Captain Phillip
JF-Expert Member
- Nov 5, 2010
- 894
- 536
Akizungumza katika mahojiano na Radio Safari ya mjini Mtwara hivi karibuni Nape amesema serikali ya Rais Jakaya Kikwete ndiyo pekee katika nchi hii iliyokwisha kutoa maamuzi magumu kuliko serikali zote zilizopita.
Nape amenukuliwa akisema...." uamuzi mgumu wa kwanza uliotolewa na serikali ya awamu ya nne ni kwa yeye Lowassa kulazimishwa kujiuzulu, kuvunjwa Baraza la Mawaziri, kuwafungulia kesi kina Mramba na Yona, kuivunja kamati kuu ya CCM na sekretarieti, Ujenzi wa chuo kikuu cha Dodoma na Ujenzi wa shule za kata".
Ufisadi unalipi naona Nape kanenepeana ile mbaya kwa siku chache tuu toka aingie kwenye uongozi wa Magamba