Moyo uliao machozi....!

Sabry001

JF-Expert Member
Jun 28, 2011
1,064
353
Am in a very very bad situation! Niliyempenda anapendwa na wengi. Kwa moyo wangu wote nilimdondokea, nikampa kwa kadri ya uwezo wangu, leo penzi limenitoa chozi. Nilidhani twashabihiana kwa tabia na mambo tuliopitia ktk maisha, nikajua atanipa pumziko nae alipate kwangu, ila yamegeuka kuwa machungu, penzi limeniumiza sitamani kupenda tena. Nilimuona wa maana mbele ya uso wangu, cheo na hadh vikanipumbaza, nikifikiri vitamfanya awe na adabu kumbe kalumekenge tu. Niliwekeza sana ktk penz hlo, nikajua litadumu, juhud zangu bure, leo limepeperuka. Ashukuriwe aliyeyaumba mapenzi kwani likiwa shwari ulimwengu hutulia ila ikiwapo shari dunia hulia. Natamani wa ukweli ajitokeze, anifute yangu machozi, anipe pendo lake nami nitampa lile la milele.
 
Mm naona uvute subra kidogo maana wengi siku hiziwanapenda kuwachezea/ kukumega kisela na kukuacha,jipe muda wa ukweli utamjua tuu hana alama ila vitendo vyake anaweza akalamba asali alafu akachonga mzinga
 
Pole sana best!
Kilugha changu huwa tunasema "Uyenyaje tee apubumile ulwayo"...Patazame sana ulipojikwaa kidole, utajifunza kitu!
Naamini sasa utatumia jicho la ziada kila unaposhawishika kuingia penzini!
Ni hilo tu!
 
Vp hujasema ilikuwaje akapeperuka au ulikuwa unambania baadhi ya vituz, ila umetangaza nafasi ngoja tutume apilication
 
Pole sana best!
Kilugha changu huwa tunasema "Uyenyaje tee apubumile ulwayo"...Patazame sana ulipojikwaa kidole, utajifunza kitu!
Naamini sasa utatumia jicho la ziada kila unaposhawishika kuingia penzini!
Ni hilo tu!
Yaani PJ kweli wantukana hivi hivi jamani!.:caked:
 
Pole sana best!Kilugha changu huwa tunasema "Uyenyaje tee apubumile ulwayo"...Patazame sana ulipojikwaa kidole, utajifunza kitu!Naamini sasa utatumia jicho la ziada kila unaposhawishika kuingia penzini!Ni hilo tu!
asante Jimy
 
Pole sana jipe moyo ,muombe mungu kwa imani atakupatia mwenza wako yaani wa ubavu wako kabisa sisi ni binadamu na ni majaribu mengi tunayokutana nayo hasa ktk mahusiano.unanikumbusha 1month now nilipata issue kama hiyo lkn kwa maombi na ushauri wa hapa jamvini nilijiona nipo na wenzangu kimawazo so jipe moyo utayashinda hayo yote jaribu kusahau yote ya nyuma pole sana
 
Vp hujasema ilikuwaje akapeperuka au ulikuwa unambania baadhi ya vituz, ila umetangaza nafasi ngoja tutume apilication
cjui ilivyotokea, nilishangaa mie sio favorate girl wake tena. Uki2ma maombi ctayapokea, ntaichanachana barua hyo
 
cjui ilivyotokea, nilishangaa mie sio favorate girl wake tena. Uki2ma maombi ctayapokea, ntaichanachana barua hyo
duh, kumbe hutak kuziba pengo! Tatizo warembo cku hzi mmekuwa wengi kupita kawaida inabidi tuonje wote, kwani nao wanahak ya kupata hyo huduma
 
Piga moyo konde dada yangu, muombe sana Mungu atakupa nguvu za kumsahau na kusahau maumivu aliyokusababishia. Huwezi jua pengine kuna kitu umeepushwa, hivyo usilalamike sana. Isitoshe ni hali ya kawaida sana ktk relationship, si wewe wa kwanza kuachwa. Mi mwenyewe niliachwa na mchumba wangu ikaniuma sana. Lakini kumbe Mungu alikuwa ananiepusha na janga kwani mchumba yule alikuja kufa kwa ukimwi baada ya miaka 3. Nilikaa mwaka na nusu (nikitafakari na kuji-assess) ndo nikaingia kwenye relationship ambayo hadi leo tunaishi kwa raha mustarehe - miaka 8 sasa. Kwahiyo jitahidi ku-take it easy. Ila usifanye papara kuingia kwenye relationship nyingine. Tumia huu muda kujipanga na kujiuliza/kufanya utafiti ni kwanini huyo jamaa ameamua kukumwaga. Hii itakusaidia kuepuka kuachwa kwa sababu hizo hizo in future. Zaidi acha kabisa tabia ya kumpenda mtu eti kwavile ana cheo/kazi nzuri, elimu, pesa, and any kind of material things. Tena epuka kabisa mwanaume anayeku-approach kwa kuonyesha hivi vitu. Kigezo chako cha kwanza na cha mwisho iwe ni kwamba umempenda tu (jinsi alivyo) kwa dhati. Pia achana na vigezo ambavyo ni rare ktk jamii kama vile mrefu, handsome n.k. Hivi vigezo vinawaponza sana akina dada, sema tu wengi wenu hamjui!
 
Piga moyo konde dada yangu, muombe sana Mungu atakupa nguvu za kumsahau na kusahau maumivu aliyokusababishia. Huwezi jua pengine kuna kitu umeepushwa, hivyo usilalamike sana. Isitoshe ni hali ya kawaida sana ktk relationship, si wewe wa kwanza kuachwa. Mi mwenyewe niliachwa na mchumba wangu ikaniuma sana. Lakini kumbe Mungu alikuwa ananiepusha na janga kwani mchumba yule alikuja kufa kwa ukimwi baada ya miaka 3. Nilikaa mwaka na nusu (nikitafakari na kuji-assess) ndo nikaingia kwenye relationship ambayo hadi leo tunaishi kwa raha mustarehe - miaka 8 sasa. Kwahiyo jitahidi ku-take it easy. Ila usifanye papara kuingia kwenye relationship nyingine. Tumia huu muda kujipanga na kujiuliza/kufanya utafiti ni kwanini huyo jamaa ameamua kukumwaga. Hii itakusaidia kuepuka kuachwa kwa sababu hizo hizo in future. Zaidi acha kabisa tabia ya kumpenda mtu eti kwavile ana cheo/kazi nzuri, elimu, pesa, and any kind of material things. Tena epuka kabisa mwanaume anayeku-approach kwa kuonyesha hivi vitu. Kigezo chako cha kwanza na cha mwisho iwe ni kwamba umempenda tu (jinsi alivyo) kwa dhati. Pia achana na vigezo ambavyo ni rare ktk jamii kama vile mrefu, handsome n.k. Hivi vigezo vinawaponza sana akina dada, sema tu wengi wenu hamjui!
sikumpendea cheo wala pato mito, ila nilidhani kwa nafasi yake alipo angekuwa na adabu, kumbe cheo kilimpa accesibility to more women!
 
sikumpendea cheo wala pato mito, ila nilidhani kwa nafasi yake alipo angekuwa na adabu, kumbe cheo kilimpa accesibility to more women!

Nadhani hicho ulichosema ndio chanzo cha tatizo. Wanaume wengi wakiwa katika nafasi fulani nzuri either kicheo/nafasi au kipato wanawake au wasichana wengi huvutiwa naye kwa sababu mbalimbali lkn kubwa ni kutaka kumchuna huyo kidume kutokana na nafasi aliyo nayo.Huo ndio ukweli ulivyo hasa kwa maisha ya sasa yalivyo.

USHAURI:

Inawezekana kabisa huyo mpz wako atakuwa amekutana na matapeli wa kimapenzi wa staili hiyo hapo juu, hivyo nakushauri jaribu kuwa mvumilivu ktk hiki kipindi kigumu, then kama unaweza kukutana naye muombe siku moja mkae sehemu tulivu then ongea naye kwa upole na umakini mkubwa ili akuambie nini tatizo hadi amefikia kukutesa moyo wako hivyo hali akijua wazi kuwa unampenda kwa dhati na yeye ndio uliyemkabidhi moyo wako wote.

Ukiona haelekei au anakuletea ujeuri fulani basi wewe chapa lapa tu mpendwa wala usijali mungu yupo nawe daima. Ila humu JF kuwa makini kuna mafataki balaaa usione watu wapo kimyaa au wanatoa comments kimtindo, yaani ukilegeza kidogo tayari wanabeep au kupiga kabisaaaa ukija kustuka utakuta umejaza Dar expresss au Yutong!
 
Nadhani hicho ulichosema ndio chanzo cha tatizo. Wanaume wengi wakiwa katika nafasi fulani nzuri either kicheo/nafasi au kipato wanawake au wasichana wengi huvutiwa naye kwa sababu mbalimbali lkn kubwa ni kutaka kumchuna huyo kidume kutokana na nafasi aliyo nayo.Huo ndio ukweli ulivyo hasa kwa maisha ya sasa yalivyo.USHAURI:Inawezekana kabisa huyo mpz wako atakuwa amekutana na matapeli wa kimapenzi wa staili hiyo hapo juu, hivyo nakushauri jaribu kuwa mvumilivu ktk hiki kipindi kigumu, then kama unaweza kukutana naye muombe siku moja mkae sehemu tulivu then ongea naye kwa upole na umakini mkubwa ili akuambie nini tatizo hadi amefikia kukutesa moyo wako hivyo hali akijua wazi kuwa unampenda kwa dhati na yeye ndio uliyemkabidhi moyo wako wote.Ukiona haelekei au anakuletea ujeuri fulani basi wewe chapa lapa tu mpendwa wala usijali mungu yupo nawe daima. Ila humu JF kuwa makini kuna mafataki balaaa usione watu wapo kimyaa au wanatoa comments kimtindo, yaani ukilegeza kidogo tayari wanabeep au kupiga kabisaaaa ukija kustuka utakuta umejaza Dar expresss au Yutong!
thanx kwa ushauri. Ila nimeshakaa nae kitako akanijibu vibaya, akaniambia mie mshamba, cpend kujirusha navaa kizee hajickii poa kutoka na mwanamke ametinga nguo za kushona. Anataka nivae tofauti na nilivyo, nguo za kuonesha sehem za mwili nami cwezi. Nimembembeleza aelewe hlo ktk mavazi lakini wapi! Nimebaki kuumia kwani siwez kuanika mwili wangu kisa namfuraisha yeye kwa kweli.
 
mi nimewahi kusikia mwanamke ananiambia yupo tayari kutembea nusu uchi as long as mumewe anafurahia. Na hii ni ukweli na nimeshuhudia. Ni ajabu sana kuona mwanaume anatangaza maumbile ya mkewe barabarani, na siku zote ukiona mkeo yupo tayari kuvaa nusu uchi ujue ni kicheche tu.
 
falling down does not mean being buried mamii. ups and downs ni sehemu ya maisha. just give yourself some time to heal and adjust. life must continue and good should prevail
 
Back
Top Bottom