Sisi wote tunaona, tunasikia na tunatafakari, hebu nieleze ni wapi katika hotuba ya Mh. Rais amesema kuwa amewasamehe waliohusika na wizi wa fedha za EPA? Alichosema kuwa amewapa hadi Novemba 1, kuwa wawe wamerudisha hizo fedha na hayo yamo katika ushauri aliopewa katika report ya wasaidizi wake yaani ya akina Mwanyika. Kama ambavyo nimeeleza hapo awali kuwa si kila kitu kilichomo ndani ya ile report aliyokabidhiwa Mh. Rais ni kwa ajili ya matumizi ya Public. Kama sisi ni waelewa wazuri hatuna budi kuiona kazi nzuri iliyokwisha fikiwa hadi sasa. Hajasamehewa mtu kwa mujibu wa ile hotuba, kama ulifuatilia vizuri hati zao za kusafiria zimeshikiliwa ikiwa ni pamoja na vitu vingine. Maamuzi ya Rais juu ya EPA bado yapo katika awamu za utekelezaji, tusubiri baada ya Novemba 1.
Tumpongeze Rais wetu baada ya Novemba 1. Utekelezaji utakapokuwa umekamilika na wezi wamefikishwa kunakostahili. IMF wamemtia moyo tu.