Elections 2010 Mpaka wanaotaabika watakapoliona tatizo

Hekima Ufunuo

JF-Expert Member
May 28, 2009
220
11
Uchaguzi wa Mwaka huu hautaleta mabadiliko makubwa kwenye ngazi ya Raisi na hata Wabunge na Madiwani pamoja na kwamba hapa JF panaonyesha kuwa watu wanamwamko mkubwa wa mabadiliko.

Nikiangalia utafiti wa kura ambao unaendeshwe na JF, inaonyesha kuwa mwaka huu utakuwa na mabadiliko makubwa katika ushindi kwa wapiganaji na wapenda mabadiliko (Upinzani). Nikichukua ushindi huu wa hapa JF nikaupeleka kwa wapiga kura, matokeo yanakuja tofauti.

Inaniuma sana kwamba kuna miaka mingine mitano ya kuendelea kushuhudia malumbano yasiyokuwa na tija kwa Taifa huku watu wakijineemesha wenyewe na familia zao. Foleni ikiendele kuwa jambo la kawaida kwa wakazi wa DSM, Mwanza, Arusha. Wizi wa rasilimali za bahari ukiendelea kama kawaida. MIsitu na utalii vikiendelea kudorora kwa kutonufaisha taifa na wenye akili zao kunufaika pasipo na wa kuwadhibiti. Wakinamama wakijifungu kwenye lango la hospitali na wengine kulala chini au mzungu wa nne bila wa kuwaonea huruma wala kuleta majibu. Sukari na unga vikiendelea kupanda bei pasipo na wa kuhangaika navyo kama bidhaa muhimu kwa jamii. Dola ikiendelea kutumika katika taifa lenye uhuru wa miaka hamsini wakati lina sarafu yake ya shilingi. Aridhi ikichukuliwa na wageni pasipo na wa kuhoji. Elimu ikiendelea kudorora kwa kufikisha kidato cha nne watoto ambao hawajui kusoma wala kuandika. (inakuwaje mtoto asiyejua kusoma wala kuandika anafaulu darasa la saba?) Ufisadi ukiendelea kulitesa taifa kama vile halina uongozi. Majambazi yakiendelea kuuwa watu pasipo na wa kuwatisha ama kusimamia sheria (Jhwani Mwaikusa ni mfano tu wa Watanzania wengi wanaokufa kwa ujambazi) Pensheni kwa wazee ikiendelea kuwa ndoto kwao baada ya kutaabika kwa mika mingi ya utumishi. (kima cha chini cha pensheni kwa mstaafu ni 52,000?=, Kinatosha nini kwa nchi ambayo sukari kilo ni shilingi 2,000?=?) na mengine mengi.

Haya yote yatafikia tamati siku "WANAOTAABIKA WATAKAPOLIONA TATIZO"

Mpaka sasa wanaoliona tatizo siyo wanaotaabika, wanaoweza kuingia JF Wanaliona Tatizo lakini hawataabiki. Kilo ya sukari kuuzwa sh. 2,000/= kwake ni tatizo lakini lenye majibu. Mke au mume wake hawezi kulala sakafuni muhimbili wakati wa kujifungua au anapoumwa kwa sababu anaweza kulipia fast truck na akapewa kitanda. Nauli za Daladala kupanda ni tatizo lakini kwa mwana JF anao uwezo wa kukabiliana na hilo tatizo. Wale ambao haya ni matatizo kwao kwa kutokuwa na uwezo wa kukabiliana nayo HAWAJAYAONA hivyo wanataabika tu bila msaada.

Kura ya JF siyo hali halisi kule kwa wapiga kura ambao hawalioni tatizo.

Kuwafanya walione tatizo, tufanyeje????????

Respect
 
njia zifuatazo zaweza kuwasaidia.
  • kuandika makala za uchambuzi unaohusianisha taabu watanzania wanazopata na kuzihusianisha vyema na utawala mbivu tulio nao madarakani
  • viongozi makini wa vyama kutumia mikutano ya kampeni kuhusianisha na kufafanua kwa wananchi kwenye mikutano ya kampeni chanzo hasa cha hali ngumu ya maisha inayoletwa na utawala mbovu.
  • viongozi wa dini na taasisi binafsi kuendeleza kampeni za kupinga ufisadi, kuelimisha jinsi ya kchagua viongozi bora na wazalendo
  • kwa sisi tuliokwisha kuelewa tutitokeze na kuhamasisha wale walio karibu yetu kupiga kura ya mabadiliko ya kweli.
 
Uchaguzi wa Mwaka huu hautaleta mabadiliko makubwa kwenye ngazi ya Raisi na hata Wabunge na Madiwani pamoja na kwamba hapa JF panaonyesha kuwa watu wanamwamko mkubwa wa mabadiliko.

Nikiangalia utafiti wa kura ambao unaendeshwe na JF, inaonyesha kuwa mwaka huu utakuwa na mabadiliko makubwa katika ushindi kwa wapiganaji na wapenda mabadiliko (Upinzani). Nikichukua ushindi huu wa hapa JF nikaupeleka kwa wapiga kura, matokeo yanakuja tofauti.

Inaniuma sana kwamba kuna miaka mingine mitano ya kuendelea kushuhudia malumbano yasiyokuwa na tija kwa Taifa huku watu wakijineemesha wenyewe na familia zao. Foleni ikiendele kuwa jambo la kawaida kwa wakazi wa DSM, Mwanza, Arusha. Wizi wa rasilimali za bahari ukiendelea kama kawaida. MIsitu na utalii vikiendelea kudorora kwa kutonufaisha taifa na wenye akili zao kunufaika pasipo na wa kuwadhibiti. Wakinamama wakijifungu kwenye lango la hospitali na wengine kulala chini au mzungu wa nne bila wa kuwaonea huruma wala kuleta majibu. Sukari na unga vikiendelea kupanda bei pasipo na wa kuhangaika navyo kama bidhaa muhimu kwa jamii. Dola ikiendelea kutumika katika taifa lenye uhuru wa miaka hamsini wakati lina sarafu yake ya shilingi. Aridhi ikichukuliwa na wageni pasipo na wa kuhoji. Elimu ikiendelea kudorora kwa kufikisha kidato cha nne watoto ambao hawajui kusoma wala kuandika. (inakuwaje mtoto asiyejua kusoma wala kuandika anafaulu darasa la saba?) Ufisadi ukiendelea kulitesa taifa kama vile halina uongozi. Majambazi yakiendelea kuuwa watu pasipo na wa kuwatisha ama kusimamia sheria (Jhwani Mwaikusa ni mfano tu wa Watanzania wengi wanaokufa kwa ujambazi) Pensheni kwa wazee ikiendelea kuwa ndoto kwao baada ya kutaabika kwa mika mingi ya utumishi. (kima cha chini cha pensheni kwa mstaafu ni 52,000?=, Kinatosha nini kwa nchi ambayo sukari kilo ni shilingi 2,000?=?) na mengine mengi.

Haya yote yatafikia tamati siku "WANAOTAABIKA WATAKAPOLIONA TATIZO"

Mpaka sasa wanaoliona tatizo siyo wanaotaabika, wanaoweza kuingia JF Wanaliona Tatizo lakini hawataabiki. Kilo ya sukari kuuzwa sh. 2,000/= kwake ni tatizo lakini lenye majibu. Mke au mume wake hawezi kulala sakafuni muhimbili wakati wa kujifungua au anapoumwa kwa sababu anaweza kulipia fast truck na akapewa kitanda. Nauli za Daladala kupanda ni tatizo lakini kwa mwana JF anao uwezo wa kukabiliana na hilo tatizo. Wale ambao haya ni matatizo kwao kwa kutokuwa na uwezo wa kukabiliana nayo HAWAJAYAONA hivyo wanataabika tu bila msaada.

Kura ya JF siyo hali halisi kule kwa wapiga kura ambao hawalioni tatizo.

Kuwafanya walione tatizo, tufanyeje????????

Respect

Siyo Rahisi Mkuu
Maana watanzania tumefundishwa mbinu nyingi za medani kuwa wavumilivu:
1. Kufunga Mikanda
2. Miezi 18 ya Hali ngumu ya uchumi
3.n.k

Tuanze kwa maombi tu....katika imani zetu mbali mbali
 
Mwamko wa JF ni mwanzo mzuri siyo kazi ndogo,imetoa changamoto kubwa kwa jamii yetu za kitanzania ,imefungua au kuonyesha njia jinsi ya kujenga hoja,kujadili,na kutetea hoja mbali mbali hasa kuhusu maswala ya uchaguzi mkuu wa October.La muhimu nikuzidi kuwaelemisha jamii elimu ya uraia na umuhimu wa kuwa na katiba mpya.Tusikate tamaa bandubandu humaliza gogo.
 
Mwamko wa JF ni mwanzo mzuri siyo kazi ndogo,imetoa changamoto kubwa kwa jamii yetu za kitanzania ,imefungua au kuonyesha njia jinsi ya kujenga hoja,kujadili,na kutetea hoja mbali mbali hasa kuhusu maswala ya uchaguzi mkuu wa October.La muhimu nikuzidi kuwaelemisha jamii elimu ya uraia na umuhimu wa kuwa na katiba mpya.Tusikate tamaa bandubandu humaliza gogo.


Nakubaliana na wewe kabisa mkuu kwamba hapa JF pameleta changamoto nyingi sana na uwezo wa kuchambua hoja umejidhihrisha.

Shida ni kuwa wasomi wengi hawapigi kura siku yenyewe, wanaopiga kura kwa wingi ni wale ambao hawalioni tatizo na matokeo yake ni ushindi usiokuwa na kwa watu amao hawataleta matumaini mapya.

Respect.
 
njia zifuatazo zaweza kuwasaidia.
  • kuandika makala za uchambuzi unaohusianisha taabu watanzania wanazopata na kuzihusianisha vyema na utawala mbivu tulio nao madarakani
  • viongozi makini wa vyama kutumia mikutano ya kampeni kuhusianisha na kufafanua kwa wananchi kwenye mikutano ya kampeni chanzo hasa cha hali ngumu ya maisha inayoletwa na utawala mbovu.
  • viongozi wa dini na taasisi binafsi kuendeleza kampeni za kupinga ufisadi, kuelimisha jinsi ya kchagua viongozi bora na wazalendo
  • kwa sisi tuliokwisha kuelewa tutitokeze na kuhamasisha wale walio karibu yetu kupiga kura ya mabadiliko ya kweli.

Mkuu Negotiator.
Magazeti kama Rai Mwema na Mwanahalisi yanafanya sana uchambuzi na naamini kwamba ni magazeti yanayosomwa sana kwa sababu ya kukubalika kwake katika jamii yetu.

Lakini ni vigumu sana kwa Gazeti au hata taasisi za kidini kuandika wazi wazi kuwa chama fulani kisichaguliwe. Ambao huwa wanatoa msimamo wao bila hofu ni Kundi fulani la waislamu jambo ambalo huwa linapingwa mara moja na bakwata (chombo rasimi cha kuwasemea waislam) Katika hali kama hiyo nahisi kuna shida kubwa sana mkuu.
 
Kwa mtazamo wangu anayetaabika tayari ameshakata tamaa, anayetaabika kafikia kujiona hana nguvu tena na anaishi kwa kudra za mwenyezi mungu day in day out! sasa kizazi cha mtaabika pia kinajikuta kinalelewa ktk malezi ya kutaabika na kinachukulia kutaabika ndio mfumo wake na kile kizazi cha wale kina fisadi nacho ndio kinaona kufisadi ndio haki yake na kitaendelea kufisadi sabau ya kukuzwa au kulelewa kifisadi, hapo siku zote kunakuwaga na matatizo. Tuna mzigo mkubwa sana wa kuwaelimisha wenzetu wataabika haswa kule vijijini ili tusafiri wote!
 
Back
Top Bottom