Mkataba (MoU) kati ya Serikali na Kanisa Katoliki na Taasisi nyingine za Kidini

serikali iepuke negotiations za namna hii zinatia wasiwasi. Kwa nini iwe kanisa peke yake? Memorandum ya namna hii ihusishe dini na madhehebu mengine. Serikali inaongoza wananchi siyo kanisa. Mou ya serikali ni kwa manufaa ya nchi siyo kanisa. Serikali yetu haina dini ila watu wake wana dini, wakipewa madaraka ya serikali wasi assume dogma za dini zao.kufanya hivyo ni kukaribisha mkanganyiko wa kisiasa, kiitikadi, kifalsafa na kiutawala.wenye nchi mpo!

nianze na wewe.

Nilichokielewa ni kuwa serikali haikuwa na uwezo wa kuhudumia watu wake kikamilifu. Hivyo kwa kuwa mashirika ya kidini yalikuwa na miundombinu ya kutosha, ndo wakaomba kusaidiana na mashirika ya dini ili kuhakikisha kila mtu ndani ya nchi anapata huduma zile mhimu elimu na afya bila kujali dini yake.

Kuhusiana na hiyo bilateral agreement, ni kweli serikali lazima iwatambue nchi wahsani. Kwa mfano, kuna hospital zilizojengwa na kuendeshwa na nchi wahsan kupitia makanisa yao. Sasa ili makubaliano yawe mazuri, yule mhisani kuwepo si tatizo.

Kuhusu wahindi, the aga khan ni mfano, sijui kama waliingia mkataba, lakini kama sio mkataba sidhani kama leo mie mwenye bima ya serikali ningeweza kwenda kutibiwa mahali pale. Ni mikataba hiyo inayoniwezesha mie kutibiwa hospital yoyote, bila kujali dini yangu.

Kinachowakumba ndugu zangu waisalm, hawana taasisi kubwa zinazotoa huduma hadi kuishawishi serikali kuingia nao mkataba. Kama ipo waiseme, hiyo shule au hospital ambayo ni tegemeo la watanzania wengine. Maana wenyewe hata wakijenga mfano shule watajenga mazngira ya waislam tu ndo wafike kupata huduma zao. Udini sana
 
Sasa bwanyenye wetu, hembu tuambie sababau ya msingi ya serikali kupania kujitenga na kanisa zaidi ya kukimbizana na vitu ambavyo hakuna pa kupanga wala kukopa?Is it kwa vile waislam hawataki hilo?

Kwa taarifa yako serikali huokoa hela sana kama wanaweza punguza vitu vinavyohitaji mainteanance kwa kiais kiwezekanavyo.Hata makampuni yaliyo na ufanisi hayamiliki magari ya usafirishaji kwani hasara ya kuyatengeza na ongezeko la mianya ya wizi huwa ni mikubwa sana kampuni inapojihushisha.Serikali kumiliki hospital ni kufungua mianya ya ufisadi ktk matengenezo, na mambo mengine.

Seriklai ingeweza toa tender kwa taasisi na watu binafsi wengi tuu wajenge majengo ya shule na hospital halafu serikali ipange.sasa hivi hata mabank hayana majengo ya kudumu.Makampuni mengi tuu hukodisha magari huku wakiwa na mkataba wenye vipengele vinavyombana mmiliki wa magari kuhakikisha kuwa saa yoyote kuna magari kwa shughuli huku yakiwa katk hali nzuri.


sijui kama Barubaru atakuelewa......
ila mimi ninachojua Nicholas kichaa akibeba nguo zako ukabaki uchi usimkimbize maana wewe ndio utaoneka kichaa zadi
ndio maana makanisa yamechomwaaaaa lakini hakuna anayegusa misikiti - wenye busara huwa hawapigani wala kuharibu mali za wenzao
 
Mkataba huwa ni mzuri kabla haujavunjwa,ukivunjwa tu ndio utasikia kwamba kipengere namba kadhaa kimevunjwa.
 
Naona pumba tupu pamoja na ushauri wako kwamba nisome kwa makini.Unauliza tunda limetoka wapi wakati mti waujua.Kalale uamke na mawazo mengine
 
Serikali iepuke Negotiations za namna hii zinatia wasiwasi. Kwa nini iwe Kanisa peke yake? Memorandum ya namna hii ihusishe Dini na madhehebu mengine. Serikali inaongoza wananchi siyo Kanisa. MoU ya Serikali ni kwa manufaa ya nchi siyo Kanisa. Serikali yetu haina Dini ila watu wake wana Dini, wakipewa madaraka ya serikali wasi assume dogma za Dini zao.Kufanya hivyo ni kukaribisha mkanganyiko wa kisiasa, kiitikadi, kifalsafa na kiutawala.Wenye nchi mpo!

Shida iko wapi kwa wasio na interest na huduma za jamii au wenye interest na huduma za jamii? Kwani Waislamu waliomba hiyo MoU wakanyimwa au wao approach yao ya kutumikia jamii ni tofauti na ndio maana hawashughuliki?
 
Shida iko wapi kwa wasio na interest na huduma za jamii au wenye interest na huduma za jamii? Kwani Waislamu waliomba hiyo MoU wakanyimwa au wao approach yao ya kutumikia jamii ni tofauti na ndio maana hawashughuliki?

Tatizo la hawa Jamaaa Helena wao ni Mfinyu sana na mambo yenyewe yapo wazi na wanajifanya kutoona wakati wanaona kila kitu,kwanza wazembe kazi hawafanyi join kahawa tende na mengine sasa leo unakuja kilalamika pasipo sababu za msingi unadhan utaeleweka?makanisa chomeni lakin dawa yenu ipo mbinguni na ntakuja kulitambua hili bandage sana pale mtakapo funguka na kujua kwamba Kanisa lipo juju yenu.
Haki yako hailazimishwi Kama mnanyanyasika someni kwa bidii midanganye watoto wenu kwa kitu Kimoja cha elimu dunia wakati kuna vitu vya msingi vinahitaji upeo na elimu kusudi uweze kujadili Hoja mbele
 
cover.jpg


quote_icon.png
By Dr.W.Slaa


Wana JF,

Nashukuru mwana JF aliyeweka hadharani MOU husika
. Ningependa tu kuongezea machache na hasa historia ya jinsi na kwanini MOU hiyo ilizaliwa:-

1)
Wote mtakumbuka kuwa huko nyuma Serikali ilitaifisha Shule na nyingi za madhehebu ya Dini. Utaifishaji huo uliendana pia na Ardhi, hasa ikizingatiwa kuwa wakati shule zinajengwa zilijengwa kwenye maeneo ya madhehebu ya dini na papo hapo kukukiwa na kanisa, nyumba za mapadre na kadhalika. Hii ilikuwa hivyo kwa shule nyingi za Middle School (Model Schools, Upper Primary kama mnavyojua majina yalibadilika sana kati ya 1962 hadi 1965 hivi na ndipo pia mtihani au darasa la nane lilipofutwa rasmi).

2)
Kwenye miaka ya 1980 madhehebu yakataka warudishiwe ardhi yao, hasa ardhi ambayo ina majengo mengine yasiyohusiana na shule hizo. Mchakato wa mjadala ulishika kasi, mwaka 1986 Baraza la Maaskofu Katoliki TEC, lilipopitisha azimio rasmi,na kumtaka Katibu Mkuu, awasiliane na Serikali, kuanzisha mchakato wa kufanya survey na kutenga ardhi ya shule rasmi kutoka kwenye ardhi inayotumika kwa huduma nyinginezo za madhehebu ya dini. Wakati huo mimi Dr. Slaa, ndiye nilikuwa Katibu Mkuu wa TEC baada ya kupokea rasmi kazi hiyo December, 1985. Wakati huo madhehebu yaliisha kudai yarudishiwe Shule zao kwa kuwa zimegeuka kuwa aibu kwa kukosa ukarabati, na ziko kwenye hali mbaya sana. Serikali ilikuwa imekataa ombi hilo kwa lengo la kuwa Shule hizo zinawahudumia watanzania wote bila ubaguzi, jambo ambalo ndilo lilikuwa lengo kuu la utaifishaji, na sababu ya utaifishaji ilikuwa bado inaendelelea.

3) Wakati mawasiliano yalipoanza na Serikali wakati huo kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu na Wizara ya Elimu, Serikali iliomba TEC na madhehebu ya Dini kwa ujumla, kama yanaweza kusaidia ukarabati wa shule hizo kwa kuwa ziko kwenye hali mbaya na hali ya uchumi wa nchi haikuwa nzuri na hivyo mapato ya Serikali.

4) Wakati mchakato huo kwa upande wa Elimu umeanza kulikuwa pia na mgogoro kati ya Serikali na TEC baada ya Serikali kuichukua Hospitali ya Bugando almost kwa utaratibu huo huo wa kuitaifisha. Hospitali hiyo ilikuwa kwenye awamu ya Pili ya ujenzi kwa msaada mkubwa wa Shirika la Misereor( Shirika la Maendeleo la Baraza la Maaskofu Katoliki la Ujerumani) toka Ujerumani.

5) Katibu Mkuu wa TEC alipowasiliana na Wahisani walikataa kata kata kujihusisha tena na ujenzi au ukarabati wa Shule au Hospitali ( Hospitali, vituo vya Afya na zahanati) kwa kuhofia kuwa Serikali ya Tanzania imekuwa ikitaifisha huduma hizo bila majadiliano ya aina yeyte, na hawawezi kuwekeza fedha za walipa kodi wao ( ujerumani Madhehebu ya dini yanapata fedha rasmi kutoka kodi ya wananchi) kwa ratio waliyokubaliana kuendana na idadi ya madhehebu ya dini. Lakini walikuwa tayari kuendelea na huduma mbalimbali za kusaidia madawa na elimu kwa shule zilizoko bado chini ya madhehebu kwa kuwa hawawezi kuwaadhibu wananchi na watoto.

6) Kwa kuwa shughuli zote za Bugando zilikuwa zinaelekea kusimama na kulikuwa na mgomo kila siku, kwa madaktari na manesi na watumishi, Serikali ikaomba tujadiliane upya juu ya mambo makubwa mawili :
a) Utoaji huduma katika sekta za huduma za Jamii,
b) Kuwa na chombo cha mawasiliano na majadiliano kati ya Ikulu na madhehebu ya dini, na kwa kuwa madhehebu ni mengi wakaomba chombo hicho kiundwe na viongozi wakuu wa madhehebu yaliyokuwa yanajulikana kwa mujibu wa Sheria.

Hivyo Bakwata ( Waislamu- sitaki kuingia kwenye mjadala wa kama Bakwata ni chombo kinachowasilisha waislamu au la), Tanzania Episcopal Conference TEC na CCT ( kwa madhehebu zaidi ya 60 yaliyoko chini ya Christian Council of Tanzania) . Baada ya Mashauriano tuliunda chombo hicho kikiwakilishwa na Mwenyekiti na Katibu wa vyomb o nilivyovitaja hapo juu. Uratibu ulikuwa unabadilika kila mwaka katika ya madhehebu hayo, vivyo hivyo kwa Sekretariat. Kutokana na utaratibu huo tuliweza kupatia ufumbuzi matatizo yaliyokuwa yakijitokeza mara kwa mara na ikawa rahisi kwa Serikali kuwasiliana na chombo hicho badala ya kila dhehebu peke yake, na kwa upande wetu pia chombo hicho kikatupa nguvu ya kujadiliana na serikali (power of negotiation).

7) Kutokana na hali mbaya ya Shule Serikali, ikaomba madhehebu ya dini kusaidia ukarabati wa shule zilizoonekana zitafungwa kutokana na hali mbaya , nasi kwa upande wetu kwa nia njema ya kuisaidia Serikali lakini pia kuwahudumia watanzania tuliwasiliana na Wahisani ambao walikazia msimamo wao kuwa hawako tayari kuingia kwenye shughuli za ujenzi wala ukarabati kwa kukosa msimamo wa wazi na au wa kisheria wa Serikali ya Tanzania kuhusiana na utaifishaji wa huduma hizo. Serikali ilipojulishwa, ilichukua hatua ya kuanzisha mchakato mzima wa kupata suluhu ya jambo hilo. Ndipo akapewa jukumu hilo, Mhe. Anne Makinda wakati huo, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, na mkutano wa kwanza ulifanyika Kurasini Conference Centre (TEC) Mikutano ya baadaye ilikuwa ina alternate kati ya TEC na CCT. Hii ni kwa sababu huduma zilizokuwa zinajadiliwa ni za TEC na CCT ( ambao walikuwa wameathirika na utaifishaji huo). Hatimaye, Serikali ilikubali kuwa haitataifisha tena, na kwa kuthibitisha hivyo, ikawa tayari kuwekeana MOU na madhehebu ya Dini.
Ndipo tukaanzisha mchakato wa majadiliano na Wahisani, na wahisani, nao katika umoja wao kati ya dhehebu la kikatoliki Ujerumani na Kilutheri pia la Ujerumani tukaanzisha mchakato wa namna bora ya kutoa huduama za jamii. Daima Serikali ilishirikishwa kama Observer katika michakato hiyo, na kwa upande wa Ujerumani Serikali yao nayo ilishirikishwa katika timu za majadiliano. Hatimaye, makubaliano yalifikiwa, na ndipo ikazaliwa chombo kipya Christian Social Services Commission (CSSC), chenye Secretariat yake ( Katibu Mtendaji wa kwanza akawa Dr. F.Kigadye aliyekuwa Mkurugenzi wa Bugando).

Huduma za kilichokuwa Christian Medical Board (ya TEC na CCT ikavunjwa na kuwekwa chini ya CSSC) na idara za Elimu zilizokuwa chini ya TEC na CCT huduma zake zikaunganishwa na kuwekwa chini ya CSSC. Ndiyo MOU iliyosainiwa na Askofu Stanford Shauri wa Diocese ya Ruvuma, Mwenyekiti/Katibu Mkuu wa CCT wakati huo, na Askofu Josephat Lebulu, wakati huo Askofu wa Jimbo Katoliki la Same, na Mwenyekiti wa TEC. Kwa upande wa Serikali kama sikosei aliweka saini Mhe. Edward Lowassa, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (au Waziri sikumbuki).

8) TEC na CCT nazo zikawekeana na Wahisani Mkataba MOU yao ya ndani ili kupata misaada ya ujenzi, ukarabati na uendelezaji wa huduma zote za jamii . Huduma hizo zinaendelea hata sasa japo sasa kwa kiwango kidogo baada ya mkataba wa awali kwisha.

Narudia tena, namshukuru sana aliyeweka kwenye JF MOU hiyo.
Ninarudia kuwaomba wenzangu, tumetumia muda mrefu sana kujadiliana kwa hisia ya aina mbalimbali. Watanzania hatukuzoea huko nyuma kuulizana dini zetu, wala kabila wala ukanda. Haya mambo tukiyaendekeza Taifa letu litakuwa hatarini. Tukumbuke kubomoa ni kazi nyepesi sana, sekunde lakini kujenga tena inachukua muda mrefu na ni kaz ngumu, na wakati mwingine hata ukifanikiwa huwezi kujenga kama ilivyokuwa. Nashauri ili JF ibaki na heshima yake ya Home of Great Thinkers tupende kufanya Research zaidi kabla ya kulaumiana au kuhisiana, kama mtu hana taarifa za kina awaombe wenye taarifa. Kama mnavyoona mimi nilikuwa nafahamu historia yote, nafahamu MOU, lakini sikuwa nayo. Mtu huwezi kujua kila kitu na au kuwa na kila kitu, we need to complement each other. Tunaweza tukidhamiria, na JF itabaki na hadhi na heshima yake daima.
___________________________________________________

MAJIBU KWA DR SLAAA:


Issue hapa inatokana na Dhana ya Serikali kutokuwa na Dini au Serikali ya Kisekula Dhana hiyo ni maarufu Tanzania. Mara nyingi katika masuala yahusuyo dini, viongozi wa serikali husikika wakisema «serikali haina dini, ila wananchi wake wana dini zao ». Hoja ya usekula wa serikali ni ya kihistoria. Ilijengwa kiasi cha miaka miambili iliyopita ikitaka serikali ijiepushe na shughuli za kidini hususan katika masuala ya elimu, mafundisho ya maadili na na ibada.Japokuwa Tanzania imekuwa ikidai kwamba serikali yake ni ya kisekula, hali halisi haioneshi hivyo. Pamoja na madai hayo, serikali ya Tanzania imewahi kuingia katika msuguano na Waislamu na baadhi ya wasiokuwa waislamu pale Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ilipotaka kuanzisha somo la dini au maadili ya nchi. Kadhia hii ni maarufu kwa jina la "dini mseto". serikali ya kisekula haiwezi ikaja na mipango ya kusomesha dini kwa jina lolote lile liwe la maadili au vyovyote vile.

Mifano mingine inayotia wasiwasi usekula wa serikali ya Tanzania ni hii ifuatayo:

1. Wimbo wa Taifa – unaomba mungu aibariki nchi

2. Dua ya Bungeni – ina muomba mungu

3. Kuapishwa kwa wanaochukua nafasi za uongozi.
Japo wanaoapa huapa kwa dini zao, aneapishasi kiongozi wa dini husika bali wa serikali au wabunge.

Utaratibu huo hauendani na madai kuwa nchi au serikali ya Tanzania haina dini, bali wananchi wake ndiyo wenye dini. Swali ni je, tunapomtaja Mungu katika wimbo wa taifa au katika dua ya bungeni, na kadhalika, tunamkusudia mungu yupi? Mungu wa Waislamu? Wa Wakristo? Wa dini za asili? Je, kuna mungu wa kitaifa? Mungu huyo wa kitaifa ni yupi na ni wa dini gani?Je, katika hali hiyo, ni kweli serikali haina dini? Katika mazingira ya Waislamu kuandamwa na kukandamizwa na mila ya Mfumokristo, mfumo ambao unajidhihirisha zaidi katika vitendo vya kibaguzi vinavyofanyiwa Waislamu na sehemu kubwa ya watendaji serikalini na katika taasisi mbalimbali, kwa nini mwananchi Muislamu asiamini kuwa serikali hii si ya kisekula bali ni ya kidini; na dini yenyewe ni Mfumokristo.

Kufuatia makubaliano hayo katika ya serikali na makanisa mabilioni ya fedha za walipa kodi yamekuwa yakitolewa kila mwaka kwa taasisi mbalimbali za makanisa zinazotoa huduma za afya nchini. Kwa mfano jedwali lifuatalo linaonesha baadhi ya fedha za umma zilizotolewa mwaka 2009 na 2010 na serikali kwa taasisi mbalimbali za makanisa zinazotoa huduma za afya nchini ikilinganishwa na kiasi cha fedha zinazopelekwa kwa taasisi za afya zinazomilikiwa na serikali.

Data za WIZARA YA AFYA zinaonesha kuwa hospitali na taasisi nyingine za afya zaidi ya 80 zinazomilikiwa na Makanisa zinaendeshwa kwa kutumia fedha za serikali. Aidha utafiti wetu umeonesha kuwa serikali imekuwa ikitumia mabilioni ya fedha kila mwaka kuendesha hospitali na taasisi za afya zinazomilikiwa na Makanisa.

Kwa mfano Jedwali lifuatalo linaonesha fedha za serikali zilizotumiwa na hospitali na taasisi za afya zinazomilikiwa na Makanisa ikilinganishwa na matumizi katika hospitali za serikali mwaka 2009 na 2010.
attachment.php

attachment.php


attachment.php

Jedwali hilo hapo juu linaonesha fedha zilitolewa na serikali kwa hospitali na taasisi nyingine za huduma ya afya zinazomilikiwa na makanisa na zile zinazomilikiwa na serikali kwa ajili ya kulipa mishahara wafanyakazi na gharama za uendeshaji.

Men lie, women lie, numbers dont lie....

attachment.php

attachment.php

attachment.php

chanzo: wizara ya Elimu



 
Dr.Tunashukuru kwa ufafanuzi wako mwanana.Serikali ya CCM inaelewa ukweli wote lakini kwa makusudi inawahadaa Waislamu kwa kutowaambia ukweli ili watu wafarakane kidini na yenyewe ipumue kwani ina stress ya kushindwa kuwaletea Watanzania Maisha Bora iliyowaahidi.Inaelewa Mashekh wengi(mf.shekh Ponda)hawana uwezo wa kufanya Research na hivyo ni wepesi wa kudanganyika.Serikali makini haiwezi kutegemea Cheap politics kama hizi.Tujiulize,Muda wote huu Waislamu wanavyopiga kelele kuhusu MOU kwa nini Serikali yenye kuujua ukweli wote isiwaambie ukweli?Hapo ndipo wenye akili huamini kwamba Waislamu hutumwa kuhubiri chuki.
 
One morning Jesus walked along the edge of Lake Galilee and beckoned to a few local fishermen. He said, “Follow me” (Matthew 4:19). At that moment, everything began for them. ‘Everything’ had only been fish, and then it became people, action, and changing world history, with ever-increasing faith, ever-increasing effects.
 
Du!!! Kumbe MOU maana yake ni makubaliano ya kimaendeleo baina ya Wakristo wa Tanzania na Ujerumani!!??? Kumbe serikali ya Tanzania iliridhia tu kama observer!!! Kweli jambo usilolijua ni kama usiku wa giza! Sasa maskini kelele nyingi kuhusu MOU ni za nini???
 
Dr. Slaa kaelezea kwa kirefu tu mantiki nyuma ya MoU. Nimeelewa.

Pamoja na maelezo ya kina juu ya jambo hili, hitimisho hili alivyoeleza Dr. Slaa:

Narudia tena, namshukuru sana aliyeweka kwenye JF MOU hiyo. Ninarudia kuwaomba wenzangu, tumetumia muda mrefu sana kujadiliana kwa hisia ya aina mbalimbali. Watanzania hatukuzoea huko nyuma kuulizana dini zetu, wala kabila wala ukanda. Haya mambo tukiyaendekeza Taifa letu litakuwa hatarini. Tukumbuke kubomoa ni kazi nyepesi sana, sekunde lakini kujenga tena inachukua muda mrefu na ni kaz ngumu, na wakati mwingine hata ukifanikiwa huwezi kujenga kama ilivyokuwa. Nashauri ili JF ibaki na heshima yake ya Home of Great Thinkers tupende kufanya Research zaidi kabla ya kulaumiana au kuhisiana, kama mtu hana taarifa za kina awaombe wenye taarifa. Kama mnavyoona mimi nilikuwa nafahamu historia yote, nafahamu MOU, lakini sikuwa nayo. Mtu huwezi kujua kila kitu na au kuwa na kila kitu, we need to complement each other. Tunaweza tukidhamiria, na JF itabaki na hadhi na heshima yake daima.

lina uzito stahiki kwa nchi yetu. Nakumbuka ilivyotokea kubomolewa kwa dakika kisha imebaki historia kama picha hiyo hapo chini katika jiji la New York ground zero. Tusiombe haya yatokee, nilishuhudia kwa macho yangu live hadi dege la pili linavyoingia kwenye mnara wa pili, bora kusikia kuliko kushuhudia. Ilikuwa kihoro, watu walikata tamaa, hakuna pa kujishika. Wengine wanarukia majini kuogelea mkondo wa Hudson river kuvukia Jersey City. Ilikuwa blaa tupu.


8284285337_cfb6b46466_z.jpg


:A S-omg:Amani:A S-omg:​
 
Sidhani kama hili ni tamko la Dr.Slaa kama mtoa mada ulivyoliweka.Ingekuwa sahihi zaidi kama ungeuchukulia huu kama ufafanuzi wa Dr.Slaa.Sio tamko.Tamko is more demanding,this one here presented by him is quite descriptive.Sio kila kitu ni tamko.Hili sio tamko,huu ni ufafanuzi.
 
Sidhani kama hili ni tamko la Dr.Slaa kama mtoa mada ulivyoliweka.Ingekuwa sahihi zaidi kama ungeuchukulia huu kama ufafanuzi wa Dr.Slaa.Sio tamko.Tamko is more demanding,this one here presented by him is quite descriptive.Sio kila kitu ni tamko.Hili sio tamko,huu ni ufafanuzi.

Jaribu kutazama na kuisoma vizuri taswira ya mada, utakuja kugundua kwa kuisoma body of language ni ya Dr. Slaa, moderator wamejitahidi kuunganisha na document. Inaonyesha Dr. Slaa hakuanza mada ila alichangia hiyo mada, moderator wakaiweka pamoja ili kuleta mtiririko wa habari.

JF ina safu ya wasanifishaji, haiendi kienyeji tu. Thanks Mods.
 
Wenye akili ndogo watakubali kwamba MOU iko safi lakini,ukweli utasimama,kuna dini nyingine wamezoea propaganda na uongo mana dini zao na imani zao zinawafundisha hivyo.unaweza kumdanganya mtu kwa muda flani ila huwezi kumfanya mjinga muda wote.eti wanadai MOU iko kisheria,Kanisa ndio waasisi wa Ufisadi Tanzania,ndio mana adui yao mkubwa ni ujamaa na uislamu,ukisoma kitabu cha prof Huntington na john Sivalon utajua mfumo kiristo wa nchi yetu.ha ha ha inachekesha sana mtu anavyofagilia MOU na kansa inayolitafuna taifa
 
Back
Top Bottom