Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,060
- 22,755
Ukimya wa Reginald Mengi wa IPP, aliyewahi kuapa hapo nyuma kuwa moto aliouwasha dhidi ya wahujumu na mafisadi wa nchi hii kamwe hautazimika, unatisha. Kwa mbali nakumbuka hotuba ya Jakaya Kikwete kwa wazee wa Dar es Salaam kuwa waliotaka kuleta mdomo wameshashughulikiwa na sasa wako kimya.
Je Reginald Mengi ni moja wa hawa watu walioshughulikiwa kimya kimya na sasa kapoa kama kamwagiwa maji ya friji. Kama hii itakuwa ni kweli, tumweleweje huyu Reginald Mengi, alikuwa ni mpiganaji wa kweli au wa kuchonga kama wale wachumia tumbo waliokuwa wakipayuka bungeni na kujiita wapiganaji ndani ya CCM ?
Wote aliodai amewawashia moto bado wanatamba na kusonga mbele lakini yeye pamoja na magazeti yake kimya. Hii ni sababu kubwa na tosha kwa wazalendo kuutambua ujasiri wa mpiganaji Dr. P. W. Slaa ambaye ameweza kusimama kidete kukabiliana na makombora ya mafisadi na vibaraka vyao ndani ya CCM na serikalini bila kutetereka.
Je Reginald Mengi ni moja wa hawa watu walioshughulikiwa kimya kimya na sasa kapoa kama kamwagiwa maji ya friji. Kama hii itakuwa ni kweli, tumweleweje huyu Reginald Mengi, alikuwa ni mpiganaji wa kweli au wa kuchonga kama wale wachumia tumbo waliokuwa wakipayuka bungeni na kujiita wapiganaji ndani ya CCM ?
Wote aliodai amewawashia moto bado wanatamba na kusonga mbele lakini yeye pamoja na magazeti yake kimya. Hii ni sababu kubwa na tosha kwa wazalendo kuutambua ujasiri wa mpiganaji Dr. P. W. Slaa ambaye ameweza kusimama kidete kukabiliana na makombora ya mafisadi na vibaraka vyao ndani ya CCM na serikalini bila kutetereka.
Tumuunge mkono Dr. P. W. Slaa, tuung'oe huu utawala wa kifisadi.