Elections 2010 Moni ya kada na kiongozi wa CCM kutoka Kagera kuhusu Shule Za Kata

Sophist

Platinum Member
Mar 26, 2009
4,484
3,400
Majaribio ya Ajabu!

Shule za kata ni mfano halisi wa kuharibu mfumo wa elimu nchini Tanzania kwa makusudi. Kwa kawaida, hata majaribio ya matabibu wa madawa au upasuaji huanza na wanyama; vitu ambavyo siyo halisi, na baada ya kuona mafanikio kadhaa utabibu huamishiwa kwa walengwa halisi.
Inasikitisha kuona kuwa Serikali yetu imekosa hata ka chembe ka weledi. Kamwe watu weledi na makini wasingeweza kuanza majaribio ya shule za kata kwa kutumia wanafunzi halisi. Maandalizi yalitakiwa. Kuandaa walimu, majengo, vifaa na baadaye shule za kata. Sera hii imeharibu kabisa mwelekeo wa maisha ya wanafunzi na taifa kwa ujumla. Wanafunzi wamefanywa mali ghafi kwa ajili ya majaribio ya shule za kata. Je, nani atawalipa fidia? Hii ni serikali ya ajabu; inafanya majaribio kwa kutumia watu halisi badala ya vitu kifani. Aibu kwa CCM na serikali yake. Waathirika wanatakiwa kudai fidia kutoka serikalini kutokana na sera hii mbovu. Waambie Dr Silaa na wenzake walizungumzie hili jambo. Hasa katika mikutano yake ya Mikoa ya Kanda ya Ziwa.
 
Can you name this leader nimtumie gunia la congratulation? haya ni maoni ya watu walio na uchungu na nchi hii.
 
Back
Top Bottom