Moshi Chini ya CHADEMA: Yajipanga kulipia wanafunzi wa sekondari ada

huu upuuzi wa Bi Bernadeta Kinabo unatakiwa ku hit headline za magazeti.... sijawahi kukutana na pumba pevu kama hizi zaidi ya miaka ishirini ... yaani mungu amrehemu aende motoni
 
Hii ndo namna ya utendaji ya viongozi wa serikali yetu. Hakuna kiongoz anaemjali mwananchi. Huyu mama/bibi ni mtu anaefurahi kuona watz wanateseka. Ni pure SADIST
 
BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi limeanza kazi kwa kufanya mapinduzi makubwa kwenye bajeti yake ikiwamo kupunguza matumizi kwenye mambo yasiyo ya lazima huku ikiazimia kuwalipia ada wanafunzi wote wa shule za sekondari za kutwa.

Matumizi yaliyopunguzwa ni yale ya ofisi ya meya kutoka shilingi milioni 16 zilizotengwa kwenye bajeti ya mwaka 2010/11 hadi shilingi milioni 4.7 kwenye bajeti ya mwaka 2011/12.

Katika bajeti hiyo, kiasi kikubwa cha fedha kimepunguzwa kwenye fungu la chai na vitafunwa kutoka shilingi milioni 10.3 mwaka 2010/11 hadi kufikia milioni 1.8 kwa mwaka 2011/12.

Wanafunzi wa sekondari 8,528 watalipiwa ada ya shilingi 20,000 kila mmoja itakayogharimu halmashauri hiyo kiasi cha shilingi milioni 170.5 huku wazazi wao wakitakiwa kulipia michango mingine ya shule ikiwamo kulipia wapishi, walinzi na huduma nyingine zinazotolewa kwenye shule hizo.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa manispaa hiyo Bernadette Kinabo, alipingana na uamuzi wa madiwani hao juu ya kuwalipia ada wanafunzi kwa madai kuwa inapingana na sera ya serikali inayowataka wazazi kuwalipia wanafunzi wao ada ili wajisikie wana uchungu na elimu ya watoto wao.

Je viongozi kama hawa kweli wapo kwa faida ya Taifa? Kama Halmashauri/nchi inakusanya mapato ya kutosha kwa nini wananchi wake wasifaidike na matunda ya kazi yao? Je kumuacha Mzazi apate uchungu na ugumu wa maisha na kuweka budget yote kwenye Chai na vitafunwa ndio halali ya sera za CCM?
Huyu mkurugenzi anawakilisha mtazamo na mawazo ya aliyemteua, Yani RAIS& Waziri Mkuu na sera zao za CCM.
Watanzania tuamke na kuwaondoa hawa wanyonyaji.

Source: Tanzania Daima

Hongera CDM - Endelea kuonyesha njia.
 
........Hata hivyo, Mkurugenzi wa manispaa hiyo Bernadette Kinabo, alipingana na uamuzi wa madiwani hao juu ya kuwalipia ada wanafunzi kwa madai kuwa inapingana na sera ya serikali inayowataka wazazi kuwalipia wanafunzi wao ada ili wajisikie wana uchungu na elimu ya watoto wao.
Source: Tanzania Daima........

huyu mwananke siye kabisaa... kwa hiyo uchungu wa elimu unapimwa kwa elfu 20? inaelekea huyu she ukienda kwake hata maji ya kunywa
hupati ama anatumia mti ndiii kufikiria
 
Hongera CDM - Endelea kuonyesha njia.

mmmmh hiyo kauli ya mkurugenzi haina mashiko kabisa,MBONA ANASAHAU KUWA WAKATI WA NYERERE VIGOGO WENGI WALISOMA BURE!WAKATI ULE KUNGEKUWA NA WAKURUGENZI WAVIVU WA KUFIKIRI KAMA MAMA KINABO WANGEWEZA KUFIKA HAPO ?

Mi nadhani ingefaa kuridhia na kuona namna gani hiyo sera inaweza kuenezwa sehemu nyingine za nchi ili tuweze kupambana na ujinga.AU YEYE ANATAKA WAZAZI MASIKINI WAONE UCHUNGU KILA UCHAO?MBONA VIGOGO WANAPELEKA WATOTO WAO NJE TENA WAKATI MWINGINE KWA KODI ZA WALALAHOI?

IFIKE MAHALI TUANGALIE MASLAHI YA NCHI KWANI SI KILA KIANZISHWAPO NA WAPINZANI NI HARAMU,MENGINE MAZURI KWA MANUFAA YA TAIFA.


HONGERENI MADIWANI WA MOSHI KWA KUONESHA NJIA,WENGINE IGENI MPUNGUZIENI MLALAHOI MZIGO WA MAISHA.
 
mambo kama haya ndiyo cdm ilitakiwa at least ifanye toka mwanzo na siyo maandamano yasiyomsaidia mtanzania kwa sasa zaidi ya kuchochea chuki katika jamii. hapo madiwani wameonesha mchango wa mawazo yao na huyo mkurugenzi hatakiwi kupinga tu bila hoja labda yeye naye aseme hapana walipe ada lakini michango ya aina yoyote wao ndio watakao toa, maana wakuu kama mnavyojua shule za misingi ada ilitolewa lakini hiyo michango iliyopo imekuwa ni mara kadhaa ya ile ada waliyokuwa wanachangia. kwahiyo hilo nalo liangaliwe pia. maana isije ikaondolewa ada lakini michango ya wapishi wa chai na vitafunwa na walinzi ikawa mikubwa zaidi.lakini pia hao madiwani mawzo hayo kama yatafanya kazi yafikiriwe hadi ngazi ya A level kwani wasije fika huko wakakuta utaratibu huo wa kulipiwa haupo wazazi wakagoma kutoa ada.

Ingeyafanya vipi wakati wana wabunge na madiwani wachache katika bunge na Halmashari. usilete uvuvuzela hapa.
 
Huyo mama anadhani uchungu wa kuzaa hautoshi? Anataka kutuambia wananchi Watanzania wateseke ili waone uchungu! hayo wanaokunywa chai kwa gharama ya watoto hawastahili nao kuona uchungu?
 
sera nzuri ingeweza kuwa kuwalipia wanafunzi ambao wazazi/wasimamizi wao hawana uwezo na si kwa wote. kwa hali ya sasa kuna baadhi ya wafanyakazi au wafanyabiashara wenye uwezo mzuri tu. na kulipa ada huenda isingeweza kuwa shida. mf. Loan Board kwa wanafunzi wa vyuo vikuu.
hii nchi bado ina matatizo mengi including manispaa ya Moshi. kulipia kila mtu hata wenye wazazi wenye uwezo it doesn't make sense.
inategemea na vipaumbele
 
You are absolutely right Mkuu......................kuna sehemu nilisema hawa CDM ni kama sikio la kufa vile..............kuna vitu muhimu sana vinafanywa na CDM vya ku-capitalize na malengo yao..........lakini jamaa utaona wako kimya tu............

Mkuu we have to look about our darkness side sio kulichukulia jambo kama lilivyo na kama tunavyoelewa siasa ni mchezo unaohitaji umakini wa hali ya juu sana kuucheza kuliko ambavyo tunadhani.
Binafsi mimi niwasifu nakuwapongeza sana uongozi mzima wa Chadema kwanza kwa kuto kukurupukia kila jambo nahata kwa jambo ambalo ni tatizo na la moja kwa moja na lina takiwa kufikishwa kwa wana inji kama lilivyo bado lakini kwa busara zao huliangalia kwa mapana sana kama litabomoa au kujenga chama au wanainji na mali zao wataathirika vipi kama litafikishwa lilivyo na pindi inapo onekana linastahili kufikishwa kwa wana inji na mipango tekelezi huanzia hapo sio tu kila jambo likitokea kwenye jamii yetu jamaa wamwagike nalo nooo.!
Mchakato kama huu wa Moshi nikielelezo kua inji hii hata ikiamua kujiendesha yenyewe bila hata ya misaada ya hao wezi wetu tunaweza.
Changamoto zipo nyingi sana kwenye inji yetu tunahitaji yu kumpata kiongozi jasiri na makini ambaye ataweza kuiunganisha Tanzania iongee kwa sauti moja.
Naimani wa TANZANIA mioyo ya kizalendo bado inawaka ndani yetu bado tunasubiri wakutuunganisha tu.Hongera CHADEMA.
 
BARAZA la Madiwani wa Halmashauri ya Manispaa ya Moshi limeanza kazi kwa kufanya mapinduzi makubwa kwenye bajeti yake ikiwamo kupunguza matumizi kwenye mambo yasiyo ya lazima huku ikiazimia kuwalipia ada wanafunzi wote wa shule za sekondari za kutwa.

Matumizi yaliyopunguzwa ni yale ya ofisi ya meya kutoka shilingi milioni 16 zilizotengwa kwenye bajeti ya mwaka 2010/11 hadi shilingi milioni 4.7 kwenye bajeti ya mwaka 2011/12.

Katika bajeti hiyo, kiasi kikubwa cha fedha kimepunguzwa kwenye fungu la chai na vitafunwa kutoka shilingi milioni 10.3 mwaka 2010/11 hadi kufikia milioni 1.8 kwa mwaka 2011/12.

Wanafunzi wa sekondari 8,528 watalipiwa ada ya shilingi 20,000 kila mmoja itakayogharimu halmashauri hiyo kiasi cha shilingi milioni 170.5 huku wazazi wao wakitakiwa kulipia michango mingine ya shule ikiwamo kulipia wapishi, walinzi na huduma nyingine zinazotolewa kwenye shule hizo.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa manispaa hiyo Bernadette Kinabo, alipingana na uamuzi wa madiwani hao juu ya kuwalipia ada wanafunzi kwa madai kuwa inapingana na sera ya serikali inayowataka wazazi kuwalipia wanafunzi wao ada ili wajisikie wana uchungu na elimu ya watoto wao.

Je viongozi kama hawa kweli wapo kwa faida ya Taifa? Kama Halmashauri/nchi inakusanya mapato ya kutosha kwa nini wananchi wake wasifaidike na matunda ya kazi yao? Je kumuacha Mzazi apate uchungu na ugumu wa maisha na kuweka budget yote kwenye Chai na vitafunwa ndio halali ya sera za CCM?
Huyu mkurugenzi anawakilisha mtazamo na mawazo ya aliyemteua, Yani RAIS& Waziri Mkuu na sera zao za CCM.
Watanzania tuamke na kuwaondoa hawa wanyonyaji.

Source: Tanzania Daima

1. Hongereni Chadema kwa kuthubutu kupingana na uongozi-kwa-mazoea (business as usual)

2. Pamoja na hayo, kuna ukweli kuwa kutoa elimu bure siyo solution. Inajenga "sense of entitlement", yaani, dhana ya kuwa unastahili kitu kwa kuwa upo tu. Hii ni mbaya sana kwani;

- inapunguza juhudi ya wananchi kujitafutia. Juhudi za kujitafutia ndiyo uchumi wenyewe
- inapunguza thamani ya kitu kinachotolewa bure. Watu wanakichukulia poa
- unazoesha watu tabia mbaya ya utegemezi

Ushauri wangu ni kuwa hizo million 170.5 kwa mwaka, zingetumika kukarabati shule ili Moshi iwe na shule nzuri kuliko miji yote Tanzania ifikapo mwaka 2015. Kila mwaka karabati shule kadhaa.

3. Ukitaka kuona athari za hii dhana ya kustahili angalia viongozi wa sasa na mashangingi yao. Yaani mtu kwa kuwa tu ni mkurugenzi, basi hawezi tena kupanda land-rover. Au eti hawezi kutibiwa Mawenzi hospital ni lazima aende Morningside Hospital Sandton akatibiwe tumbo la kuhara. Siyo kwa sababu amefanya kitu kikubwa sana, la hasha, ni kwa sababu yeye ni yeye tu.

Tusiilete hi dhana kwa wananchi, kwani tupo wengi mno.
 
Aisee budget ya chai ya mil 10.3 kwa mwaka ni sawa na zaidi ya laki 8 kwa mwezi au 42,000/= kwa siku (Ada ya watoto 2). Hiyo Ofisi ina wafanya kazi wangapi ambao hutumia that amount per day?

Hongera CDM; mlistahili kuchukua nchi, now l can see ACTIONS loud and clear, sio maneno ya matumaini ya kila siku ya watu waliokulia kwebye Mipasho!

Ukizingatia bongo tuna sikukuu karibu mbili kila mwezi, unakuta hiyo 42,000.00 inaweza kuwa 45,000.
 
1. Hongereni Chadema kwa kuthubutu kupingana na uongozi-kwa-mazoea (business as usual)

2. Pamoja na hayo, kuna ukweli kuwa kutoa elimu bure siyo solution. Inajenga "sense of entitlement", yaani, dhana ya kuwa unastahili kitu kwa kuwa upo tu. Hii ni mbaya sana kwani;

- inapunguza juhudi ya wananchi kujitafutia. Juhudi za kujitafutia ndiyo uchumi wenyewe
- inapunguza thamani ya kitu kinachotolewa bure. Watu wanakichukulia poa
- unazoesha watu tabia mbaya ya utegemezi

Ushauri wangu ni kuwa hizo million 170.5 kwa mwaka, zingetumika kukarabati shule ili Moshi iwe na shule nzuri kuliko miji yote Tanzania ifikapo mwaka 2015. Kila mwaka karabati shule kadhaa.

3. Ukitaka kuona athari za hii dhana ya kustahili angalia viongozi wa sasa na mashangingi yao. Yaani mtu kwa kuwa tu ni mkurugenzi, basi hawezi tena kupanda land-rover. Au eti hawezi kutibiwa Mawenzi hospital ni lazima aende Morningside Hospital Sandton akatibiwe tumbo la kuhara. Siyo kwa sababu amefanya kitu kikubwa sana, la hasha, ni kwa sababu yeye ni yeye tu.

Tusiilete hi dhana kwa wananchi, kwani tupo wengi mno.



tayari moshi ina shule bora kabisa tanzania... ingawa ushauri wako ni mzuri, labda tuangalie njia gani ingine ambayo tunaweza kuzitumia hizo fedha ili ziwe kwa manufaa zaidi
 
Chai ni sehemu ya chakula ambapo Mtumishi yoyote analipwa mshahara ili kukidhi mahitaji yake ikiweomo la chakula.
Sio watumishi wote maofisini huwa wanapata huduma ya chai (hasa wale wa chini wenye mishahara midogo) ila huwa wanakunywa chai kwa mishahara yao hiyo hiyo midogo, inashindikanaje kwa mkurugenzi ambae mshahara wake ni above 1.7m kunywa chai kwa mshahara wake.
sioni haja wala mtu kufanya mambo ya kistarehe wakati kuna watu wanapata shida. nafikiri kama huyo mkurugenzi hata kubaliana na wazo la madiwani wampigie kura ya kutokuwa na imani nae ili atoke. tukiweza kufanya hivi atimae halimashauri nyingi zitaiga na hivyo kuendelea kutekeleza sera za CDM ingawa hatujashika dola, tukishika dola itakuaje?
 
1. Hongereni Chadema kwa kuthubutu kupingana na uongozi-kwa-mazoea (business as usual)

2. Pamoja na hayo, kuna ukweli kuwa kutoa elimu bure siyo solution. Inajenga "sense of entitlement", yaani, dhana ya kuwa unastahili kitu kwa kuwa upo tu. Hii ni mbaya sana kwani;

- inapunguza juhudi ya wananchi kujitafutia. Juhudi za kujitafutia ndiyo uchumi wenyewe
- inapunguza thamani ya kitu kinachotolewa bure. Watu wanakichukulia poa
- unazoesha watu tabia mbaya ya utegemezi

Ushauri wangu ni kuwa hizo million 170.5 kwa mwaka, zingetumika kukarabati shule ili Moshi iwe na shule nzuri kuliko miji yote Tanzania ifikapo mwaka 2015. Kila mwaka karabati shule kadhaa.

3. Ukitaka kuona athari za hii dhana ya kustahili angalia viongozi wa sasa na mashangingi yao. Yaani mtu kwa kuwa tu ni mkurugenzi, basi hawezi tena kupanda land-rover. Au eti hawezi kutibiwa Mawenzi hospital ni lazima aende Morningside Hospital Sandton akatibiwe tumbo la kuhara. Siyo kwa sababu amefanya kitu kikubwa sana, la hasha, ni kwa sababu yeye ni yeye tu.

Tusiilete hi dhana kwa wananchi, kwani tupo wengi mno.
The Stig

Una maana gani unaposema tusiilete hii dhana kwa wananchi hutaki wazazi wapate msaada, kama nchi zinazotupa misaada zingekuwa na mawazo kama yako kuwa zisitoe misaada kwa sababu nchi masikini nyingi budget yetu isingekuwa inatosha hata Quater moja.

Serikali ina budget ya maendeleo, ina pokea msaada chini ya mpango wa MMEM na MMES wa kuendeleza elimu (shule za kata) ikiwemo kuboresha majengo, mbali ya kupokea misaada kwa ajili hiyo Serikali haitimizi wajibu wake. Hadi sasa kwenye huo mpango hakuna sehemu iliyotengwa na serikali kwa ajili ya kulipia wanafunzi, wanachofanya Chadema ni kusaidia sehemu ambayo serikali haina hata wazo, inawasaidia wazazi kulipia ada za watoto wao. Ni kipi cha msingi kumsaidia mzazi au kuisaidia serikali inayotumia vibaya funds za maendeleo ikiwemo kuboresha majengo.

Nashangaa sana watu wenye mawazo kama yako akiwemo huyo mkurugenzi ni kama wivu fulani vile kwa sababu nyie mnauwezo wa kusomesha na kuwalipia watoto wenu nje sasa mkiona wazazi wengine wanawezeshwa ili watoto wao angalau wapate elimu ya msingi hampendi kwa kisingizio cha eti wazazi hawataona uchungu, inawezekana kabisa hata huyo Kinabo alipata elimu ya bure ina maana wazazi wake hawakuwa na uchungu kwa vile serikali ilimsomesha bure, ni mawazo mgando kabisa ndiyo maana nikayaita ni Bogus statement ya mwaka.
 
The Stig

Una maana gani unaposema tusiilete hii dhana kwa wananchi hutaki wazazi wapate msaada, kama nchi zinazotupa misaada zingekuwa na mawazo kama yako kuwa zisitoe misaada kwa sababu nchi masikini nyingi budget yetu isingekuwa inatosha hata Quater moja.

Serikali ina budget ya maendeleo, ina pokea msaada chini ya mpango wa MMEM na MMES wa kuendeleza elimu (shule za kata) ikiwemo kuboresha majengo, mbali ya kupokea misaada kwa ajili hiyo Serikali haitimizi wajibu wake. Hadi sasa kwenye huo mpango hakuna sehemu iliyotengwa na serikali kwa ajili ya kulipia wanafunzi, wanachofanya Chadema ni kusaidia sehemu ambayo serikali haina hata wazo, inawasaidia wazazi kulipia ada za watoto wao. Ni kipi cha msingi kumsaidia mzazi au kuisaidia serikali inayotumia vibaya funds za maendeleo ikiwemo kuboresha majengo.

Nashangaa sana watu wenye mawazo kama yako akiwemo huyo mkurugenzi ni kama wivu fulani vile kwa sababu nyie mnauwezo wa kusomesha na kuwalipia watoto wenu nje sasa mkiona wazazi wengine wanawezeshwa ili watoto wao angalau wapate elimu ya msingi hampendi kwa kisingizio cha eti wazazi hawataona uchungu, inawezekana kabisa hata huyo Kinabo alipata elimu ya bure ina maana wazazi wake hawakuwa na uchungu kwa vile serikali ilimsomesha bure, ni mawazo mgando kabisa ndiyo maana nikayaita ni Bogus statement ya mwaka.

Aisee nimekuelewa mtazamo wako!:lying:

Umejikita kwenye hiyo na siyo rahisi kukutoa huko, tutaishia kujibizana tu.

Lakini ushauri wa bure (manake kwa dezo haujambo), NOBODY OWES YOU ANYTHING. Ukiishi unategemea misaada na kuwezeshwa utaishia kuwa mzigo kwa jamii. This country will become strong only when everyone is pulling his own weight and creating value. Wale mnaokaa vibarazani mnasubiri kuwezeshwa na kodi zilizokatwa kwa wenzenu wanaofanya kazi hamsaidii hili taifa.
 
Aisee nimekuelewa mtazamo wako!:lying:

Umejikita kwenye hiyo na siyo rahisi kukutoa huko, tutaishia kujibizana tu.

Lakini ushauri wa bure (manake kwa dezo haujambo), NOBODY OWES YOU ANYTHING. Ukiishi unategemea misaada na kuwezeshwa utaishia kuwa mzigo kwa jamii. This country will become strong only when everyone is pulling his own weight and creating value. Wale mnaokaa vibarazani mnasubiri kuwezeshwa na kodi zilizokatwa kwa wenzenu wanaofanya kazi hamsaidii hili taifa.

Stig. in addition to you concern naweza kusema kwa kutumia mifano ya baadhi ya wanafunzi ambao wanasomeshwa na halmashauri kadhaa (kwa mfano wakai nikiwa Karatu nililiona hili), sio tu kwamba watoto wanapewa ufadhili tu ili mradi wamepewa ufadhili na ionekane kuwa wamepewa ufadhili, hapana, ila inaambatana na tathmini ya hali ya juu ambayo mwisho ndiyo inayoamua nani wanastahili kweli kuwa beneficiaries wa udhamnini huo

Kwa mfano mimi nimeshuhudia mtoto mmoja ambae mpaka mwezi wa 4 unafika alichaguliwa shule moja ya sekondari lakini hakwenda ila alikuwa anazurura tu kwa kukosekana fedha za kumsomesha mpaka pale ambao halmashauri ilikuja kuingilia kati wakati ule ndipo akaenda shule

Sasa katika hali kama hii huwezi kuweka tu doubt kirahisi kuwa itajenga dependency syndrome....labda kama haitaendeshwa vizuri na selection ya beneficiaries ikawa bias na ku-favor wenye uwezo ikiwatupa wanyonge na wasio na uwezo pembeni kitu ambacho tayari CCM wameshafanya na CDM haina haja ya ku-duplicate approach hii ya CCM zaidi ya kuja na ya kwake ya kinyume (favoring the minority as opposed to wenye nazo)
 
Back
Top Bottom