nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Nape Nnauye not all business people who joined the politics are gready; there are some good business people whom because of Azimio la Arusha and Tanzanian Style of Socialism, they are more dedicated to our people more than heavy ranking CCM leaders whom love to drive around and abuse the population...
Na Hillary Shoo, Singida.
Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini Mohammed Dewji (MO) amewashangaza walimu wa shule za Msingi Manispaa ya Singida pale alipowapa posho ya shilingi 50,000 kila mmoja wakati wa hafla fupi ya kuzungumzia changamoto zinazowakabili walimu hao.
Ndugu zangu walimu kwa kuwa leo hii nimefurahi kukutana nanyi hapa na kuzungumzia changamoto zinazowakabili katika kutekeleza kazi zenu za kila siku posho ya leo kila mwalimu atapata shilingi 50,000 . alisema MO na kusababisha ukumbi mzima kulipuka kwa nderemo na vifijo.
Akizungumza mwishoni mwa wiki na walimu hao kwenye ukumbi wa chuo kipya cha ualimu Misuna Dewji aliwashukuru walimu kwa kukichagua chama cha CCM na kukipa ridhaa ya kuongoza nchi.
Aidha alisema heshima waliyompa pamoja na wananchi wa jimbo hilo anaienzi na kuithamini kwa moyo wake wote kwani anatambua umuhimu wao katika jimbo hilo Nani kama mwalimu, walimu waliitikia hakuna.
Mapema Kaimu Ofisa Elimu wa Manispaa ya Singida Ramadhan Labito alimweleza Mbunge kuwa walimu wanakabiliwa na changamoto nyingi ikwemo ukosefu wa madawati na uchakavu wa vyumba vya madarasa katika shule nyingi za msingi.
Labito alitaja changamoto nyingine kuwa ni ukosefu wa nyumba za walimu maeneo ya vijijini, kukopeshwa vyombo vya usafiri, kupatiwa viwanje vyenye hati, kupatiwa mikopo mbalimbali yenye masharti nafuu, kuimarishwa kwa vituo vya kulelea watoto yatima kititimo na Kompyuta mashuleni.
Zingine kwa mujibu wa Kaimu Ofisa elimu Labito ni kuchimbiwa visima vidogo mashuleni ili upatikanaji wa maji kwa ajili ya kutunza mazingira ya shule yawe mazuri, kuuziwa vifaa vya ujenzi kwa bei poa pamoja na umeme wa jua kwa maeneo ya vijijini.
Akijibu changamoto hizo MO alisema amezipokea na zile ambazo ana uwezo nazo atazitekeleza mwenyewe haraka iwezekanavyo lakini nyingine ambazo ziko nje ya uwezo ataziwasilisha serikalini kwa ajili ya utekelezaji.
Walimu wa shule za msingi Manispaa ya Singida wakimsikiliza kwa makini Mh. Dewji kwenye ukumbi wa Chuo cha Ualimu Misuna.
Walimu wakilipuka kwa nderemo na vifijo mara baada ya MO kuwatangazia posho ya 50,000 kila mmoja walimu hao.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya
Singida Salum Mahami akizungumza katika hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Yona Maki akizungumza kwenye hafla hiyo.
Katibu Mwenezi wa CCM Singida Mjini Hassan Mazala alikuwa MC kwenye hafla hiyo.
MO akiwa katika picha ya pamoja na walimu wa shule ya msingi Mtamaa, walioketi mbele kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Yona Maki, Katibu wa CCM Mjini Mary Maziku na Kaimu Ofisa Elimu Manispaa ya Singida Ramadhan Labito.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida Salum Mahami akisalimiana na MO.
The ultimate success in the work of building socialism in Tanzania-aselsewhere-depends upon the people of this nation. For any society is onlywhat the people make of it. The benefits to the people of a socialist societywill depend upon their contributions to it-their work, their co-operation forthe common good, and their acceptance of each other as equals andbrothers.
Julius K. Nyerere, 1968
Mbunge wa Singida Mjini Mh. Mohammed Dewji akizungumza na walimu 808 wa shule 43 za Msingi Manispaa katika hafla fupi iliyoandaliwa na ofisi yake kwa ajili ya kukutana na walimu hao ili kubaini changamoto zinazowakabili katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.Julius K. Nyerere, 1968
Na Hillary Shoo, Singida.
Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini Mohammed Dewji (MO) amewashangaza walimu wa shule za Msingi Manispaa ya Singida pale alipowapa posho ya shilingi 50,000 kila mmoja wakati wa hafla fupi ya kuzungumzia changamoto zinazowakabili walimu hao.
Ndugu zangu walimu kwa kuwa leo hii nimefurahi kukutana nanyi hapa na kuzungumzia changamoto zinazowakabili katika kutekeleza kazi zenu za kila siku posho ya leo kila mwalimu atapata shilingi 50,000 . alisema MO na kusababisha ukumbi mzima kulipuka kwa nderemo na vifijo.
Akizungumza mwishoni mwa wiki na walimu hao kwenye ukumbi wa chuo kipya cha ualimu Misuna Dewji aliwashukuru walimu kwa kukichagua chama cha CCM na kukipa ridhaa ya kuongoza nchi.
Aidha alisema heshima waliyompa pamoja na wananchi wa jimbo hilo anaienzi na kuithamini kwa moyo wake wote kwani anatambua umuhimu wao katika jimbo hilo Nani kama mwalimu, walimu waliitikia hakuna.
Mapema Kaimu Ofisa Elimu wa Manispaa ya Singida Ramadhan Labito alimweleza Mbunge kuwa walimu wanakabiliwa na changamoto nyingi ikwemo ukosefu wa madawati na uchakavu wa vyumba vya madarasa katika shule nyingi za msingi.
Labito alitaja changamoto nyingine kuwa ni ukosefu wa nyumba za walimu maeneo ya vijijini, kukopeshwa vyombo vya usafiri, kupatiwa viwanje vyenye hati, kupatiwa mikopo mbalimbali yenye masharti nafuu, kuimarishwa kwa vituo vya kulelea watoto yatima kititimo na Kompyuta mashuleni.
Zingine kwa mujibu wa Kaimu Ofisa elimu Labito ni kuchimbiwa visima vidogo mashuleni ili upatikanaji wa maji kwa ajili ya kutunza mazingira ya shule yawe mazuri, kuuziwa vifaa vya ujenzi kwa bei poa pamoja na umeme wa jua kwa maeneo ya vijijini.
Akijibu changamoto hizo MO alisema amezipokea na zile ambazo ana uwezo nazo atazitekeleza mwenyewe haraka iwezekanavyo lakini nyingine ambazo ziko nje ya uwezo ataziwasilisha serikalini kwa ajili ya utekelezaji.
Walimu wa shule za msingi Manispaa ya Singida wakimsikiliza kwa makini Mh. Dewji kwenye ukumbi wa Chuo cha Ualimu Misuna.
Walimu wakilipuka kwa nderemo na vifijo mara baada ya MO kuwatangazia posho ya 50,000 kila mmoja walimu hao.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya
Singida Salum Mahami akizungumza katika hafla hiyo.
Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Yona Maki akizungumza kwenye hafla hiyo.
Katibu Mwenezi wa CCM Singida Mjini Hassan Mazala alikuwa MC kwenye hafla hiyo.
MO akiwa katika picha ya pamoja na walimu wa shule ya msingi Mtamaa, walioketi mbele kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Manispaa ya Singida Yona Maki, Katibu wa CCM Mjini Mary Maziku na Kaimu Ofisa Elimu Manispaa ya Singida Ramadhan Labito.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Singida Salum Mahami akisalimiana na MO.