Mohamed Said ni Shujaa wa wakati huu

anaalikwa sana oxford,baadhi ya vitabu vyake vinatumika vya lugha ya kiingereza.Acha kuropoka kama hujui uliza ndio dogma
Atakua anaalikwa kutoa mihadhara vyuo vya uarabuni bila shaka huyu,......lakn ni poa_maake mihadhara yote ni poa,iwe ya elimu dunia ama ilmu akhera.

hongera yake.
 
anaalikwa sana oxford,baadhi ya vitabu vyake vinatumika vya lugha ya kiingereza.Acha kuropoka kama hujui uliza ndio dogma

Kama ni vya lugha ya kiingereza_basi namkubali mkuu,.............My bad,i take it back!..na sintarudia tena kuropoka.
 
Taifa linasherekea miaka 50 ya uhuru wengine wana chuo kimoja tu tena cha kupewa na Mr Clean! Mwambieni huyo mtu wenu akafuge majini na kufundisha madrassa.

Ndugu yangu mnyisanzu acha chuki zako dhidi ya Uislam.Chochotw kihusucho Uislam kikiletwa hapa JF kinapingwa kwa kejeli na matusi.Kwa hakika Wakristu wengi huwaona Waislam kama mzuka flani hivi mataahira.Lkn jee vyuo vyenu vikuu ambavyo vimejengwa kwa kodi za Waislam haviwaelimishi muache KUFIKIRISHWA?Haviwapi nafasi japo kidogo ya kufikiri wenyewe na kuuona ukweli ambao historia imeurekodi juu historia ya Tanganyika Yetu.Dharau na matusi yenu kwetu ni dhihirisho la upeo wa juhudi kubwa alizozifanya "Mtakatifu Mtarajiwa" JKN kuwapa nguvu kisiasa,kijamii na kiuchumi,ndio maana shukrani za Kanisa kwake ni kumfanya "Mtakatifu"SOMA kitabu :Kanisa Katoliki na Siasa za Tanzania Bara, 1961-1984.Anapotokea mtu anaejua akawaeleza wenzake ukweli kuhusu Tanganyika basi huyo ataitwa mdini wakati mdini hasa anajulikana.Unapotuambia tumwambie mtu wetu akafuge majini,basi tuambie akina Joe Davie wa "Ngurumo ya Upako" tumwambie afuge nini?Na Mnyisanzu nae ni Greet Thinker.Tusizibane midomo.Mwnyezi Mungu ni Mjuzi Zaidi
 
Hili ndilo ninaloliona kila kona katika nchi yetu watu wanaukimbia ukweli, wanauogopa, unawasuta, unawachoma miyo yao kwa sababu wameamua kuishi katika uongo. Imeandikwa kuwa kweli itakuweka huru siku zote, lakini sisi tumeamua kujiweka katika uongo. Matokeo ya maisha yetu na hali ilivyo leo ni sababu ya unafiki na uongo, oungo na unafiki ndio imekuwa tabia yetu, watu wazima wanaopaswa kujiheshimu wanatamka uongo hadharani hali wakijua huo ni uongo. Waziri mkuu anasema hivi, Rais anasema hivi, ni wazi mmoja wapo ni muongo na anaongopa bila kujali kitu kwa vile anajua anaishi katika jamii iliyolelewa katika uongo, imefanya uongo sehemu ya maisha yao na kila wanapotaka kufanya lolote lile wanatoa sababu za uongo ambazo hizo ndizo zinazokubalika. Msema kweli anachukiwa na kupingwa, anatukanwa na kusakamwa, watu wanataka uongo tu, uongo ndio unaowapa faraja, ukweli unawanyima usingizi, wengine wanadiriki hata kuwashawishi wengine wasishiriki katika mijadala inayotafuta ukweli kwani hawautaki kuusikia ukweli wala hawataki wengine waujue ukweli. Tusizungumzie udini, tusitaje imani tuseme tu mambo ambayo viongozi wetu wametudanganya, tuyaoredheshe na pia tujiangalie tumefanya nini katika kushughulikia uongo wao halafu pia tujiangalie tumefanya nini katika kumshughulikia Mohamed Said na "uongo" wake halafu tupime tumetumia nguvu nyingi wapi.

Nchi ya Wapenda uongo,Wadanganyika.Ewe Mwenyezi Mungu,tupe nguvu tuupige vita uongo na kuusimamisha Ukweli.
 
Hatuwezi kamwe kumuacha aendelee kupanda mbegu na chuki zake za kideen....

Hebu watuambie ana ushujaa gani?

rejea ushauri wa Pasco hapo juu.
Mwamedi Saidi ni bonge moja la mwandishi,
nachelea kumfananisha na Kwame Nkrumah...
Huyu inafaa tumpe nchi, ana maono sana!
 
Back
Top Bottom