Morogoro: Viongozi wa CHADEMA wakamatwa na polisi, vurugu zaibuka!

ccm dhaifu, mwenyekiti wake dhaifu, maamuzi yake dhaifu..........dhaifu kila kona. Haina tena uwezo wa kuwaongoza watanzania.
 
Ni kweli. Polisi wamevuruga maandamano yaliyokuwa yafanyike kwenda eneo la mkutano, Uwanja wa Ndege, hapa Morogoro Mjini. Wamedhalilisha viongozi waliowakamata na sasa wameanza kuomba samahani, yaishe.

Kamanda wa Polisi Morogoro, Shilogile (mnaojua alihamishwa Dar es Salaam kuja hapa...) amevunja makubaliano yaliyofanyika mara mbili ya kuruhusu maandamano. Tunajua wapo wanasiasa hapa Morogoro ambao hawataki meseji ifike leo kwa wakazi wa Morogoro Mjini.

Inajulikana namna ambavyo CCM wamekuwa shaken big time na operesheni iliyokuwa na mafanikio huko vijijini, itawaumiza zaidi ikifanikiwa hapa mjini. Kwa hiyo lengo hapa si kuvuruga tu maandamano, bali ni kuvuruga mkutano, ili hatimaye watu waogope kuja mkutanoni, ujumbe usifike. Hawatafanikiwa kwa hilo, maana wananchi sasa wanazidi kujikusanya, maeneo kama ya Masika, kwenda eneo la mikutano, kwa maandamano.

Polisi wanachafua mji sasa, polisi wanawapitisha wana-Morogoro kwenye tanuru ambalo watu wa Mwanza, Mbeya, Arusha, Moshi, Musoma, Tarime, Ruaha na kwingineko kwingi, walipita/kupitishwa ili kuwa hapo walipo wakiwa na imani isiyoyumba katika mapambano haya ya kudai na kuwaandaa Watanzania kwa mabadiliko makubwa ya kimfumo na kiutawala. Chuma hakiwezi kuwa chuma mpaka kipite kwenye tanuru, lakini why doing it unnecessary?

Tutawapatia more updates on the issue?
well said kamanda Makene, nimefarijika Moro kupita kwenye hilo Tanuru, wawe STRONG... safi sana poliCCM kwa kuzidi kutukomaza na kututoa woga wa kupigwa mabomu ya machoz. go on poliCCm
 
Source: Radio aboud polisi mkoani morogoro wanakabiliana na waandamanaji wa chadema..mmoja anadaiwa kupigwa na polisi,hali yake ni mbaya.
 
Watakaoanzisha fujo hapo ni vibaraka wa CCM ambao ni baadhi ya polisi wasio na uelewa.
 
toba... niko huku juu barabara ya kingalu nasikia Pipoooz Power.....!!!!!, ila shukuru kuwa mabom yameisha sasa
 
Nguvu ya umma imeshinda mabomu ya polisi na mabavu ya polisi. Watu wameandamana na tayari wameshakusanyika eneo la mkutano, Uwanja wa Ndege.

Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Hamad Mussa Yusuf naye alikamatwa, lakini wamemwamchia. Bado wanamshikilia Kigaila, hawataki kumpeleka kituoni, badala yake wanazunguka naye ndani ya gari.

Pia walimkamata mwandishi mmoja wa habari, kwa kupiga picha (sijui ni kosa?????), lakini naye pia wamemwachia.
 
Nape alishasema CHADEMA watafanya mkutano wao Morogoro na utakuwa na fujo yeye alijuaje kama sio maandalizi ya chama mbadala kuwapiga mabomo wananchi wasio na hatia?

Ikumbukwe hata wakati tunatafuta UHURU hata wakoloni hawakufanya vurugu kuwapiga wananchi ambao walitaka kuwarudisha kwao kutoka nchi waliyoizoea wakati huo TANGANYIKA waliwakubalia watanganyika na kuwaachia nchi yao tukapata Uhuru leo watu wanataka babadiliko tena ya Amani polisi mnawapiga Baba Zenu, mama zenu, Dada zenu, Kaka zenu hata watoto wenu kisa watu wanakusanyika kwenda kwenye mkutano wa chama Chao je mnataka wasikutane kujadili yanayogusa nchi yetu?

Bahati mbaya nyie Mapolisi mnashindwa kumwambia MFALME aliye juu ya Jukwaa Mbele yenu, kwamba Mfalme inuka ukae vizuri juu ya kiti ulichopewa kuketi kwani umekaa UUUUUUUCHI ndio kwa maana kusanyiko la watu walio mbele yako wanakucheka kwa vile hujavaa nguo vizuri, na wengine wanahuzunika kwa jinsi unavyoonekana upaswi kukaa mkao huooooooooooo, jifunzeni alama za nyakati Angalieni kwa OBAMA nchi kubwa duniani sasa hivi wapo katika mchuano wa kinyanganyiro cha Urais lakini uwezi kusikia mwananchi wa kawaida kapigwa Bomu kisa eti hakitaki chama Tawala viongozi wa Tanzania tunajijengea tabia ya chuki miongoni mwetu huku mkijinadi nchi ya utulivu na Amani Amani iko wapi polisi mnaacha kufukuzana na majambazi mnashindwa kulinda mipaka yetu vizuri maharamia wanapenya kutoka nchi hadi nchi haya hamyaoni , hamwaoni wanaotorosha fedha za walala hoi lasilimali zetu yote haya macho yenu hayaoni.

Mnapoteze fedha ya wtz kutumia magari yetu ya walala hoi kuwaumiza watu wasio na hatia.

Eeeeeeeeeee Mwenyezi Mungu Watie Upofu wa Macho wadhalimu hawa wasioziona shida za wenzao macho yakawaonyesha wale wanaoiambia Dunia Mdhambi yanayotendeka ndani ya nchi yao.
 
mxii kitaeleweka tu, ccm ni km ghost halina uhai lkn linatesa wananchi, sasa tunalimalizia kwa kulizika moja kwa moja
 
Polisi wetu hawana jipya, wameshindwa kuwakamata watu waliojifungia msikitini mbagala kuharibu sensa, wanawapiga mabomu raia walioahidiwa maisha bora , yaliyogeuka maji jangwani
 
Nguvu ya umma imeshinda mabomu ya polisi na mabavu ya polisi. Watu wameandamana na tayari wameshakusanyika eneo la mkutano, Uwanja wa Ndege. Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Hamad Mussa Yusuf naye alikamatwa, lakini wamemwamchia. Bado wanamshikilia Kigaila, hawataki kumpeleka kituoni, badala yake wanazunguka naye ndani ya gari. Pia walimkamata mwandishi mmoja wa habari, kwa kupiga picha (sijui ni kosa?????), lakini naye pia wamemwachia.

Mara zote CCM na polisi ndo wachochezi wa fujo. Hawataki kuamini kuwa utawala wao umefika ukingoni.
 
Nguvu ya umma imeshinda mabomu ya polisi na mabavu ya polisi. Watu wameandamana na tayari wameshakusanyika eneo la mkutano, Uwanja wa Ndege. Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Hamad Mussa Yusuf naye alikamatwa, lakini wamemwamchia. Bado wanamshikilia Kigaila, hawataki kumpeleka kituoni, badala yake wanazunguka naye ndani ya gari. Pia walimkamata mwandishi mmoja wa habari, kwa kupiga picha (sijui ni kosa?????), lakini naye pia wamemwachia.
Huo ni ujumbe tukiamua tunaweza kwa nguvu ya umma M4C forever!
 
Haya maandamano ni upuuzi mtupu bora wachezee kichapo, wameyataka wenyewe liwalo na liwe.
 
Wimbo:peleka mtoto akapate elimu eee atafaidika na maisha yake.dunia ilivyo hivyo ndivyo ilivyo.
Katiba mpya:police lazima awe amemaliza form six awe na prinsipal walau 2.
 
Nguvu ya umma imeshinda mabomu ya polisi na mabavu ya polisi. Watu wameandamana na tayari wameshakusanyika eneo la mkutano, Uwanja wa Ndege. Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Hamad Mussa Yusuf naye alikamatwa, lakini wamemwamchia. Bado wanamshikilia Kigaila, hawataki kumpeleka kituoni, badala yake wanazunguka naye ndani ya gari. Pia walimkamata mwandishi mmoja wa habari, kwa kupiga picha (sijui ni kosa?????), lakini naye pia wamemwachia.

Ikifika hapa hua naikumbuka sana ile mistari ya SUGU "Huwezi kuzuiya mvua, kama inanyesha inanyesha tu". Upepo huu hauzimiki tena,.. hii ni masika kuu.. nguvu, hila, vitisho na ghiliba, havina tena nafasi katika kuwazuia watanzania kutafuta haki zao, kupigania mabadiliko na kujenga nchi yao yenye ustawi na uongozi thabiti kwa mustakabali wa Tanzania na watanzania wa vizazi hivi na vijavyo.

Nafurahi sana maana pia kila leo polisi wanatenda bila kujifunza, hata sikumoja vitisho, mitutu na mabomo havijawahi kupata kuwa ufumbuzi endelevu wa kuzuia maandamano na kukinga watu kutumia haki na uhuru wao zaidi milio hiyo na vitisho hivyo vimeendelea kuwajenga watanzania shupavu zaidi na inawapa watanzania hari zaidi, kujiamini zaidi na utayari zaidi wa kudai haki zao... wajifunze Arusha, Mwanza, Tarime, Mbeya na Songea... Mabomu yameendelea kutuimarisha na kuwapa watanzania moyo wa utayari zaidi.

Viva CDM.... aluta continua
 
Mbunge mwarabu Abood ndio kalazimisha eti huo mkutanoM4C, usifanyike kwa garama yoyote!
swali; kwa nini polisi inatumiwa/ kuamuliswa na mtu yoyote hapa Bongo? mbunge na jeshi la polisi wapi na wapi?

Hivi kwa nini huyo mwarabu asiuwawe?
 
Back
Top Bottom