hapo kwenye red serikali itapata wakati mgumu sana ndani ya muda mfupi na si serikali tu bali wananchi haswa maskini walala hoiSerikali ilishasema (JK) kwamba hawana kitu cha kuongea na madaktari, kama daktari haridhiki na achomoe aende atakako. Na kweli wengi sana wameenda nje kuhudumiwa mara saba ya hapa, wanawacheka waliobaki. Hao waliobaki ni kwa sababu hawataki kwenda nje ili waionyeshe serikali kwamba Tanzania sio ya wanasiasa tu, ni yetu sote. Halafu kumbuka Kayaanza mizengwe pita pinda kwamba liwalo na liwe na likawa. Madaktari wamezibwa midomo na kila atakayeongea analimbokiwa. Wote twataka kuishi, hakuna daktari mjinga wa kujining'iniza kamba shingoni wakati watu kibao wanamtegemea, na watoto wao huzaliwa uzeeni sababu miaka mingi wako shule. Waandishi umeona nao wakiisema serikali kwamba inatupeleka ndiko siko wanawadaudi. Kwa hiyo mambo kimyakimya, wananchi waendelee kuishabikia serikali yao maana imeona kwamba ndo inalipa.