwenda shule ya kutakata ndiyo wanao iongoza dunia tena wanaiongoza kibabe!
 
mie hujiuliza kulikoni kupinga na kushutumu kila kitu, hata kwa hoja nyaufu kisai hiki.

hivi nani asiejua kuwa jitihada zinafanyika kunyanyua elimu tanzania?

hivi kuonesha darasa moja la skuli kukaa chini ndio kigezo cha kuandaa wajinga?

tupeni takwimu tulikuwa na shule ngapi na walimu wangapi na sasa tuko wapi?

maendeleo si jambo la siku moja, hiki ni kipindi cha mpito tumo kwenda na jitihada zipo, ila wako wahuni na wababaishaji wengi ktk watanzania ambao ni watendaji bila ya kujali vyama vyao au itikadi zao ambao hurejesha nyuma jitihada hizo kwa matashi yao


mbona nchi za wenzetu yako madaarasa wanasoma chini ya miti tena kwenye vumbi, hao angalau wako kwenye jengo na wamekaa juu ya sakafu ya saruji.


bado sijashawishika kama kuna lengo la kuua elimu, ni kweli sijaridhika na hali hii na nnaamini mm ni mmoja ambae nnaamini msaada wangu unahitajika kusaidia elimu na mengine badala kudoea kutafuta udhaifu ili nichonge kwa saaana


Ukiwa na Afya hujilinganishi na mgonjwa kujua kiwango cha afya yako.

Nchi za kuigwa katika kukuza elimu yetu Tanzania ni lazima ziwe zile za ulimwengu wa kwanza.
Tukianza kujilinganisha na Msumbiji, Malawi, Congo, Sudan ya Kusini, Somalia Liberia Siera Leone na Angola katika ubora wa Elimu; haitakuwa tofauti na Kijana mwenye afya kujilinganisha na mgonjwa wa Mwaisela pale Muhimbili.

Wenzetu wamepigana vita tangu nchi zao zipate Uhuru, sisi vita yetu imepiganwa majukwaani kwa vipaji vya wasema uongo wa kurudia rudia. Risasi za ndimi zao zimetujaza viraka kwenye kaptula zetu Kanga zetu kanzu zetu hata nguo zetu za ndani, kwa umasikini wa kujitakia.

Sisi tuliotembea nchi nzima na kujionea mengi kwa macho yetu tunajua fika kwamba vijana wetu kuendelea kusoma shule katika mazingira duni na yenye kutoa elimu duni ni matokeo ya siasa duni na za ubabaishaji.

Ni matokeo ya kuunda kamati za Uchumi na mipango ndani ya chama kwa kuzingatia ukubwa wa midomo ya wasemaji na si hekima ya maneno yao au elimu na ufahamu wa uchumi na mipango yenyewe.Aidha, ni kutawaliwa na hofu za hirizi na ibada za giza.

Kitu kibaya zaidi ni kwamba; ujinga ulianzishwa na baadhi ya waasisi waliokuwa na nguvu za kupenyeza mawazo yao,wengi walishatutoka siku nyingi kwa umri wao mkuu, bado unadumishwa na kulindwa kwa nguvu zote na makinda walio uzao wa itikadi mfu za vikongwe hao.

Kitu kizuri ni kwamba; himaya zote zilizo jengwa kwa mapokeo yenye mafukizo yote haramu ya kikoloni na kibwanyenye na itikadi iliyojengwa kwa kugandisha mawazo ya watu kwa baridi la hofu ya kuhofia visivyo hofiwa , taratibu zinapoteza uimara wa wimo wake na kulegea. Upotevu wa uimara wa misingi ya kudumaza mawazo na maendeleo ya Watanzania unatokana na ongezeko la fukuto la mapambano ya kujikomboa na kujinasua katika mzunguko wa umasikini.

Jitihada za kuzuia fukuto hilo kutoka kwa wanasiasa wababaishaji na makuwadi wao zinabuma kila dakika inayopita.
 
Ni aibu tena aibu kubwa kwa nchi yetu kuwa na wanafunzi wanaokaa chini. Hivi kutengeneza madawati kunahitaji fedha za kigeni? Au mbao za kutengenezea madawati tunahitaji kuagiza kutoka nje ya nchi?

Kuna pesa zilichangishwa kwa ajili ya sherehe za miaka 45 ya Uhuru, makampuni yakachanga mamia ya mamilioni ya pesa. Kuna pesa pia zilichangishwa kupambana na baa la njaa, zikachangwa pesa nyingi sana. Hivi leo hii Waziri Mkuu akisimama kidete kabisa na kutangaza rasmi kwamba tunataka kuondoa tatizo la wanafunzi kukaa chini, pesa hazitapatikana!

Niuzembe na kutojali na kutojali au ni kweli kuna ajenda ya siri ya kujenga taifa la watu wasioweza kuhoji chochote! Kama hili la pili ni la kweli, basi dhambi hiyo itawafuata viongozi wetu mpaka makaburini kwao na hata kwa vizazi vyao!
 
mie hujiuliza kulikoni kupinga na kushutumu kila kitu, hata kwa hoja nyaufu kisai hiki.

hivi nani asiejua kuwa jitihada zinafanyika kunyanyua elimu tanzania?

hivi kuonesha darasa moja la skuli kukaa chini ndio kigezo cha kuandaa wajinga?

tupeni takwimu tulikuwa na shule ngapi na walimu wangapi na sasa tuko wapi?

maendeleo si jambo la siku moja, hiki ni kipindi cha mpito tumo kwenda na jitihada zipo, ila wako wahuni na wababaishaji wengi ktk watanzania ambao ni watendaji bila ya kujali vyama vyao au itikadi zao ambao hurejesha nyuma jitihada hizo kwa matashi yao


mbona nchi za wenzetu yako madaarasa wanasoma chini ya miti tena kwenye vumbi, hao angalau wako kwenye jengo na wamekaa juu ya sakafu ya saruji.


bado sijashawishika kama kuna lengo la kuua elimu, ni kweli sijaridhika na hali hii na nnaamini mm ni mmoja ambae nnaamini msaada wangu unahitajika kusaidia elimu na mengine badala kudoea kutafuta udhaifu ili nichonge kwa saaana

Mtu wa pwani heshima mbele,

Labda ungesaidia wana JF kwa kuwaambia kuwa matumizi ya pesa ya kodi ya serikali kuu ni yapi - kama pesa haitumiki kwenye elimu afya na huduma muhimu za maisha kama maji na umeme au barabara na mawasiliano basi kuna sababu gani ya kulipa kodi?
 
Mtu wa pwani heshima mbele,

Labda ungesaidia wana JF kwa kuwaambia kuwa matumizi ya pesa ya kodi ya serikali kuu ni yapi - kama pesa haitumiki kwenye elimu afya na huduma muhimu za maisha kama maji na umeme au barabara na mawasiliano basi kuna sababu gani ya kulipa kodi?

Nimeona kila siku hapa Dar kwenye TV Kandoro anakusanya pesa za kujenga madarasa mi yapi haya ? Tabata haiko Dar ?Hali hii ni Dar je mikoani kuna maisha gani?
 
Nimeona kila siku hapa Dar kwenye TV Kandoro anakusanya pesa za kujenga madarasa mi yapi haya ? Tabata haiko Dar ?Hali hii ni Dar je mikoani kuna maisha gani?

Haya wao hawataki kuyajadili na ndio maana wanakimbilia kujadili mambo eti Mbowe amefanya mapenzi na mama mkapa! Mimi nakubaliana na hii thread kuwa ccm ina mpango wa siri wa kuua elimu Tanzania maana haya ni makusudi kabisaaa na wala sio kingine!
 
Ukiwa na Afya hujilinganishi na mgonjwa kujua kiwango cha afya yako.

Nchi za kuigwa katika kukuza elimu yetu Tanzania ni lazima ziwe zile za ulimwengu wa kwanza.
Tukianza kujilinganisha na Msumbiji, Malawi, Congo, Sudan ya Kusini, Somalia Liberia Siera Leone na Angola katika ubora wa Elimu; haitakuwa tofauti na Kijana mwenye afya kujilinganisha na mgonjwa wa Mwaisela pale Muhimbili.

Wenzetu wamepigana vita tangu nchi zao zipate Uhuru, sisi vita yetu imepiganwa majukwaani kwa vipaji vya wasema uongo wa kurudia rudia. Risasi za ndimi zao zimetujaza viraka kwenye kaptula zetu Kanga zetu kanzu zetu hata nguo zetu za ndani, kwa umasikini wa kujitakia.

Sisi tuliotembea nchi nzima na kujionea mengi kwa macho yetu tunajua fika kwamba vijana wetu kuendelea kusoma shule katika mazingira duni na yenye kutoa elimu duni ni matokeo ya siasa duni na za ubabaishaji.

Ni matokeo ya kuunda kamati za Uchumi na mipango ndani ya chama kwa kuzingatia ukubwa wa midomo ya wasemaji na si hekima ya maneno yao au elimu na ufahamu wa uchumi na mipango yenyewe.Aidha, ni kutawaliwa na hofu za hirizi na ibada za giza.

Kitu kibaya zaidi ni kwamba; ujinga ulianzishwa na baadhi ya waasisi waliokuwa na nguvu za kupenyeza mawazo yao,wengi walishatutoka siku nyingi kwa umri wao mkuu, bado unadumishwa na kulindwa kwa nguvu zote na makinda walio uzao wa itikadi mfu za vikongwe hao.

Kitu kizuri ni kwamba; himaya zote zilizo jengwa kwa mapokeo yenye mafukizo yote haramu ya kikoloni na kibwanyenye na itikadi iliyojengwa kwa kugandisha mawazo ya watu kwa baridi la hofu ya kuhofia visivyo hofiwa , taratibu zinapoteza uimara wa wimo wake na kulegea. Upotevu wa uimara wa misingi ya kudumaza mawazo na maendeleo ya Watanzania unatokana na ongezeko la fukuto la mapambano ya kujikomboa na kujinasua katika mzunguko wa umasikini.

Jitihada za kuzuia fukuto hilo kutoka kwa wanasiasa wababaishaji na makuwadi wao zinabuma kila dakika inayopita.

Kinachoumiza zaidi ni kuwa shule wanalazimishwa watu kuchangia na yule asiyenapesa anawekwa jela hadi miezi sita kwa hili? Hii inaita kuuliza kama kazi ya serikali ni kutumbua mapesa kwa magari na ndege za kifahari au kutumia pesa za kodi ili kutoa huduma za jamii!?!?!?!?!
 
Hili suala la watoto kukaa chini tuliangalie vile vile kwa kutumia kurunzi ya "uzazi wa mpango" Hivi hawa watoto wanaokaa chini, huko majumbani kwao wanakotoka wanaishi vipi??? Pamoja na ukweli kwamba serikali inawajibika kutengeneza madawati nk, je hao wazazi wenye watoto katika hizo shule wanayamudu vipi maisha yao ya kila siku??? Elimu ya uzazi wa mpango ni muhimu kwa hao watoto waliokaa chini!!
 
Mi hata sioni kama ni mpango wa siri, naona ni mpango wa wazi kabisa.

Linganisha idadi ya graduate wetu, si na Uingereza wala Marekani, bali Kenya tu utajua.Priority katika elimu hamna, wasomi wanaingiliwa na wanasiasa.Walioiba vyeti kama kina Nchimbi, Mkullo Nagu na Mathayo ndiyo wanapewa Uwaziri.

Halafu kuna mpango wa siri hapo? Siri iko wapi?
 
Mi hata sioni kama ni mpango wa siri, naona ni mpango wa wazi kabisa.

Linganisha idadi ya graduate wetu, si na Uingereza wala Marekani, bali Kenya tu utajua.Priority katika elimu hamna, wasomi wanaingiliwa na wanasiasa.Walioiba vyeti kama kina Nchimbi, Mkullo Nagu na Mathayo ndiyo wanapewa Uwaziri.

Halafu kuna mpango wa siri hapo? Siri iko wapi?

Mzee unanichekesha sana hahahahah Kilaza Nchimbi, Nagu, Mkullo, Mathayo, Kamala mawaziri kwenye sirikali, nasikia muungwana atalifanyia kazi baada ya JF kulivalia njuga.....
 
Atugawie sehemu ya mshahara wake basi, maana kila kitu mpaka JF ipigie kelele, yeye anafanya initiative gani?
 
Atugawie sehemu ya mshahara wake basi, maana kila kitu mpaka JF ipigie kelele, yeye anafanya initiative gani?

kweli kabisa inabidi asaidie kulipa gharama za kuiendesha JF ili asipate ushauri wa bure hapa maana hakuna free lunch anyway!
 
Mi hata sioni kama ni mpango wa siri, naona ni mpango wa wazi kabisa.

Linganisha idadi ya graduate wetu, si na Uingereza wala Marekani, bali Kenya tu utajua.Priority katika elimu hamna, wasomi wanaingiliwa na wanasiasa.Walioiba vyeti kama kina Nchimbi, Mkullo Nagu na Mathayo ndiyo wanapewa Uwaziri.

Halafu kuna mpango wa siri hapo? Siri iko wapi?

Inaonekana kabisa kuwa huu mpango sasa umekuwa wazi maana kama watu wenyewe ni kina Nchimbi na Mkullo basi mambo yote yako wazi kabisaaaa!
 
Wachangiaji:

Hiyo picha aionyeshi kipya. Hiyo ni hali ya shule za Tanzania kwa zaidi ya miaka 30 sasa.

Kuna sehemu tulikosea. Sehemu tuliyokosea ni kukubali kuwa BURE kuwa sub-standard. Tulipomruhusu rais wa kwanza kutoa vitu bure kwa sub-standard, inakuwa vigumu kuwaambia wanaomfuatia kuongoze ubora wa vitu wanavyotoa. Na tatizo kubwa linalokuja ni kuwa watu wamekubali kuwa huo ni utamaduni.
 
Wachangiaji:

Hiyo picha aionyeshi kipya. Hiyo ni hali ya shule za Tanzania kwa zaidi ya miaka 30 sasa.

Kuna sehemu tulikosea. Sehemu tuliyokosea ni kukubali kuwa BURE kuwa sub-standard. Tulipomruhusu rais wa kwanza kutoa vitu bure kwa sub-standard, inakuwa vigumu kuwaambia wanaomfuatia kuongoze ubora wa vitu wanavyotoa. Na tatizo kubwa linalokuja ni kuwa watu wamekubali kuwa huo ni utamaduni.

Kama kungekuwa na sehemu ambako mtu angeweza kuomba wafu warudi kuwa hai hata kwa dakika moja, Naamini kabisa ningekuwa wa kwanza kwenda huko na kudai Nyerere afufuke ili apewe lawama zote kwa yale yanayoendelea miaka 20 baada ya yeye kuachia ngazi na miaka 10 baada ya kifo chake!

Poor guy, naamini hata miaka 100 ijayo watu watakuwa wanamlaumu kwa kila kitu. Laiti wamarekani wangekuwa na hii attitude basi naamini leo watu wangekuwa bado wanamlaumu Jimmy carter kwa kile kilichotokea mwishoni mwa miaka ya 70!
 
Nafikiri hiki kichwa cha habari ni misleading. Ni kweli kwamba kuna matatizo ya uhaba wa madawati, madaftari, penseli, choki n.k. But i dont see that as a way kujenga taifa la wajinga ! Akili ya mtu haiji kwa kukaa kwenye dawati, na kama utakumbuka (sijui wewe ni wa mwaka gani) lakini wengi nadhani humu wamesoma katika sehemu ambazo kwa kweli tukiangalia nyuma zile sehemu, haziridhishi na still tuliweza kusoma !

Topic ni very misleading !
 
Jamani lets try see things from a CCM perspective...they are lost lambs..victims of circumstance...they been messing up for so long its normal..sasa times are changing the media is exposing things..hawajui waanze wapi kijisafisha ...its crazy guys..lol...tukae tuangalie movie ya Scarface...Tony Montana=CCM...he is destroying himself..hamna cha upinzani wala nini...JF has ruined so many peoples dreams of getting into politics thru CCM..As much as i hate to say this it seems CCM will have the same fate as KANU of kenya...its a matter of time...
 
Kama kungekuwa na sehemu ambako mtu angeweza kuomba wafu warudi kuwa hai hata kwa dakika moja, Naamini kabisa ningekuwa wa kwanza kwenda huko na kudai Nyerere afufuke ili apewe lawama zote kwa yale yanayoendelea miaka 20 baada ya yeye kuachia ngazi na miaka 10 baada ya kifo chake!

Poor guy, naamini hata miaka 100 ijayo watu watakuwa wanamlaumu kwa kila kitu. Laiti wamarekani wangekuwa na hii attitude basi naamini leo watu wangekuwa bado wanamlaumu Jimmy carter kwa kile kilichotokea mwishoni mwa miaka ya 70!

Aunt:

Nimesema tulikosea kwa kukubali bure zilizo chini ya sub-standards na matokeo tunashindwa kuuliza ubora wa kile tunachopewa na sirikali yetu tukutu.

Lakini kama tungekuwa na watu kama wewe miaka 30 iliyopita wanaocheza machale yao na kuuliza kulikoni? Tusingefika hapa tulipo. Hilo ni somo la kujifunza na hatuhitaji mtu kukufuka.
 
Aunt:

Nimesema tulikosea kwa kukubali bure zilizo chini ya sub-standards na matokeo tunashindwa kuuliza ubora wa kile tunachopewa na sirikali yetu tukutu.

Lakini kama tungekuwa na watu kama wewe miaka 30 iliyopita wanaocheza machale yao na kuuliza kulikoni? Tusingefika hapa tulipo. Hilo ni somo la kujifunza na hatuhitaji mtu kukufuka.

Bin Maryam,

Asante sana kwa maelezo ya hili. Yaliyotokea miaka 45 iliyopita ni historia sasa. Ukiangalia kwa makini utagundua kuwa kuanzia mwaka 1984 Tanzania ilipokubali rasmi kushauriwa na IMF mambo yalibadilika significantly.

Inasikitisha bado kuwa hata pamoja na kuwa na IMF kwa miaka yote hiyo bado mambo yamekuwa mabovu zaidi kuliko hata maisha ya kabla yao IMF.

Msingi wa matatizo ya Tanzania ni ccm, hadi muda ambapo itatoka madarakani na watu kama Mramba, Mkapa na wenzake wakawekwa ndani, nchi itakuwa ni the living hell!
 
Bin Maryam,

Asante sana kwa maelezo ya hili. Yaliyotokea miaka 45 iliyopita ni historia sasa. Ukiangalia kwa makini utagundua kuwa kuanzia mwaka 1984 Tanzania ilipokubali rasmi kushauriwa na IMF mambo yalibadilika significantly.

Inasikitisha bado kuwa hata pamoja na kuwa na IMF kwa miaka yote hiyo bado mambo yamekuwa mabovu zaidi kuliko hata maisha ya kabla yao IMF.

Msingi wa matatizo ya Tanzania ni ccm, hadi muda ambapo itatoka madarakani na watu kama Mramba, Mkapa na wenzake wakawekwa ndani, nchi itakuwa ni the living hell!

Aunt:

1984 kabla ya mikataba na IMF kuingia ndo nilianza four one. Kutoka Mwanza kwenda Musoma shuleni ilinichukua zaidi ya wiki moja.

Meli, mabasi, treni zilikuwa hazifanyi kazi kwa ukosefu wa mafuta. Kama sikosehi waLibya walileta meli ya mafuta na serikali ilishindwa kulipa.

Hali ilikuwa mbaya sana kabla ya kuingia mikataba na WB na IMF. Nadhani Mzee Mtei anaweza kutoa somo hapo kwanini aliachia ngazi.

Tatizo linalokuja ni kuwa hatujaweka Priorities zetu right. Baada ya kuchukua mikopo migumu, kitu cha kwanza wabunge wakadai magari mapya hili waweze kutembelea majimbo yao vijijini. Wajumbe wa NEC nao wakadai magari ya nguvu.

Tuachene kulaumu IMF au WB, tuna matatizo ya akili sisi wenyewe.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom