Lukolo
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 5,143
- 3,196
Huyu anasema ikitokea, ilihali kila siku tunaambiwa? Mimi ninainteract na waKenya almost kila wiki, na wanasema kabisa, Tanzania ina serikali legelege kuliko zote Africa mashariki. Tena kuna mmoja amekwenda mbali sana na kunambia Tanzania haina rais bali ina kivuli cha rais. Huyu alikuwa anashangaa namna wanyama walivyoweza kupakiwa kwenye ndege na kutoroshwa bila ya serikali kujua. Wanaomsifia Kikwete ni waganda tu, lakini si wakenya na wanyarwanda. Sina taarifa kuhusu waburundi wanachosema juu yetu.Nitajisikia vibaya kwamba hata wao wamelijua hilo
Binafsi sijisikii vibaya kwa kuambiwa ukweli, ambacho huwa nafanya ni kuwaunga mkono na kuonyesha masikitiko yangu, ya kuwa na Rais asiyejua ni kwanini yupo Ikulu. Hilo linaniumiza sana. Laiti yangekuwa ni mamlaka yangu, huyu jamaa alikuwa aondolewe siku nyingi sana. Ni dhaifu kupitiliza, tena hana hata sifa ya kuwa mjumbe wa nyumba kumi. He is just a laissez-faire!