Pundamilia07
JF-Expert Member
- Oct 29, 2007
- 1,439
- 54
- Thread starter
- #101
kichuguu;278338]Afadhali unatambua kuwa uko huru kutoa mawazo yako kulingana na unavyoamini. Kwa hiyo, haya ni mawazo yako tu kulingana na imani yako, na wala hayana ukweli wowote ule.
Je unatamabua vile vile kuwa imani yako inaweza kuwa si sahihi hivyo ukatoa mawazo yasiyo sahihi?
Na wewe hayo hapo juu pia ni mawazo yako siyo lazima yawe na ukweli wowote.
Je unatamabua kuwa siyo vyema kulazimisha watu wengine wakubaliane na mawazo yako.
Hakuna mahali popote nilipoandika kuwa ninalazimisha ukubalianae na mawazo yangu, kama ipo nitafurahi kama utanionesha.
Ukiona wengi hawakubaliani nawe, ama nyamaza uachane nao au kubaliana nao; lakini kujaribu kulazimisha ili mawazo yako yakubalike ni kupoteza muda bure.
Unachekesha sana, itabidi hii kauli yako tuwapatie wana-demokrasia waliobobea waifanyie kazi.
Sidhani kamakutokukubaliana na mtu kimawazo suluhisho ni kunyamaza? Ninyi ndiyo mliyoifikisha nchi hii hapa ilipo kwa vile hamkukubaliana na CCM basi mkanyamaza!!!
Ni afadhali ungetuelimisha ambao hatujaona ya kusifia kuliko kutulazimisha tusifie lislokuwepo. Hii tabia ya kufuata mkumbo kama vile kuandamana eti kuunga mkono hotuba ya raisi ni kati ya mambo yayoturudisha nyuma sana kimawazo.
Sioni uhusianao wowote wa kitendo changu cha kumuunga mkono Mh Rais na kukurudisha wewe nyuma kimawazo
'Hatujaona matokeo' kichuguu ni wewe na nani ambao hamjaona?
Hivi umesahahu kuwa ni wewe mwenyewe uliyeanzisha thread hii ya kutaka tumpongeze Kikwete. Baada ya hapo umekuja mbogo sana kwa kila aliyekujibu kwa kutokubaliana nawe. Hebu kuwa mkweli urudi nyuma uangalie idadi, aina na maudhui ya post ulizoweka hapa tangu uanzishe thread hii. Ukaichia ile uliyotumia kufungua thread, post nyingine zote ni za kumshambulia kila aliyejibu bila kukubaliana nawe.
Kutokukubaliana ni sehemu ya demokrasi ambayo inafundisha kuwa wengi wape. Wachache wasiokubaliana wengi huwa hawawalazimishi wengi wakubaliane nao, badala yake huwaelimisha kama kweli wanadhani kuwa hao wengi wamekosea.
Unataka sisi tufuate mkumbo wako wa kumsifia Rais wakati tunaona wazi kabisa kuwa hajafanya kazi yake; tabia ya kufuata mkumbo ni mbaya na inachangia kurudisha nyuma maendeleo. Wewe hujafanikiwa kutufanya tufuate mkumbo wako kwa hiyo hujachangia lolote kuturudisha numa kimawazo.
Bubu ataka kusema,
Wewe siyo msemaji wa 'Watanzania wengi' hizo zako ni hisia tu na ambazo hazijengi hoja ya nguvu katika majadliano
mimi pia sijayaona
Bubu ataka kusema,
Wewe siyo msemaji wa 'Watanzania wengi' hizo zako ni hisia tu na ambazo hazijengi hoja ya nguvu katika majadliano.
In fact sioni wapi pa kubadilisha pamoja na maelezo yako marefu ndiyo umezidi kuharibu na kuonesha kwa kiasi gani umepoteza mwelekeo. Tafuta mtu atayeweza ku-refresh your mind.
Tatizo ninaloliona hapa ni kuwa EPA imegeuka kuwa ajenda ya kisiasa badala ya kuchukuliwa kama criminal act ambayo ina taratibu zake za kushughulikiwa.Yangu macho.
Ukiona umesifiwa na IMF pia ukakaribishwa IKULU YA BUSH (White house) jua nchi imeshauzwa yote.
Hiyo ni dhana kwani haina hata chembe moja ya ukweli juu ya hili tunaloliongelea, nithibitishie kwa kunipa ushahidi kuwa hilo unalodhania ni kweli.
Pundamilia nakushauri ujiunge na wana-CCM wanaompongeza kwa hotuba yake nzuri na maisha bora kwa kila MTZ wakati majumbani mwao hata kibaba cha unga hawana
Mimi si mwana-CCM wala CHADEMA. Inapofikia issue ya kitaifa sitaona aibu kutimiza wajibu kuitetea nchi yangu. Ikibidi kumpongeza Rais nitafanya hivyo kwa kujali utaifa wangu.[/SIZE]
Ikibidi kumpongeza Rais nitafanya hivyo kwa kujali utaifa wangu.
Yaani kumpongeza Rais nako ni kujali utaifa? wewe ndiyo pundamilia kabisa!!
No commentYaani kumpongeza Rais nako ni kujali utaifa? wewe ndiyo pundamilia kabisa!!
Tukipata Rais mwingine kama huyu Pundamilia tumekwisha huku porini.Yaani kumpongeza Rais nako ni kujali utaifa? wewe ndiyo pundamilia kabisa!!