Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,422
- 911,172
Mnyika kuendelea na hoja yake Sunday, 09 January 2011 20:52
Claud Mshana
MBUNGE wa Ubungo kupitia Chadema, John Mnyika, amesema ataendelea na mpango wake wa kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusu Katiba, licha ya Rais Jakaya Kikwete kutoa tamko kuwa, ataunda tume itakayoshughulikia mchakato wa kupatikana kwa Katiba mpya.
Kwa mujibu wa Mnyika, amefikia uamuzi huo baada ya kuwasiliana na baadhi ya wataalam wa masuala ya Katiba, viongozi wa asasi za kiraia, baadhi ya viongozi wa dini, viongozi wa chama chake na wapiga kura wake.
Katika taarifa aliyotuma kwa vyombo vya habari jana, Mnyika anasema serikali ya Rais Kikwete imeshindwa kutoa ufafanuzi kuhusu utaratibu utakaotumika, hivyo anaamini kuwa hakutakuwa na mpango wa kuhusisha umma au bunge katika mchakato huo.
Mbunge huyo alifafanua kuwa kauli ya Rais Kikwete aliyotoa mbele ya mabalozi mwishoni mwa wiki iliyopita, inadhihirisha kutokuwa na dhamira ya kuandika katiba mpya inayohusisha umma.
Badala yake, kuendeleza hodhi ya serikali ambayo kwa mujibu wa Mnyika inaweza kusababisha mapitio yenye kasoro zile zile zinazolalamikiwa.
Baada ya kauli niliyotoa ya kutaka ufafanuzi na matamko yaliyotolewa na wadau mbalimbali ya kueleza kasoro za hatua ya Rais Kikwete ya kutaka moja kwa moja kuunda tume, nilitarajia kwamba kauli yake ya kwanza kabisa ya mwaka huu, angetumia fursa hiyo kufafanua suala husika ikiwamo kueleza kusudio la kupeleka mapendekezo ya mchakato bungeni, inasema sehemu ya taarifa yake na kuongeza:
Hii inadhihirisha kwamba Rais Kikwete anataja katiba mpya kwa maneno tu, lakini haonyeshi kwa vitendo kuwezesha mchakato husika kwa kushirikisha umma kwa ukamilifu.
Kufuatia hali hiyo, Mnyika alisema anaendelea kukamilisha taratibu za kuwasilisha hoja binafsi kwenye bunge la Februari kuhusu mchakato wa katiba mpya.
Claud Mshana
MBUNGE wa Ubungo kupitia Chadema, John Mnyika, amesema ataendelea na mpango wake wa kuwasilisha hoja binafsi bungeni kuhusu Katiba, licha ya Rais Jakaya Kikwete kutoa tamko kuwa, ataunda tume itakayoshughulikia mchakato wa kupatikana kwa Katiba mpya.
Kwa mujibu wa Mnyika, amefikia uamuzi huo baada ya kuwasiliana na baadhi ya wataalam wa masuala ya Katiba, viongozi wa asasi za kiraia, baadhi ya viongozi wa dini, viongozi wa chama chake na wapiga kura wake.
Katika taarifa aliyotuma kwa vyombo vya habari jana, Mnyika anasema serikali ya Rais Kikwete imeshindwa kutoa ufafanuzi kuhusu utaratibu utakaotumika, hivyo anaamini kuwa hakutakuwa na mpango wa kuhusisha umma au bunge katika mchakato huo.
Mbunge huyo alifafanua kuwa kauli ya Rais Kikwete aliyotoa mbele ya mabalozi mwishoni mwa wiki iliyopita, inadhihirisha kutokuwa na dhamira ya kuandika katiba mpya inayohusisha umma.
Badala yake, kuendeleza hodhi ya serikali ambayo kwa mujibu wa Mnyika inaweza kusababisha mapitio yenye kasoro zile zile zinazolalamikiwa.
Baada ya kauli niliyotoa ya kutaka ufafanuzi na matamko yaliyotolewa na wadau mbalimbali ya kueleza kasoro za hatua ya Rais Kikwete ya kutaka moja kwa moja kuunda tume, nilitarajia kwamba kauli yake ya kwanza kabisa ya mwaka huu, angetumia fursa hiyo kufafanua suala husika ikiwamo kueleza kusudio la kupeleka mapendekezo ya mchakato bungeni, inasema sehemu ya taarifa yake na kuongeza:
Hii inadhihirisha kwamba Rais Kikwete anataja katiba mpya kwa maneno tu, lakini haonyeshi kwa vitendo kuwezesha mchakato husika kwa kushirikisha umma kwa ukamilifu.
Kufuatia hali hiyo, Mnyika alisema anaendelea kukamilisha taratibu za kuwasilisha hoja binafsi kwenye bunge la Februari kuhusu mchakato wa katiba mpya.