Wala sina hakika kama nipo sahii, lakini nahisi MAPENZI NA SIASA ni dugu ya nasaba moja!! Kote ni FULL UWONGO, UASI, USALITI, UZANDIKI NA UNAFIKI PIA!!Hata hivyo, ajabu ni kwamba, a well structured uovu huu ndio unaojenga MAPENZI NA SIASA!! Hebu fikiria, mpenzio anakuambia anakupenda kuliko kitu chochote na kwamba MOYO WAKE HAUNA NAFASI KWA MTU MWINGINE BALI NI WEWE PEKE YAKO!!!! Ataendelea kusema eti BILA WEWE NI HERI KUFA, na kwamba mkiachana kwa namna yeyote ile BASI ATAISHI BILA MPENZI MAISHA YAKE YOTE!!! Je, inawezekana jambo hilo?! Ni kweli moyo umeumbwa hivyo? Hebu chukua mfano huu: Mwanamke na mwanume wanapokutana kwa tendo la ndoa halafu Mbegu za Mwanaume zikakutana na yai la mwanamke na kutungisha mimba, basi ndani ya muda mfupi mfuko wa uzazi unafunga na hakuna mbegu nyingine ya kiume itakayoingia tena!! Je, moyo nao upo hivi? Kwamba pendo la fulani likishaingia moyoni mwako basi moyo hufunga na kutoruhusu upendo/penzi kwa mwingine?! Na kama moyo upo hivyo, mbona unampenda baba yako na mama yako na kinachotofautina ni kiasi tu cha upendo!!! Sasa kwanini kwenye mapenzi tudanganyane kwamba upo peke yako?
Kwa kifupi, labda niseme kwa mtizamo wangu, kauli sawa na hiyo ni unafiki na uwongo katika mapenzi. Hata kama mpenzi wako unampenda vipi, ni matumaini yangu ipo room kwa ajili ya mwingine somewhere else. Unakuta mtu anamtumia msg za mapenzi mpenzi wake huku akijifanya ni mtu mwingine kwa ajili ya kumtega ajue kama kweli anampenda!!! Hii ni kuchanganya MAPENZI NA UAMINIFU!!! Hivi ni vitu viwili tofauti. KAMA UNAAMINI KWAMBA AKUPENDAE KWA DHATI HAWEZI KUKUSALITI, basi wewe kalagha bao!! Anaweza kukupenda kwa moyo wote, lakini bado moyo wake unaacha room ya kupenda mwingine zaidi hata kama si kwa kiwango akupendacho wewe!!! Na kweli inapatikana hii room, ndipo usaliti unapotokea!! Ninachosema ni kwamba, mpenzio asikudanganye kwamba atakupenda wewe peke yako maisha yote hata baada ya kufa!!!! Akikuambia hivyo, mtemee mate usoni!! Mpenzi huyo ni mwongo sawa na mwanasiasa anayeahidi kujenga mabomba yatakayotoa maziwa bongo!! Mpenzi mkweli ni yule atakayekuambia kwamba bado moyo wake una nafasi ya kupenda mwingine na wengine zaidi lakini atahakikisha HAKUSALITI! MOYO, NI FREE ENTRY FREE EXIT ZONE!!!
NAJENGA HOJA!!
Kwa kifupi, labda niseme kwa mtizamo wangu, kauli sawa na hiyo ni unafiki na uwongo katika mapenzi. Hata kama mpenzi wako unampenda vipi, ni matumaini yangu ipo room kwa ajili ya mwingine somewhere else. Unakuta mtu anamtumia msg za mapenzi mpenzi wake huku akijifanya ni mtu mwingine kwa ajili ya kumtega ajue kama kweli anampenda!!! Hii ni kuchanganya MAPENZI NA UAMINIFU!!! Hivi ni vitu viwili tofauti. KAMA UNAAMINI KWAMBA AKUPENDAE KWA DHATI HAWEZI KUKUSALITI, basi wewe kalagha bao!! Anaweza kukupenda kwa moyo wote, lakini bado moyo wake unaacha room ya kupenda mwingine zaidi hata kama si kwa kiwango akupendacho wewe!!! Na kweli inapatikana hii room, ndipo usaliti unapotokea!! Ninachosema ni kwamba, mpenzio asikudanganye kwamba atakupenda wewe peke yako maisha yote hata baada ya kufa!!!! Akikuambia hivyo, mtemee mate usoni!! Mpenzi huyo ni mwongo sawa na mwanasiasa anayeahidi kujenga mabomba yatakayotoa maziwa bongo!! Mpenzi mkweli ni yule atakayekuambia kwamba bado moyo wake una nafasi ya kupenda mwingine na wengine zaidi lakini atahakikisha HAKUSALITI! MOYO, NI FREE ENTRY FREE EXIT ZONE!!!
NAJENGA HOJA!!