Sabry001
JF-Expert Member
- Jun 28, 2011
- 1,064
- 353
Am in a very very bad situation! Niliyempenda anapendwa na wengi. Kwa moyo wangu wote nilimdondokea, nikampa kwa kadri ya uwezo wangu, leo penzi limenitoa chozi. Nilidhani twashabihiana kwa tabia na mambo tuliopitia ktk maisha, nikajua atanipa pumziko nae alipate kwangu, ila yamegeuka kuwa machungu, penzi limeniumiza sitamani kupenda tena. Nilimuona wa maana mbele ya uso wangu, cheo na hadh vikanipumbaza, nikifikiri vitamfanya awe na adabu kumbe kalumekenge tu. Niliwekeza sana ktk penz hlo, nikajua litadumu, juhud zangu bure, leo limepeperuka. Ashukuriwe aliyeyaumba mapenzi kwani likiwa shwari ulimwengu hutulia ila ikiwapo shari dunia hulia. Natamani wa ukweli ajitokeze, anifute yangu machozi, anipe pendo lake nami nitampa lile la milele.