MNYISANZU JF Uko Wapi Mpango Mkakati wako Iramba Mashariki!!!

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Aug 24, 2011
48,758
102,105
Kiukweli majimbo ya Iramba yanapita katika wakati mgumu sana nadhani kuliko vipindi vyote. Majimbo yapo ICU, na bendera zipo nusu mlingoti hasa baada ya wabunge wake kufanya mapambano ambayo wananchi wao hawakuwatuma.

Katika kampeni 2010 sikuwahi kuwasikia wabunge hawa wakiahidi kupambana na CDM tena kwa mbinu za kishetani…….pamoja na kumwagiwa pesa chafu lakini tuliahidiwa pia maisha bora. Kutokana na majimbo yote 2 kukaribia kupalalaizi wametokea makamanda wanaoguswa kwa namna ya kipekee na ''yatima'' hawa wa Iramba kuamua ku-rescue situation, kwa upande wa Iramba Mashariki ambae mbunge wake ni Mama Salome Mwambu, mojawapo ni mwenzetu Kamanda Mnyisanzu JF.

Kwa kuwa CDM we move as a team, nadhani ni vyema sasa tukaku-assess kupitia strategies zako katika kujenga chama


  • Nini jitihada zako za kuwa ''mbunge'' wa Iramba Mashariki aliye nje ya bunge kama ilivyo kwa Dr.Slaa kuwa rais miyoni mwa wananchi i.e rais nje ya ikulu
  • Nini jitihada zako ktk kuiandalia zulia jekundu ''red carpet'' M4C Taifa kama ilivyokuwa Dar, kusini, Iringa na sasa Chato
  • Kwa kuwa ''dawa'' ya CCM 2015 ipo jikoni,nini jitihada za ''kumnywesha'' mgombea wa CCM hata kama hataki……..mfano mikakati ya mobilize vijana kiasi cha kuwa tayari hata kulinda kura kama ilivyo kwa majimbo ya CDM
  • N.k

Karibu mkuu, funguka kama hutajali…….hali ni mbaya sana huku kwetu, majimbo yamekuwa kama dustbin la kashfa za wabunge wetu, tumekuwa wasikilizaji tu jinsi wenzetu wanavyowakilishawa vyema za wabunge wao mf Ubungo, Kawe, Mbeya Mjini, Iringa n.k!
 
Jirani, samahani kwa kuchelewa kukupatia response kamili kuhusiana na haya mambo uliyoniuliza. Nimechelewa kufanya hivyo kwa sababu nilikuwa vijijini na pia nilikuwa natumia simu ambayo capacity yake ilikuwa ni ndogo.

Kwa kuanzia, for a long time nimekuwa nikifanya seminars, mikutano, workshops, et al ili kutoa elimu ya uraia kwa wananchi sambamba na kutoa elimu ya katiba hasa ikizingatiwa kuwa mimi binafsi nasomea sheria. Lengo kubwa ni kuleta awareness kwa wananchi ili waweze kuzitambua haki zao na pia wawe tayari kuzidai haki zao za msingi pale wanapoporwa na serikali/viongozi dhalimu.

Essentially ni kutoa elimu ya uraia kwa wananchi na pia kuendeleza operation ya M4C Iramba Mashariki. Kazi hii ni ngumu kutokana na ukweli kwamba kwa muda mrefu CCM imekuwa ikiwapumbaza wananchi ili wasitambue haki zao za msingi hivyo basi nimekuwa nikiji-engage ktk ku-change minds na attitudes za watu waliopumbazwa!.

Karibu kwanza ili tuendelee kujadili pamoja... pia uliza na maswali mengineyo
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom