MOH kusomesha mtoto wa mkubwa UK ni uungwana?

Tatizo sio salama kama salama ila nafasi aliyo nayo mzazi wake! Hivi uilshawahi kujiuliza kwa nini coca-cola bottlers au pepsi wakiwa na promotion wanatoa note kuwa wafanyakazi na familia zao hawaruhusiwa kushiriki?! Na hata wakishiriki, hawatapewa zawadi pindi tu status yao itakapojulikana?!

Its a matter of common sense (ethics), integrity and understanding what conflict of interest means!
(Mambo ambayo wengi wetu tulishayazika)!

Asante Mkuu kwa mchango huu, the problem here is ethics and conflict of interests! Hakuna lingine lingesababisha upuuzi kama huu kutokea. Kuna mtu anangoja cheo baada ya hilo!
Kwanza kama nchi yetu ingekuwa inaongozwa na viongozi wenye busara na wazalendo wa kweli ingukuwa marufuku kwa mtoto wa kiongozi yeyote kwenda kusoma nje! Kuruhusu hilo ndio sababu ya wao kusahau kuboresha elimu hapa nchini. Tena ingetakiwa hata mfanya biashara anayempeleka mwanaye nje wakati elimu hiyo inapatikana nchini awe anatozwa kodi ya ziada!

Waliosema kuna viongozi wameifanya nchi kuwa shamba la bibi, hawajakosea hata kidogo.
haaaa! Inasikitisha kuona viongozi waroho namna hii madarakani. Inakuwa kama tunaongozwa na genge la wacheza kamari!
 
Na mie Mkweche na nena!
Dr.Salama aende Kusoma manake nae ni Mtumishi wa Umma na Anatakiwa asimame kama yeye!Kuwa mtoto wa Raisi ndio hata ukiwa na Kazi Ukaombe ada kwa Baba! Haikubaliki
Cha msingi ni busara itumike na watendaji wa wizara, wale vijana walioomba nafasi ya Kozi kama yake hapa hapa nyumbani ni muhimi nao wapewe udhamini wakasome kwani wote wanaenda kutumikia watanzania walewale!
Kama Fungu lake la kwenda UK litatosha kuwasomesha wote hapahapa Nchini ingekuwa Busara, la kama ni lazima akapate maarifa Ughaibuni na hawa kusoma nyumbani waende!
Mie Mkweche nilisomaga Masters Bongo(si ya fani za Afya) kwa Kujilipia huku wanangu sota ile mbaya!
Sijawahi kuota kwenda Ulaya manake sijui hata nafasi zinapatikanaje!Napenda PhD siku moja
Niitwe Dr Mkweche
 
Olecranon, nakuomba usiingie kwenye long list ya 'hate preachers' wa humu jamvini.
Kila Mtanzania kwanza ni Mtanzania ndipo mengine yote yanafuati ni jinsia gani, ni kabila gani, ni familia gani, ameolewa na nani etc. Kuwa mtoto wa rais, hakumuondolei haki yake kama Mtanzania mwingine yoyote.

Bahati nzuri au mbaya, nimetokea kumfahamu huyu binti, Dr. Salama na pia nawafahamu baadhi ya watoto wengine wa JK japo sio wote nane, kwa opinion yangu, kati ya watoto wote wa JK ninaowafahamu mimi, Dr. Salama pekee ndie anaesimama mwenyewe kama Salama bila ile pride ya mtoto wa rais ambayo nduguze wanayo!. She is so humble na down to earth, fortunately kaolewa na kijana mwenye uwezo kumlipia shule popote, lakini huko hakumuondolei right yake ya kupata fellowship kama rai mwingine yoyote. Hata kama unatoka familia ya mamilioneo, kupata fellowship kunakuongezea heshima kwa sababu ili kuipata lazima uishindanie na wengine toka nchi mbalimbali duniani. Wizara sio determinant nani anapata, sponsors ndio determinant, japo recomendation ya wizara pia inanguvu.

Kama huyo dr ana sifa, na ameomba kama Mtanzania mwingine yoyote, sasa ndio anyimwe eti kwa sababu ni mtoto wa rais?.

Wanabodi, tuendelee kumsakama JK kwa maroroso yake, ya chama cheke na serikali yake, au tuwasakame watoto wake wanaofanya wanayoyafanya simply kwa sababu baba ni rais, lakini nawaomba sana tusiisakame familia ya rais kwa mambo yasiyohusika, hiyo scholarship ni issue ya proffesionalism hata kama preferential ime play part lakini she deserves and she is capable!

Please leave her alone!.

Acha kutema pumba wewe,hyo sponshp kpwa kwa kua ni mtoto wa rais,kama jamaa yake ana hela y asimsomeshe? Watz ni wabinafsi sana ndo maana hatuendelei,what sponsorship is? Navyojua mimi mtu anatafuta sponsor kwa kua hana uwezo wa kujisomesha sasa iweje yeye hazuie watoto wa wakulima yl fedha ya kujizamini anayo? Watanzania sisi ni wabinafsi tunakunywa hadi uji wa mgonjwa?? Plz usitetee ujinga wa watoto wa mafisadi.
 
Nadhani hujaelewa vizuri anachojaribu kukisema mtoa mada hapa,,issue hapa sio kupata chuo UK,canada au USA,.suala la msingi ni wangapi ambao waliapply na wanastahili lakini wakanyimwa na badala yake kupewa hawa wasio na shida kabisa!?!

Usiwatetee hawa sababu hata mimi yaliwahi kunikuta,..nilipomaliza form six mwaka 2005 tuliapply scholarship za telecom&electronics za china pale wizara ya elimu ya juu.,.wametoa majina ya waliopata including waliokuwa na division III wakituacha sisi wenye div I,..na kulikuwa hakuna mwenye admission wala mean testing iliyokuwa imefanyika kujua hali zetu za kiuchumi,.rushwa tu.

Mkuu acha tu nimeapply za china,algeria,Russia mwaka 2003 pale Tirdo acha tu,kuna kanjanja alipata olevo div3 na alevo div 2 ya kumi alipata wakati mie olv nina 8 na alvo 3 acha tu
 
jamani muda mwingine tusiwe tunalalamika sana, hawa kwanza wengi ni waajiriwa chini ya hii wizara, halafu kama watu hawana admision za huko UK basi wawape tu scholarship? tuwe tunajishughulisha jamani , mbona yupo mmoja amepata toronto , canada hujamwongelea? Hata mimi mara ya kwanza nilikuwa na mentality kama yako kuwa aaaah ni watoto wa vigogo tu wanapata , siyo kweli niliwahi kujaribu na mimi nikapata tena UK. Tatizo ni kupata admision UK ndiyo tatizo , by the way masters yenyewe hapa UK ni mwaka mmoja tu.

Wengi ya hawa wanafunzi wanafamilia tayari hivyo muda mwingine kwenda mbali sana inawawia vigumu.

Acha kufanya conclusion ya juu juu wewe.? There is a problme here.
 
Raisi ni maskini hana hela kwa nini tusimsomeshee mwanae tena UK? umaskini alionao hana uwezo wa kumlipia ada bintie!!!!!!!!Ajabu, this country bwana????????!!!!!!!!!!
 
Nadhani huna taarifa za kutosha , ni hivi home tution fee hapa UK ni kama poundi 3000 (kama million 7.5 za kibongo) na internationals ni poundi 10,000 inachofanya wizara ni kulipa home tution fee na inayozidi unajilipia mwenyewe . pale IMTU watu siwanalipa tution fee million 7? kuna tofauti gani mnayosema? mumewe anazo sasa kwa nini asimuongezee hizo poundi 7000 za juu? by the way kwa hiyo kozi tuition fee siyo gharama kama unavyosema unless angekuwa anasoma PhD ningekubali.


Acheni kuwwadanganya watu bwana huwezi kusomesha watu 200 kwa tuition fee ya mtu mmoja UK. Mathalani kama analipa tution fee ya poundi 10,000 kwa mwaka ni sawa na millioni kama 25 za kibongo na kama mtu anasoma pale chuo cha IMTU ambacho ni milioni 7 kwa mwaka , mbona inasomesha watu watatu (3) tu? hivi hesabu ndogo tu jamani zinawashinda? masters UK ni mwaka mmoja tu huku bongo ni miwili kwa mantiki hiyo aliyopo bongo atatumia millioni 14 hali wa UK millioni 25.

ungesoma toka mwanzo usingechangia upuuzi kama huu.
 
Olecranon, nakuomba usiingie kwenye long list ya 'hate preachers' wa humu jamvini.
Kila Mtanzania kwanza ni Mtanzania ndipo mengine yote yanafuati ni jinsia gani, ni kabila gani, ni familia gani, ameolewa na nani etc. Kuwa mtoto wa rais, hakumuondolei haki yake kama Mtanzania mwingine yoyote.

Bahati nzuri au mbaya, nimetokea kumfahamu huyu binti, Dr. Salama na pia nawafahamu baadhi ya watoto wengine wa JK japo sio wote nane, kwa opinion yangu, kati ya watoto wote wa JK ninaowafahamu mimi, Dr. Salama pekee ndie anaesimama mwenyewe kama Salama bila ile pride ya mtoto wa rais ambayo nduguze wanayo!. She is so humble na down to earth, fortunately kaolewa na kijana mwenye uwezo kumlipia shule popote, lakini huko hakumuondolei right yake ya kupata fellowship kama rai mwingine yoyote. Hata kama unatoka familia ya mamilioneo, kupata fellowship kunakuongezea heshima kwa sababu ili kuipata lazima uishindanie na wengine toka nchi mbalimbali duniani. Wizara sio determinant nani anapata, sponsors ndio determinant, japo recomendation ya wizara pia inanguvu.

Kama huyo dr ana sifa, na ameomba kama Mtanzania mwingine yoyote, sasa ndio anyimwe eti kwa sababu ni mtoto wa rais?.

Wanabodi, tuendelee kumsakama JK kwa maroroso yake, ya chama cheke na serikali yake, au tuwasakame watoto wake wanaofanya wanayoyafanya simply kwa sababu baba ni rais, lakini nawaomba sana tusiisakame familia ya rais kwa mambo yasiyohusika, hiyo scholarship ni issue ya proffesionalism hata kama preferential ime play part lakini she deserves and she is capable!

Please leave her alone!.

Hii issue haina hate preachers.
Ngoja tubadilishe scenario, amepewa scholarship mtoto wa mwenye uwezo, ambaye baba yake anaweza kumsomesha . Mtoto wake huyo siyo Dr. Salama, na baba yake si Kikwete. Je ni haki kwa Watanzania wasioweza kujilipia?

Watu hawamchukii Dr. Salama kama unavyotaka kunyambulisha, wala watu hawa hawabishii ustaarabu wake na wema wake. Lakini baba yake hana uwezo wa kumlipia? Kwa nini sisi tumlipie?
 
Ningekuwa JK ningewawajibisha waliompa binti yangu sponsor na kumweka kwenye hii list. Je wangempa hiyo sponsor na kuliweka kapuni jina lake likabaki kwenye makabrasha ya wizara si wangekuwa wamemvika nguo rais wetu kuliko sasa ambapo anaonekana hana huruma kwa watanzania? Hili ndo tatizo la viongozi wasiojua kusoma alama za nyakati!!!!
Ukiangalia list ya wanaoenda kusoma ni wengi sana na hata Salama Kikwete kuwemo si tatizo. Tatizo linakuja pale walipotoa nafasi moja ya UK na kumuweka mtoto wa Rais. Huu ni upuuzi na kujipendekeza kulikofanywa na watoa maamuzi wa Wizara. Japo hakuna justfication ya ubadhirifu ila ni dhahiri UNDUE INFLUENCE imetumika hapo na ni ktu kibaya sana. JK ana uwezo wa kumsomesha mtoto wake popote pale kwa kipato chake halali.

Kama watoa maamuzi wa Wizara wangekuwa na open mind wangetoa angalau nafasi tano na kumjumuisha huyo Salama. OTHERWISE THIS IS CLEAR PREFERENTIAL TREATMENT. Ningekuwa mshauri wa JK ningekataa Salama kwenda UK peke yake. Hii ina undermine my presidency. Sihitaji preferential treatment toka kwa mtu yeyote yule.

Ndiyo maana akina Madaraka Nyerere na Makongoro walikuwa wanachanganywa na nawatanzania wengine kuondoa dhana ya mtoto wa rais. Kwa hili MOH wamechemka period kwa kuonesha upendeleo wa wazi, na wanahitaji kumuomba radhi JK kwenye hili.
 
tujikumbushe kidogo juu ya hili jamani kha!


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
Ndugu yangu kuna sina nyingi za scholarships. Kuna scholarships ambazo ni merit based, hizo haziangalii uwezo wa mwanafunzi kipesa bali uwezo wake kimasomo. Kwa maana hiyo kuwa masikini hakukupi sifa ya kipesa scholarship hii na kuwa tajiri hakukuondolei sifa za kupata scholarship.

Aina nyingine ya scholarship ndiyo inaangalia uwezo wa mtu kujilipia. Scholarships hizi huangalia financial background ya mtu. Kwenye hizi uwezo wa kimasomo siyo kigezo kikuu japo mtu anatakiwa awe na uwezo kiasi Fulani kimasomo.
Kwa hiyo siyo kwamba namtetea au kumpinga mtu bali kabla hatuja lalamika ni lazima kwanza tujue sifa zinazo tumika kutoa scholarship fulani na je waliopewa wametimiza hizo sifa? Kama scholarship ni merit based na inaangalia tu uwezo wa mtu siyo sahihi kulalamika mtu fulani kapewa scholarship kisa tu jina lake la mwisho.

Kwa hiyo mkuu naomba uainishe vigezo vinavyo tumiwa na wizara ya afya kuwalipia hao wanafunzi na to a ushahidi kwamba hiyo Salama Kikwete hajatimiza vigezo hivyo. Pia tusisahau kwamba kuwa na jina la mwisho kubwa haimaanishi na wewe una uwezo wa kipesa. Mtu anaweza akawa na ndugu mwenyewe uwezo lakini kwao wasiwe na uwezo. Je mtu anyimwe fursa kwa sababu tu mjomba au baba mdogo ana uwezo?
 
Jamani binafsi sioni kosa la huyu binti Kikwete bali naliona kosa kwa planning officers wetu. Niko tayari kusahihishwa ila sidhani kweli kama hazina chombo kinachoratibu matumizi ya fedha zote za umma katika nchi hii planning officers wao wanawajibika ipasavyo.

sioni mahali ambapo wana plan for future ya watanzania, ama pia wanaplan Vs available resources.Nafikir qualities za hawa planning officers zinapaswa kuwa za watu wanaoweza kufikiri juu ya matumizi kidogo ya pesa katika kuzalisha zaid. Yaani ni kama vile mtu unaduka unakuta kuliendesha duka unatumia almost 90% ya daily income so wewe faida inabaki kuwa 10% ama pengine usipate kabisa.

may be binti Jakaya alitafuta chuo akapata akaleta maombi wizarani kama mwanafunzi mwingine yeyote lkn je ilipokwenda hazina waliyafikiria haya as tanzanians
- je akienda huyu atarudi kuja kulitumikia taifa hili ama atatokomea kama wengine?
-je kwa gharama hizi ningeweza somesha wangapi hapa Tz kwa fani hii?
-je nafasi hii ameiomba just kwasababu hapa tz hakuna vyuo vitoavyo elimu hii ama ni kwasababu anataka kusoma Uk kama wengine?
-je kumsomesha huyu mmoja na kwa bahati mbaya akifa inamaana nguvu zetu zote ndio zimeishia hapa? manake kama tukisomesha weng akifa mmoja wengine watabaki.(simuombei kifo but ni mawazo )
-je as a competent candidate plus statusqo yake angeweza pata hii scholarship kwa other sponsors ambazo kwa watanzania wa kawaida ni ngumu ili fedha hizi zitumiwe na wengine. so wangefikiria possibility ya kumtafutia sponsor mwingine ambaye ni huru kabisa.

huu ni mtazamo wangu ila bibie kama wamekupa nenda, huu ni uvivu wa watanzania wachache wa kufikiri so huna kosa kabisa na Mungu akutangulie
 
Ndugu wana JF,
Ninajua kuna maswala mengi ambayo yako mbele yetu kwa ajili ya kuyajadili na kutafutia ufumbuzi. Lakini nimesikitishwa sana na list ambayo nimeona kwenye website ya wizara ya afya inayoonyoshe majina ya postgraduate students ambao watakuwa sponsored na wizara ya afya. List yenyewe ni hii hapa http://www.moh.go.tz/POSTGRADUATE-TO-BE-SPONSORED.pdf. Kilichonifanya niweke thread hii hapa ni kuwa Wizara imeamua kusomesha mtoto mmoja wa mkubwa UK ambaye kwa jina anajulikana SALAMA KIKWETE. Cha kusikitisha zaidi ukiangalia hitimisho la list hii kuna usemi huu: THOSE CANDIDATES WHO APPLIED FOR SPONSORSHIP FROM THE MINISTRY OF HEALTH AND SOCIAL WELFARE AND DO NOT APPEAR IN THIS LIST SHOULD CONSIDER THEMSELVES UNSUCCESSFUL .
Je, ni wanafunzi wangapi zaidi wangesomeshwa hapa bongo kwa pesa hii itakayoyumika kusomesha huyu mtoto mmoja wa kigogo?
Je, ni wanafunzi wangapi walipewa opportunity ku-compete na huyu mtoto wa kigogo kwa hii nafasi ya kusoma UK?
Je, hatuna pediatric dentistry educators hapa bongo?

Kama uliapply for sponsorship ukakosa na upo humu jamvini ni vizuri ukatujulisha ili tupate a true picture ya madakitari ambao hawakuweza kujiunga postgraduate kwa kukosa sponsor.


Wengine tumesoma hiyo list hatujui ni nani Mtoto wa Kigogo; Ungetusaidia

kuyataja hayo Majina wengine hatuishi Bongo, Vigogo wengi hatuwajui samahani

sana....
 
Olecranon, nakuomba usiingie kwenye long list ya 'hate preachers' wa humu jamvini.
Kila Mtanzania kwanza ni Mtanzania ndipo mengine yote yanafuati ni jinsia gani, ni kabila gani, ni familia gani, ameolewa na nani etc. Kuwa mtoto wa rais, hakumuondolei haki yake kama Mtanzania mwingine yoyote.

Bahati nzuri au mbaya, nimetokea kumfahamu huyu binti, Dr. Salama na pia nawafahamu baadhi ya watoto wengine wa JK japo sio wote nane, kwa opinion yangu, kati ya watoto wote wa JK ninaowafahamu mimi, Dr. Salama pekee ndie anaesimama mwenyewe kama Salama bila ile pride ya mtoto wa rais ambayo nduguze wanayo!. She is so humble na down to earth, fortunately kaolewa na kijana mwenye uwezo kumlipia shule popote, lakini huko hakumuondolei right yake ya kupata fellowship kama rai mwingine yoyote. Hata kama unatoka familia ya mamilioneo, kupata fellowship kunakuongezea heshima kwa sababu ili kuipata lazima uishindanie na wengine toka nchi mbalimbali duniani. Wizara sio determinant nani anapata, sponsors ndio determinant, japo recomendation ya wizara pia inanguvu.

Kama huyo dr ana sifa, na ameomba kama Mtanzania mwingine yoyote, sasa ndio anyimwe eti kwa sababu ni mtoto wa rais?.

Wanabodi, tuendelee kumsakama JK kwa maroroso yake, ya chama cheke na serikali yake, au tuwasakame watoto wake wanaofanya wanayoyafanya simply kwa sababu baba ni rais, lakini nawaomba sana tusiisakame familia ya rais kwa mambo yasiyohusika, hiyo scholarship ni issue ya proffesionalism hata kama preferential ime play part lakini she deserves and she is capable!

Please leave her alone!.

Pasco
Kama kawaida yako umetetea tena ujinga, kwa maneno uliyoandika hapa nakuambia kabisa nimekutukana tusi baya sana... naomba ni report nipewe ban!!!
:mad:
 
Pasco
Kama kawaida yako umetetea tena ujinga, kwa maneno uliyoandika hapa nakuambia kabisa nimekutukana tusi baya sana... naomba ni report nipewe ban!!!
:mad:
Kiraka, nimekuripoti na ban yako iko njiani inakuja na itakuwa imposed mode akishalisoma hilo "tusi baya sana..."
 
Back
Top Bottom