Morgan Tsvangirai ashinda kesi ya ndoa.

S2dak_Jr

Senior Member
Jul 15, 2012
198
45
Jamaa ameshinda kesi dhidi ya pingamizi la kutofunga ndoa liliowekwa na mwanamke mmoja anayedai kuwa ana ndoa na PM huyo wa Zimbabwe.

Habari zinadai kuwa anatarajia kufunga ndoa na mwanamke wake wa sasa Bi. Elizabeth na kumuacha yule waliyekuwa na ndoa ya kitamaduni.

Jaji wa Mahakama Kuu aliyesikiliza kesi hiyo kwenye mazingira ya faragha, amesema kuwa ndoa za kitamaduni hazitambuliki kwa sasa na Bi. Tembo hakustahili kufikisha shauri hilo kwenye Mahakama Kuu.

Bi. Tembo ameshauri kulipeleka shauri hilo kwenye Mahakama za chini na si kuzuia ndoa bali afikishe hoja ya kugawana mali kwani ndoa za kitamaduni hazitambuliki na katiba/sheria za nchi hiyo.

Rais Robert Mugabe anatarajiwa kuhudhuria misa ya ndoa hiyo na kuwaandalia sherehe Ikulu, Mjini Harare.

Source: bbc.co.uk/swahili
 
Hataki Morgan aoe mwanamke mwingine na wakati huo huo ampimie kinyama ugomvi ( pressumably) ! Kazi kweli kweli na akina mama zetu! Si amtakie tu harusi njema au bado tu ana matumaini ya kwamba ataendelea kutifuliwa na Tsvangirai?
 
Hataki Morgan aoe mwanamke mwingine na wakati huo huo ampimie kinyama ugomvi ( pressumably) ! Kazi kweli kweli na akina mama zetu! Si amtakie tu harusi njema au bado tu ana matumaini ya kwamba ataendelea kutifuliwa na Tsvangirai?



Issue hapa ni kuwa First Lady kama jamaa akiichukuwa nchi au kuwa PM's Wife kama akiolewa yeye.
 
Hadithi kama ya hapa kwetu......kwanini viongozi wA upinzani wanakuwa na matatiZo ktj ndoa zao???
 
Henry Kissinja the former US secretary of state said and i quote: "Law is like the web, it's to strong for the weak and too weak for the strong"
 
Back
Top Bottom