Paparazi Muwazi
JF-Expert Member
- Dec 23, 2007
- 310
- 79
Mwanasheria Mkuu wa Serikali Jaji Werema alimjibu Mnyika bungeni kuwa bunge halina nafasi katika kushughulikia mgogoro kati ya serikali na walimu kwa kuwa kwa kufanya hivyo itakuwa ni kuingilia kazi za muhimili wa serikali.
Werema aliyasema hayo baada ya Mnyika kudai kwenye mchango wake kuwa kwa kuwa mahakama imehukumu kuwa Serikali na walimu warejee katika majadiliano kwa kuwashirikisha wataalamu wa masuala ya kazi, ni muhimu wataalamu hao wateuliwe na bunge au kamati husika ya kudumu ya Bunge.
Mnyika alisema ni lazima chombo cha tatu kiingilie kati kwa kuwa tayari walimu na serikali walishashindwa kukubaliana katika hatua ya usuluhishi na kudai kuwa chombo hicho kwa mujibu wa katiba ya nchi ibara ya 63 ni bunge ambalo ndilo lenye mamlaka ya kuisimamia serikali kwa niaba ya wananchi.
Mnyika alidai kuwa suluhisho la mgogoro huo na Serikali baada ya kupanua wigo wa mapato kufuatia marekebisho ya muswada wa sheria ya fedha iwasilishe bungeni bajeti ya nyongeza yenye kuweka vipaumbele katika masuala ya msingi ya taifa.
Mnyika alidai kuwa chanzo cha mgogoro huo ni bajeti finyu ya serikali na chombo chenye kupitisha bajeti ni bunge hivyo linapaswa kuingilia kati hoja ambayo ilipingwa na Werema kwa madai kuwa mgogoro huo unaohusu walimu na serikali na kwamba mahakama imeshaamua warejee kwenye majadiliano hivyo bunge kuingilia kati ni kuvunja katiba ya nchi na kuingilia mihimili mingine ya dola.
Kwa upande mwingine, Werema alimkosoa Mnyika kuwa mahakama haikusema kwamba serikali imevunja katiba. Werema aliyasema hayo wakati akijibu madai ya Mnyika aliyoyatoa bungeni kuwa katika kipindi cha mgomo wa walimu wapo viongozi na watendaji wa serikali waliokiuka ibara ya 4 na 107 A za katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waliyoapa kuilinda na kuhoji hatua ambazo zimechukuliwa na serikali kufuatia hali hiyo.
Aidha Jaji Werema amekemea tabia ya wanasiasa kuwapotosha wafanyakazi na kuwataka pia wasifanye mikutano nao.
Werema aliyasema hayo baada ya Mnyika kudai kwenye mchango wake kuwa kwa kuwa mahakama imehukumu kuwa Serikali na walimu warejee katika majadiliano kwa kuwashirikisha wataalamu wa masuala ya kazi, ni muhimu wataalamu hao wateuliwe na bunge au kamati husika ya kudumu ya Bunge.
Mnyika alisema ni lazima chombo cha tatu kiingilie kati kwa kuwa tayari walimu na serikali walishashindwa kukubaliana katika hatua ya usuluhishi na kudai kuwa chombo hicho kwa mujibu wa katiba ya nchi ibara ya 63 ni bunge ambalo ndilo lenye mamlaka ya kuisimamia serikali kwa niaba ya wananchi.
Mnyika alidai kuwa suluhisho la mgogoro huo na Serikali baada ya kupanua wigo wa mapato kufuatia marekebisho ya muswada wa sheria ya fedha iwasilishe bungeni bajeti ya nyongeza yenye kuweka vipaumbele katika masuala ya msingi ya taifa.
Mnyika alidai kuwa chanzo cha mgogoro huo ni bajeti finyu ya serikali na chombo chenye kupitisha bajeti ni bunge hivyo linapaswa kuingilia kati hoja ambayo ilipingwa na Werema kwa madai kuwa mgogoro huo unaohusu walimu na serikali na kwamba mahakama imeshaamua warejee kwenye majadiliano hivyo bunge kuingilia kati ni kuvunja katiba ya nchi na kuingilia mihimili mingine ya dola.
Kwa upande mwingine, Werema alimkosoa Mnyika kuwa mahakama haikusema kwamba serikali imevunja katiba. Werema aliyasema hayo wakati akijibu madai ya Mnyika aliyoyatoa bungeni kuwa katika kipindi cha mgomo wa walimu wapo viongozi na watendaji wa serikali waliokiuka ibara ya 4 na 107 A za katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania waliyoapa kuilinda na kuhoji hatua ambazo zimechukuliwa na serikali kufuatia hali hiyo.
Aidha Jaji Werema amekemea tabia ya wanasiasa kuwapotosha wafanyakazi na kuwataka pia wasifanye mikutano nao.