Moral Question: Morphine (drug) iruhusiwe kupunguza maumivu makali?

Shinto

JF-Expert Member
Dec 6, 2010
1,781
96
Wakuu nimekutana na hii issue mara mbili watu waki-debate. Nikaona si vibaya nikaleta kwa great thinkers tupate mawazo na mitizamo yenu.
  1. Medical marijuana: Kuna baadhi ya states huko U.S na MExico zimeridhia watu kupanda kisha kutumia marijuana kama njia ya kupunguza aina fulani za maumivu. Kuna mama mmoja alikuwa akitoa ushuhuda kwamba bila kutumia hiyo kitu hiwa hawezi kufanya kazi yeyote productive. Amekwenda kwa treatment for more than 30 years bila mafanikio, relief aliipata alipoanza kutumia medical marijuana!
  2. Morphine: Hii ni aina ya dawa maarufu kama nusu kaputi! ambayo imekuwa ikitumiwa kwa muda mwingi wakati wa kufanya upasuaji. Muhimu kujua ni kwamba hii dawa ina uhusiano wa karibu mno na madawa maarufu ya kulevya cocaine au heroine. (nadhani yanatokana na mmea mmoja poppy..not so sure)! Katika baadhi ya nchi hii dawa hutumiwa na watu wenye maaumivu makali na endelevu, kama vile cancer isiyopona, HIV AIDS na mengeni kama hayo!
Swali ni je, kutumia dawa hizo kwa malengo haya ni sawa na ulevi wa kawaida wowote? Je ni haki kuacha watu wateseke wakati kuna uwezekanano wa kuwapunguzia maumivu? Nenda pale ocean road ukaone watu wanavyolia kwa maumivu makali, kwa nini tusiwape tuu? Is it morally justified?

Nawasilisha!
 
Of course why not..., marijuana is a medicine (although some people are using it wrongly by smoking it) am sure if you smoke anything even paracetamol or majani ya mchicha will have ill effects..

I will even go one step further and say that marijuana should be offered in pharmacies for responsible users just as another kilevi...

By the way because people are using knives for killing its not right to stop selling knives which people might use to cut their tomatoes
 
Kuna documentary nilikuwa naangalia juzi Al-Jazeera. Uganda mbona huhitaji hata Daktari kukuandikia perscription, nesi tu anatosha, tena anakuletea mpaka nyumbani. Rationale yao ni kwamba, nchi yetu masikini na hatuwezi kuwatibu wagonjwa wengi, magonjwa mengine kama kansa hayana hata tiba hususan yakifika stage mbaya, na huku kwetu watu hawafanyi regular check-ups, kwa hiyo wanajishtukia wako kwenye hii stage mbaya, kwa hiyo kitu pekee cha kufanya ni kuwaongezea "quality of life" kabla hawajafa. Tuwape morphine waondoe maumivu.

Kuna jamaa mmoja Ukraine alikuwa anakusanya vidonge vya painkillers ambavyo vina amount ndogo za morphine, anavitumia kutengeneza morphine halafu anaisambaza kwa wagonjwa waliokuwa wanahitaji, against the law.

Inasikitisha sana.

Pale Ocean Road wagonjwa wa kansa wenye maumivu makali wanapewa sana tu.

Story ya hii documentary iko hapa Documentary by UBC journalism students aired on Al Jazeera

D
ocumentary yenyewe iko hapa

http://english.aljazeera.net/programmes/peopleandpower/2011/07/2011720113555645271.html
 
Je ni haki kuacha watu wateseke wakati kuna uwezekanano wa kuwapunguzia maumivu? Nenda pale ocean road ukaone watu wanavyolia kwa maumivu makali, kwa nini tusiwape tuu? Is it morally justified?
Nawasilisha!

Hili ni suala nyeti mkuu hasa ukizingatia sera na guidelines zinazotoa kibali kwa hospitali chache sana ( za mkoa kama sikosei) zinazoruhusiwa kutoa haya madawa makali ya kupunguza maumivu.

Ukiangalia maradhi na maumivu yako nchi nzima na kwa level zote na siyo wote wanaweza kwenda kwenye designated hospitals.Lakini hapo hapo kuna tatizo la kupambana na abuse ya madawa kama hayo uliyoyataja.

Najua kwa mfano nchi kama USA wana tatizo kubwa sana la wahudumu wa afya ku abuse madawa ikiwemo kutumia madawa ya mgonjwa na ndio maana wameweka computerised systems kuhakikisha kila nurse anayechukua dawa kwa kumpa mgonjwa anazifikisha kwa mgonjwa na siyo kuzitumia yeye mwenyewe.Ilikuwapo kesi ya baba mmoja aliyechukuliwa dawa zake za maumivu na alipolalamika nurse wa kike alitumia silaha ya kumtaka mwanaume agangamale avumilie maumivu ( man-up!).... sasa nchi maskini kama yetu ambapo kila kitu kinachakachuliwa itakuwaje?
 
Hili ni suala nyeti mkuu hasa ukizingatia sera na gudelines zinatoa kibali kwa hospitali chache sana ( za mkoa kama sikosei)ndizo pekee zinaruhusiwa kutoa haya madawa makali ya kupunguza maumivu.
Hapa the simplest way in regard to marijuana watu wasibuguziwe kulima marijuana sababu inaweza kutumika kama mboga na pia ni dawa.., kosa la bangi ni kuvuta na sio kutumia wala kuila...
 
Ningependa kusikia michango ya watu wa dini pia...........Je ni "dhambi" kutumia haya madawa kwa namna hii?
 
Sioni mantiki ya kuzuia wagonjwa wenye maumivu wasitumie Morphium. Nimeshuhudia mgonjwa wa kansa aliyekuwa kwenye stegi za mwisho za uhai, ilibidi apewe Morphium ili kumsaidia kupunguza maumivu makali wakati akisubiri kifo. It was soo sad seeing a person putting on a morphium plaster which was killing him softly.... Huwa najiuliza wagonjwa wasiokuwa na uwezo TZ wanawezaje kuhimili maumivu makuu kama kansa etc??
 
Mimi nadhani mfumo uliopo nchini kwa sasa ni effective.morphine itumike kwa wagonjwa wenye maumivu makali yenye usugu kwa dawa nyingine za maumivu.iwe prescribed na daktari pekee(M.D)
nadhani ni sahihi kuendelea na mfumo wa upatikanaji wa dawa hii kwenye level ya regional,referal au specialized hospitals
iwapo mtu amegundulika ana ugonjwa ulio katika stage za mwisho zinazoambatana na maumivu makali basi apewe prescription ya kudumu itakayomuwezesha kupata dawa hiyo mkoa wowote anaoishi.haya madawa ni hatari na inasemekana kifo cha michael jackson kilichangiwa na madawa makali ya maumivu.
Kuhusu bangi sidhani kama kuna ushahidi wa kisayansi unaotosheleza kuifanya bangi kama dawa ya maumivu,ila nimewahi kusikia bangi huwasaidia wazee wenye matatizo ya macho.
 
Mi nataka kutumia madawa yoyote unayotaka iwe halali, hakuna mwenye haki ya kumzuia mtu mzima kuweka kitu ndani ya mwili wake.
Kama unatumia kivyako bila kuwasumbua watu tatizo liko wapi?
Tusiache minority inayoshindwa kujicontrol na kuabuse drugs waiharibie jamii nzima.
 
morphine lazma itumike jamani,ukimkuta mgonjwa wa cancer mwenye severe pain yani haiwezekani bila morphine,mi nimeuguza mgonjwa wa cancer yale maumivu acha kabisa...
 
morphine lazma itumike jamani,ukimkuta mgonjwa wa cancer mwenye severe pain yani haiwezekani bila morphine,mi nimeuguza mgonjwa wa cancer yale maumivu acha kabisa...
mgonjwa wako alitibiwa wapi?mbona ocean road wanatoa morphine kwa wagonjwa bila vikwazo.
 
Mwaka wa 1969 nilivunjika mguu kwa ajali ya gari. Siku hizo morphine ilikuwa inatumika kwa masharti inatunzwa kwenye chumba cha DDA (dangerous drugs act) na baada ya mgonjwa kuandikiwa, manesi si chini ya wawili ndio wanaenda kutoa dozi kwenye hicho chumba kwa saini na kuandika mgonjwa husika, daktari, na kiasi cha dawa na saalia. Sijui huu utaratibu ulifutwa lini.

macinkus
 
Mwaka wa 1969 nilivunjika mguu kwa ajali ya gari. Siku hizo morphine ilikuwa inatumika kwa masharti inatunzwa kwenye chumba cha DDA (dangerous drugs act) na baada ya mgonjwa kuandikiwa, manesi si chini ya wawili ndio wanaenda kutoa dozi kwenye hicho chumba kwa saini na kuandika mgonjwa husika, daktari, na kiasi cha dawa na saalia. Sijui huu utaratibu ulifutwa lini.

macinkus

Twende mbali zaidi turuhusu haya madawa hata Pharmacy ili kuwafikia watu wengi zaidi?
 
Wakuu nimekutana na hii issue mara mbili watu waki-debate. Nikaona si vibaya nikaleta kwa great thinkers tupate mawazo na mitizamo yenu.
  1. Medical marijuana: Kuna baadhi ya states huko U.S na MExico zimeridhia watu kupanda kisha kutumia marijuana kama njia ya kupunguza aina fulani za maumivu. Kuna mama mmoja alikuwa akitoa ushuhuda kwamba bila kutumia hiyo kitu hiwa hawezi kufanya kazi yeyote productive. Amekwenda kwa treatment for more than 30 years bila mafanikio, relief aliipata alipoanza kutumia medical marijuana!
  2. Morphine: Hii ni aina ya dawa maarufu kama nusu kaputi! ambayo imekuwa ikitumiwa kwa muda mwingi wakati wa kufanya upasuaji. Muhimu kujua ni kwamba hii dawa ina uhusiano wa karibu mno na madawa maarufu ya kulevya cocaine au heroine. (nadhani yanatokana na mmea mmoja poppy..not so sure)! Katika baadhi ya nchi hii dawa hutumiwa na watu wenye maaumivu makali na endelevu, kama vile cancer isiyopona, HIV AIDS na mengeni kama hayo!
Swali ni je, kutumia dawa hizo kwa malengo haya ni sawa na ulevi wa kawaida wowote? Je ni haki kuacha watu wateseke wakati kuna uwezekanano wa kuwapunguzia maumivu? Nenda pale ocean road ukaone watu wanavyolia kwa maumivu makali, kwa nini tusiwape tuu? Is it morally justified?

Nawasilisha!
Jesuit, headline yako ni nzuri ila content umechanganya kidogo mambo.
Nianze na hoja yako ya msingi, mophine inatumika sana tuu mahospitalini na kuna wagonjwa wanakuwa prescribed bila kuambiwa ni mophine kwa vile inakuja kwenye dose tofauti na majina tofauti. Matumizi hayo mahosipitalini yanafanyiwa control under close supervision kwa vile mophine ina side effects mbili kuu.

1. Ni highly addictive, hivyo mwili ukishaizoea, hauwezi kufanya chochote bila hiyo kitu. Addiction tatizo lake ni dose kukuzoea hivyo lazima dose iongezwe kila baada ya muda ili kuendelea kuwa effective, hatimaye you can take no more na kuishia kuzimika jumla.
2. Ina slow down nervous system mpaka kufikia stage ya kuiparalyse kabisa. Hivyo matumizi yake yamekuwa restricted kwa mgonjwa ambaye imethibitishwa huyo ni mtu wa 'safari' tuu. Kwa mgonjwa mwenye chances za survival na kuishi, madaktari, wanaona bora ateseke kwa maumivu lakini hatimaye atapona kuliko kumpunguzia maumivu kwa kumuanzishia safari ya 'kimoja', 'jumla'.

Pia majeshi yote duniani kote huitumia miongoni mwa vifaa vita vyake kwa majeruhi wao likiwepo jeshi letu.

Tukija kwenye medical marijuana, nchi nyingi tuu inaruhusiwa, tena sio medical tuu, hata relaxation, au recreational. Nchini Usiwisi, kila mji umetenga eneo maalum la kujinafasi kwa starehe hizo ikiwemo uvutaji wa bangi na matumizi ya kila aina ya dawa za kulevya. Kwa jiji la Zurich, ni eneo la wazi lililoko mbele ya jengo la bunge la nchi hiyo 'The Bundes House'. Hii inasaidia hata kufanya biashara ya mihadarati sio deal nchini Uswisi, ila uhuru huo ni kwa viwango vya personal use sio kibiashara.

Hapa nchini pia matumizi ya bangi kwa viwango maalum yanaruhusiwa japo sio kisheria. Ukikutwa na msokoto mmoja tuu wa bangi, hafikishwi mahakamani, kosa ni ama kukutwa unavuta kwenye public, ama kukutwa na msokoto zaidi ya mmoja kama kiashiria cha kufanya biashara hiyo haramu.

Mimi nimesoma Tambaza, baadhi ya wanafunzi tulikuwa nao tukitinga 'summit' kupata', wako waliotoka na Div 1 kali na wako waliotoka na zero. Nakumbuka kuna lecture mmoja wa UDSM toka Jamaica, alikuwa anaipiga hiyo kitu wazi wazi, akaripotiwa polisi na kufikishwa mahakamani, akajitetea kwake ni kawaida toka nchini kwake, na kusisitiza bila kupata, lecture haipandi. Aliachiwa na kuelezwa kwa vile hapa nchini ni bangi ni marufuku, basi ajivutie nyumbani kwake privately na sio public na ndivyo wengi wanaitumia kwa nia njema wanavyofanya. Sisi kwetu Usukumani hiyo ni normal power booster ndio maana alifajiri tuu, ugali wa nguvu unapanda kama kifungua kinywa!.

Ugumu wa ku legalize marijuana ni kwa vile huwezi kutenganisha wale inaowatuma vizuri na wale inawatuma vibaya. Kungekuwa na vigezo vya nani itamtuma vizuri, nadhani ingekuwa legal kwa inaowatuma vizuri na illegal kwa inaowatuma vibaya bila kuonekana ni double standards.
 
Jesuit, headline yako ni nzuri ila content umechanganya kidogo mambo.
Nianze na hoja yako ya msingi, mophine inatumika sana tuu mahospitalini na kuna wagonjwa wanakuwa prescribed bila kuambiwa ni mophine kwa vile inakuja kwenye dose tofauti na majina tofauti. Matumizi hayo mahosipitalini yanafanyiwa control under close supervision kwa vile mophine ina side effects mbili kuu.

1. Ni highly addictive, hivyo mwili ukishaizoea, hauwezi kufanya chochote bila hiyo kitu. Addiction tatizo lake ni dose kukuzoea hivyo lazima dose iongezwe kila baada ya muda ili kuendelea kuwa effective, hatimaye you can take no more na kuishia kuzimika jumla.
2. Ina slow down nervous system mpaka kufikia stage ya kuiparalyse kabisa. Hivyo matumizi yake yamekuwa restricted kwa mgonjwa ambaye imethibitishwa huyo ni mtu wa 'safari' tuu. Kwa mgonjwa mwenye chances za survival na kuishi, madaktari, wanaona bora ateseke kwa maumivu lakini hatimaye atapona kuliko kumpunguzia maumivu kwa kumuanzishia safari ya 'kimoja', 'jumla'.

Pia majeshi yote duniani kote huitumia miongoni mwa vifaa vita vyake kwa majeruhi wao likiwepo jeshi letu.

Tukija kwenye medical marijuana, nchi nyingi tuu inaruhusiwa, tena sio medical tuu, hata relaxation, au recreational. Nchini Usiwisi, kila mji umetenga eneo maalum la kujinafasi kwa starehe hizo ikiwemo uvutaji wa bangi na matumizi ya kila aina ya dawa za kulevya. Kwa jiji la Zurich, ni eneo la wazi lililoko mbele ya jengo la bunge la nchi hiyo 'The Bundes House'. Hii inasaidia hata kufanya biashara ya mihadarati sio deal nchini Uswisi, ila uhuru huo ni kwa viwango vya personal use sio kibiashara.

Hapa nchini pia matumizi ya bangi kwa viwango maalum yanaruhusiwa japo sio kisheria. Ukikutwa na msokoto mmoja tuu wa bangi, hafikishwi mahakamani, kosa ni ama kukutwa unavuta kwenye public, ama kukutwa na msokoto zaidi ya mmoja kama kiashiria cha kufanya biashara hiyo haramu.

Mimi nimesoma Tambaza, baadhi ya wanafunzi tulikuwa nao tukitinga 'summit' kupata', wako waliotoka na Div 1 kali na wako waliotoka na zero. Nakumbuka kuna lecture mmoja wa UDSM toka Jamaica, alikuwa anaipiga hiyo kitu wazi wazi, akaripotiwa polisi na kufikishwa mahakamani, akajitetea kwake ni kawaida toka nchini kwake, na kusisitiza bila kupata, lecture haipandi. Aliachiwa na kuelezwa kwa vile hapa nchini ni bangi ni marufuku, basi ajivutie nyumbani kwake privately na sio public na ndivyo wengi wanaitumia kwa nia njema wanavyofanya. Sisi kwetu Usukumani hiyo ni normal power booster ndio maana alifajiri tuu, ugali wa nguvu unapanda kama kifungua kinywa!.

Ugumu wa ku legalize marijuana ni kwa vile huwezi kutenganisha wale inaowatuma vizuri na wale inawatuma vibaya. Kungekuwa na vigezo vya nani itamtuma vizuri, nadhani ingekuwa legal kwa inaowatuma vizuri na illegal kwa inaowatuma vibaya bila kuonekana ni double standards.

Mkuu Pasco, heshima mbele!
Kwanza nashukuru kwa kutoa mchango wa kina juu ya hoja yangu hapo juu. Nadhani inathibitisha kuwa maelezo yangu uliyaelewa vizuri kama nilivyokusudia. Tatizo halikuwa kwenye maelezo bali ni "heding". Unajua ni vigumu kustructure heading kwenye JF ikabeba yote unayokusudia kwenye maelezo.........ndio maana wakaacha nafasi ya mtu ku-elaborate hiyo thread.

Najua kuna restricted use ya hito morphine and co. huko hospitali. Ila watu wanadai " FREEDOM FROM PAIN" iwe human right! kwa nini watu wateseke na maumivu hali inaweza kudhibitiwa kwa gharama ndogo tuuuu? Kuhusu addiction, kuna aina za hizo morphine ambazo zimekuwa diluted to an extent ya kupunguza maumivu only, bila kumfanya mtu kuwa "high".
 
Ningependa kusikia michango ya watu wa dini pia...........Je ni "dhambi" kutumia haya madawa kwa namna hii?
Hivi hata kwenye dini kwa mfano wa Bangi inakataza kutumia kama kilevi (hence kuvuta) au kama mbonga au dawa hence kupika na kula? (Bangi inakuwa abused kwa kuvuta na sio kwa kuipika kama mboga..)

Na je tusinywe dawa za kikoozi sababu zinakufanya uwe kama umelewa kwa sababu za kiimani...?

Mimi nadhani watu tunazimiss interpret dini zetu
 
mgonjwa wako alitibiwa wapi?mbona ocean road wanatoa morphine kwa wagonjwa bila vikwazo.
yap alitibiwa ocean road baadae kansa ikawa imeadvance akawa yupo hme terminally ill,ofcoz tulikua tunapata morphine pale ocean road bila vikwazo,ila kuna kipindi ilituishia weekend,mbona tulikoma..mgonjwa hakulala usiku
 
Back
Top Bottom