apprentice1997
Senior Member
- Jun 8, 2016
- 107
- 99
Wakubwa zangu shikamoni,
Niliamua kutulia na msichana mmoja tu nikaamua nitulie nae huyo, kiukweli nampenda sana mpaka nimeamua kuwa mwaminifu kwake. Jana alinielekeza kuwa nimekuwa muwazi sana kwake na yeye ameamua kuniambia ukweli kuwa amekuwa na mahusiano na vijana wengine 3 jumla tupo wa 4. Lakini yeye bado ni bikra na hajawahi kulala na mtu yeyote.
Yeye ni mtu wa dini sana na amekuwa akihudhuria semina wiki hili na akaamua kunieleza ukweli wote na pia anasema anataka kuachana na sisi wote na atulie. Mimi nimetafakari sana Jana hiyo nikaenda kanisani muhubiri akasema ili ufanikiwe ni lazima ujitoe mahali unapodhani ni comfort zone yako nikaguswa nikajua kuwa natakiwa kuachana na mapenzi nae na nisiwe na mwanamke yoyote. Umri wangu ni miaka 19, nimefaulu na mwezi huu naanza kwenda college na yeye bado yupo shule.
Baada ya kutoka church akili yangu ilitulia na kuniambia kuwa ninataka kuwa na amani nae ninatakiwa niachane nae na nikaridhia baada ya mimi na yeye kuonana nikakumbuka mambo mengi sana tuliyopanga pamoja na ninampenda kwa kuwa anajiheshimu na ana hofu ya Mungu. Moyo unaniuma toka hapo ninafikiria mipango yangu na malengo niliyokuwa nae ninaumia sana natamani hata nisingejiingiza kwenye mapenzi.
Ninatamani nifuate sauti ya Mungu ila ninatambua maamuzi ya Mungu ni magumu na ndio haya yanayonikumba sasa. Leo ninataka nionane nae sitapenda aondoke tukiwa hatujaelewana hili jambo litatuathiri sana na hatutaweza kuendelea na masomo na kiukweli tunapendana sana.
Nikifikiria sina cha kumwambia ninatamani niseme neno moja tu na roho yangu ipone haya maumivu ninatamani kumlaumu ninaishia kumsamehe kwa kuwa nampenda sana na pia ninatamani kuachana nae ila hofu yangu ni kuwa nitaumia sana siku za mbeleni.
Na sina mpango wa kuwa mzinzi ninatamani Mungu anibariki anipe mwanamke ambaye atakuwa wangu mimi peke yangu na asinisumbue. Inafika muda najilaumu sana kwanini nilianza mapenzi maana naumia sana. Wapendwa naombeni ushauri wenu nimwambie nini ili tuweze kuelewana na moyo wangu utulie. Na pia nifanye maamuzi yapi kuhusu sauti inayonena ndani yangu.
Niliamua kutulia na msichana mmoja tu nikaamua nitulie nae huyo, kiukweli nampenda sana mpaka nimeamua kuwa mwaminifu kwake. Jana alinielekeza kuwa nimekuwa muwazi sana kwake na yeye ameamua kuniambia ukweli kuwa amekuwa na mahusiano na vijana wengine 3 jumla tupo wa 4. Lakini yeye bado ni bikra na hajawahi kulala na mtu yeyote.
Yeye ni mtu wa dini sana na amekuwa akihudhuria semina wiki hili na akaamua kunieleza ukweli wote na pia anasema anataka kuachana na sisi wote na atulie. Mimi nimetafakari sana Jana hiyo nikaenda kanisani muhubiri akasema ili ufanikiwe ni lazima ujitoe mahali unapodhani ni comfort zone yako nikaguswa nikajua kuwa natakiwa kuachana na mapenzi nae na nisiwe na mwanamke yoyote. Umri wangu ni miaka 19, nimefaulu na mwezi huu naanza kwenda college na yeye bado yupo shule.
Baada ya kutoka church akili yangu ilitulia na kuniambia kuwa ninataka kuwa na amani nae ninatakiwa niachane nae na nikaridhia baada ya mimi na yeye kuonana nikakumbuka mambo mengi sana tuliyopanga pamoja na ninampenda kwa kuwa anajiheshimu na ana hofu ya Mungu. Moyo unaniuma toka hapo ninafikiria mipango yangu na malengo niliyokuwa nae ninaumia sana natamani hata nisingejiingiza kwenye mapenzi.
Ninatamani nifuate sauti ya Mungu ila ninatambua maamuzi ya Mungu ni magumu na ndio haya yanayonikumba sasa. Leo ninataka nionane nae sitapenda aondoke tukiwa hatujaelewana hili jambo litatuathiri sana na hatutaweza kuendelea na masomo na kiukweli tunapendana sana.
Nikifikiria sina cha kumwambia ninatamani niseme neno moja tu na roho yangu ipone haya maumivu ninatamani kumlaumu ninaishia kumsamehe kwa kuwa nampenda sana na pia ninatamani kuachana nae ila hofu yangu ni kuwa nitaumia sana siku za mbeleni.
Na sina mpango wa kuwa mzinzi ninatamani Mungu anibariki anipe mwanamke ambaye atakuwa wangu mimi peke yangu na asinisumbue. Inafika muda najilaumu sana kwanini nilianza mapenzi maana naumia sana. Wapendwa naombeni ushauri wenu nimwambie nini ili tuweze kuelewana na moyo wangu utulie. Na pia nifanye maamuzi yapi kuhusu sauti inayonena ndani yangu.