AdvocateFi
JF-Expert Member
- Jan 15, 2012
- 11,492
- 5,040
Mida hii nikiwa hapa morogoro mjini msamvu ambapo polisi wamewatia mbaroni viongozi wa CHADEMA akiwemo na BENSON KIGAAlA.
Subirieni taarifa zaidi.
=====================
MATUKIO KATIKA PICHA
=====================
============================
Marehemu Ally Zona [R.I.P Kamanda]
============================
==================
MMOJA WA MAJERUHI
==================
Subirieni taarifa zaidi.
Habari kutoka Morogoro zimetufikia hivi punde kutoka chanzo cha uhakika nguvu ya umma imeshinda watu wanaendelea na maandamano baada ya Mabomu kushindwa kutawanya watu. Hali ni tete polisi wamelegea mabomu yamewaishia watu wanasonga mbele
Ni kweli. Polisi wamevuruga maandamano yaliyokuwa yafanyike kwenda eneo la mkutano, Uwanja wa Ndege, hapa Morogoro Mjini. Wamedhalilisha viongozi waliowakamata na sasa wameanza kuomba samahani, yaishe.
Kamanda wa Polisi Morogoro, Shilogile (mnaojua alihamishwa Dar es Salaam kuja hapa...) amevunja makubaliano yaliyofanyika mara mbili ya kuruhusu maandamano. Tunajua wapo wanasiasa hapa Morogoro ambao hawataki meseji ifike leo kwa wakazi wa Morogoro Mjini.
Inajulikana namna ambavyo CCM wamekuwa shaken big time na operesheni iliyokuwa na mafanikio huko vijijini, itawaumiza zaidi ikifanikiwa hapa mjini. Kwa hiyo lengo hapa si kuvuruga tu maandamano, bali ni kuvuruga mkutano, ili hatimaye watu waogope kuja mkutanoni, ujumbe usifike. Hawatafanikiwa kwa hilo, maana wananchi sasa wanazidi kujikusanya, maeneo kama ya Masika, kwenda eneo la mikutano, kwa maandamano.
Polisi wanachafua mji sasa, polisi wanawapitisha wana-Morogoro kwenye tanuru ambalo watu wa Mwanza, Mbeya, Arusha, Moshi, Musoma, Tarime, Ruaha na kwingineko kwingi, walipita/kupitishwa ili kuwa hapo walipo wakiwa na imani isiyoyumba katika mapambano haya ya kudai na kuwaandaa Watanzania kwa mabadiliko makubwa ya kimfumo na kiutawala. Chuma hakiwezi kuwa chuma mpaka kipite kwenye tanuru, lakini why doing it unnecessary?
Tutawapatia more updates on the issue?
Nguvu ya umma imeshinda mabomu ya polisi na mabavu ya polisi. Watu wameandamana na tayari wameshakusanyika eneo la mkutano, Uwanja wa Ndege. Naibu Katibu Mkuu Zanzibar, Hamad Mussa Yusuf naye alikamatwa, lakini wamemwamchia. Bado wanamshikilia Kigaila, hawataki kumpeleka kituoni, badala yake wanazunguka naye ndani ya gari. Pia walimkamata mwandishi mmoja wa habari, kwa kupiga picha (sijui ni kosa?????), lakini naye pia wamemwachia.
Taarifa ambazo nimeweza kuzithibitisha ni kuwa kuna watu watatu wamepigwa risasi, ni risasi za moto. Mmoja amekufa baada ya risasi kumpata kichwani, anaitwa Ally Zona; wengine wawili wamelazwa hospitali ya Mkoa wa Morogoro.
I'll keep u updated wakuu, for anything good or bad...
Habari za uhakika ni kua polisi wameua mtu maeneo ya Msamvu bila sababu ya msingi,kisa ni kua walikua tu wanajaribu kuzuia maandamano ya Cdm na kijana huyo aliyekua akiuza magazeti aliwaonyesha alama ya V ndipo walipomlipua! My take: ni wazi jeshi la police chini ya IGP Mwema limeshindwa kuwalinda raia na mali zake,na kuwachukulia hatua wezi wakubwa na wahujumu nchini,bali jeshi la polisi limegeuka kua la mauaji kwa raia wasio na hatia kwa jinsi watakavyo! Source: mimi mwenyewe nipo kwenye mkutano hapa Morogoro
=====================
MATUKIO KATIKA PICHA
=====================
Wafuasi wa chama cha demokrasia na maendeleo chadema
Askari waliokuwa katika eneo la tukio kabla ya kuanza kwa maandamano hayo
Moshi wa mabomu yaliolipuliwa kutawanya maandamano ya chadema leo mjini morogoro
Gari la chadema lililokuwa likiongoza maandamano hayo
Mmoja wa kiongozi wa chadema akiwa amekamatwa akiwa ndani ya gari la polisi
Wafuasi wa chadema wakiwa na maandamao hayo mjini morogoro
============================
Marehemu Ally Zona [R.I.P Kamanda]
============================
==================
MMOJA WA MAJERUHI
==================