Mombasa Republican Council wanataka nchi yao...

Mmmhh wajue tu wanasafari ndefu sana, hvyo waandae vizazi vya kutosha kusafiri! Kudai nchi haijawahi kuwa rahisi,
serikali za kiafrika zinachochea haya mambo kwa implementation ya sera za maendeleo kiubaguzi.
Hivyo siwazi walaumu hao watu ila kama tu hizo harakati zao hazina mkono wa nje (kitu ambacho sio rahisi).

point noted.
Serikali za kiAfrika zimeyataka haya,
mfano ni jinsi mikoa ya kusini ya Tanganyika ilivyokuwa nyuma kimaendeleo pamoja na kuwa na rasilimali zote.
Mfano wa ujinga wa karibuni ni huo mradi wa bomba la gesi kutoka sijui ni Ntwara vile, mpaka Dar es salaam, kwanini power plant isijengwe kule, halafu umeme ukaingizwa mu-gridi ya taifa.
Ujinga tu!
 
let them go ask the north east what happened to them when they demanded to seperate themselves from kenya. kenya will not seperate. we will do what it takes inluding soldiers guns and bombs to supress any attempts by anyone to secede a part of kenya from kenya. the shifta war should serve as a warning/reminder to any secessionist movements.

however, the MRC has legitimate concerns that NEED to be adressed, the kenyan govt cannot dismiss their grievances. it is their constitutional right to assemble and to say whatever the heck they want to say and that right should be respected and protected. i will support their right to assemble and have free speech

umesomeka GT!
 
Kimsingi mipaka aliweka mkoloni, sasa kuna taabu gani na sisi tukiweka yetu ambayo tunadhani itakua na manufaa kwetu?

hili nalo neno.
Moja ya athari za mipaka ya ukoloni ni kuyatenga makabila,
mfano Wamasai katika Kenya na Tanganyika, na Waluo katika Kenya na Uganda, bila kusahau Wasotho katika SA na Lesotho...
Tuweke ya kwetu bwana...
 
Huo ni urithi aliouacha mwarabu ktk pwani yote ya africa mashariki hadi kusini, wakati wakoloni wenzao walikuwa wanajenga makanisa kwa ajili ya kuwafundisha watu kwenda mbele za mungu kwa hofu,shule kwa ajili ya kupata makarani na wasaidizi kwenye utawala wao na mahospitali kwa ajili ya afya za watu wao wa kuwatumikia hao vipofu waliendelea kuwafundisha waswahili kuvaa kanzu ya kutofanya kazi ila biashara zisizo na tija ( zisizolipia ) matokeo yake ndiyo hayo.
 
Huo ni urithi aliouacha mwarabu ktk pwani yote ya africa mashariki hadi kusini, wakati wakoloni wenzao walikuwa wanajenga makanisa kwa ajili ya kuwafundisha watu kwenda mbele za mungu kwa hofu,shule kwa ajili ya kupata makarani na wasaidizi kwenye utawala wao na mahospitali kwa ajili ya afya za watu wao wa kuwatumikia hao vipofu waliendelea kuwafundisha waswahili kuvaa kanzu ya kutofanya kazi ila biashara zisizo na tija ( zisizolipia ) matokeo yake ndiyo hayo.

hiyo elimu tulopewa na hao wazungu imetusaidia nini??
naona bado tunazidi kudidimia kwenye umasikini, bora ya hao waarabu hawafi na njaa
 
Huo ni urithi aliouacha mwarabu ktk pwani yote ya africa mashariki hadi kusini, wakati wakoloni wenzao walikuwa wanajenga makanisa kwa ajili ya kuwafundisha watu kwenda mbele za mungu kwa hofu,shule kwa ajili ya kupata makarani na wasaidizi kwenye utawala wao na mahospitali kwa ajili ya afya za watu wao wa kuwatumikia hao vipofu waliendelea kuwafundisha waswahili kuvaa kanzu ya kutofanya kazi ila biashara zisizo na tija ( zisizolipia ) matokeo yake ndiyo hayo.

maybe.
Lakini usiwe biased, take your time upitie malalamiko yao, then ndio uhitimishe.
 
Mimi hua najiuliza swali moja. kwanini MRC watake kujivuta kando na kutaka nchi yao? Na nikiangalia kwa undani, sipati jibu kamili. maana kama ni kutaka kujikimu kimaendeleo, sioni wakitoboa. Ombi hilo la kutaka kujivuta msingi wake ni wa kidini na sio ya kujali maslahi ya wadigo au wagiriama ambao shida zao za kawa sote tunazielewa. Hivi miaka tatu iliyopita 2008, rais wa Iran amedinajad alizuru mombasa, huenda ikawa mvuto ambao kundi haramu la MRC unao inachochewa na ziara hiyo.
 
Mimi hua najiuliza swali moja. kwanini MRC watake kujivuta kando na kutaka nchi yao? Na nikiangalia kwa undani, sipati jibu kamili. maana kama ni kutaka kujikimu kimaendeleo, sioni wakitoboa. Ombi hilo la kutaka kujivuta msingi wake ni wa kidini na sio ya kujali maslahi ya wadigo au wagiriama ambao shida zao za kawa sote tunazielewa. Hivi miaka tatu iliyopita 2008, rais wa Iran amedinajad alizuru mombasa, huenda ikawa mvuto ambao kundi haramu la MRC unao inachochewa na ziara hiyo.

wewe ndio ulietia udini kwenye comment yako.
Kumbuka kuwa mkoa wa Pwani hauishii tu ufukweni kwa waswahili, unasogea mpaka miteremko ya Ml. Kilimanjaro sehemu za Voi na Taveta, na kule kaskazini unaenda mpaka Garsen, na kwenye mpaka wa Pwani na North East, jirani kabisa na mji wa Garissa, na wakazi wa huko kote, ambao sio waislamu, wanashiriki harakati hizi.
Huo udini unatoka'pi?
Kwa hiyo we have to trace back tujue ni nani mwenye alitembelea Mombasa recent years? Nadhani Ahmadinejad alikuja kwa ziara ya kirais, na sio kijasusi. Inashangaza kuona unamtuhumu rais wa jamhuri kwa tatizo kama lile, ingekuwa yeye ndio muasisi wa chokochoko hizo wala asingehitaji kuja binafsi, angetuma tu agents.
Sawasawa?
 
kama hiyo ndio hoja kua kwa vile rasilimali nyingi ziko kwao ndio wanendelee kuliko wote mbona hapa tanzania wasukuma ni maskini wakat utajiri wa madini uko kwao tena kwenye ardhi wanayoishi na cjackia msukuma akidai wajitenge ili waendelee! ni small minded people tu hawana lolote!
 
kama hiyo ndio hoja kua kwa vile rasilimali nyingi ziko kwao ndio wanendelee kuliko wote mbona hapa tanzania wasukuma ni maskini wakat utajiri wa madini uko kwao tena kwenye ardhi wanayoishi na cjackia msukuma akidai wajitenge ili waendelee! ni small minded people tu hawana lolote!

labda pengine walikuwa wameshadai kwanza kutambulika ikashindikana,
who knows?
Viongozi wa Kiafrika hawana muamana ati...
 
Sultani at work, working hard to bring back his Influence over fomer colonies. Lets see mwishowe utakuwaje?
 
Sultani at work, working hard to bring back his Influence over fomer colonies. Lets see mwishowe utakuwaje?

do you reckon that Zanzibar will be that proclaiming Sultan's next step after Indian shores of Kenya?
 
Wanachogombania ni kile kile ambacho binadamu yeyote mpenda haki anakihitaji.Yawezekana maana halisi ikapotoshwa kwa sababu mbali mbali jazba na upeo wa kujenga na kusimamia hoja.Upole wao na ukarimu wao ndio umewaponza wakamezwa.
 
acha pumba mkuu.
Na serikali yetu inavyotembeza bakuli nayo imeathiriwa na Waarabu?
Na mbona nchi za Kiarabu ndio zenye maendeleo hapa Afrika?
Unaweza linganisha Tanganyika yako na Misri, Libya, Tunisié au Maróc?
Take your time to think berore posting,
anyways, refer the heading above.
 
Wanachogombania ni kile kile ambacho binadamu yeyote mpenda haki anakihitaji.Yawezekana maana halisi ikapotoshwa kwa sababu mbali mbali jazba na upeo wa kujenga na kusimamia hoja.Upole wao na ukarimu wao ndio umewaponza wakamezwa.

wewe umesema la maana.
Kuna watu wanatumia peripherals kukwepa hoja msingi. Kama alivyofanya Pinda v/s Dkt. Ulimboka (MD)...
Unadhani MRC watafanikiwa kwenye move yao? Na nini mchango wa mataifa yenye ushawishi katika kufanikisha azma yao?
 
Nimefuatilia harakati za hawa jamaa kwa muda mrefu, pamoja na mkwara mzito wa serikali ya Kenya kulipiga marufuku kundi hili na kuliita 'kundi haramu',
bado jamaa hawarudi nyuma. Bado wanasisitiza kuwa Pwani ya Kenya si sehemu ya taifa la kenya.
Pamoja na viongozi wao kufikishwa mahakamani kwa makkosa ya uhaini, jamaa hawaja-give up.
Moja ya madai yao ni kukithiri kwa umasikini katika maeneo ya Pwani wakati kuna rasilimali za kutosha.
Sasa hivi harakati zao zimehamia mtandaoni.


Profile Pictures | Facebook

Mwanzo ngoma ni lele!
 
Back
Top Bottom