Nikupateje
JF-Expert Member
- Dec 22, 2009
- 1,334
- 988
Acha wewe. wewe umetafiti nini? Amesema nini kuhusu Ubungo? Jimboni Mnyika ni mtupu mimi nalijua hilo kwa kuwa Mnyika ni Mbunge wangu. Mimi nimewahi kusema hapa Mnyika aitumie Ilani ya CCM kuwakandamiza sijui hataki kuisoma? Sijasikia akiwakumbusha watekeleze ahadi lukuki za barabara za jimboni Ubungo. Akisimamia hilo na barabara zile zikatengenezwa mbona atapeta tu mwaka 2015 lakini kinyume na hapo huenda akausikia Ubunge kwenye Bomba. Nyie mdanganyeni mkidhani mnamsaidia kumbe mnampoteza ati kinara; kinara wakati jimbo lake hali inatisha? wewe umewahi kupita barabara ya Kimara Mwisho kuelekea Kisukuru/segerea? Hali inatisha. Unaijua Bonyokwa wewe, Golani je, unaifahamu Kibangu ama King'ong'o au Kilungule. Utadhani hawakupiga kura hawa.
Najua hana pesa za kuleta maji wala barabara lakini hata kelele na kuwahamasisha watu wake. Mnyika ahamasishe tu barabara zile hazihitaji pesa nyingi na watu wa kule hawana makuu wewe pata grader la manispaa watajaza mafuta lichonge barabara. Awahakikishie watu kwamba atawaletea grader la manispaa waao wajitolee mafuta watu watatoa hela za mafuta na barabara zitachongwa; watu wa huko hawalalilii lami wao wanataka passability tu.
Ndiyo maana nasema acheni uvivu wa kusoma. Muulize Magufuli majibu ya Mnyika kuhusu kituo cha Ubungo na wakati mwingine anapavamia pale Ubungo bila watu kuwa na taarifa.
Ni nani aliyebuni kuwepo na barabara za pembezoni ili kupunguza foleni za Dar ambako jiji zima ni foleni kila kona.
Unaposema kuwa wewe ni mkazi wa Ubungo ukumbuke hii ni JF hujui anaye-press keyboard yuko wapi na si ajabu anaishi nyumba mnayotizamana. Na hilo si la msingi.
Na hivi vigezo ndiyo maana halisi ya mbunge. Mabunge hafukuzwi kwa sababu akirudi jimboni analala. Ubunge ni uwakilishi mle bungeni. Hiyo definition yenu ni wenye njaa wametuzoesha na ndiyo tunayopigania kuondokana nayo maana hakuna sehemu ya katiba ya nchi yoyote duniani inasema mbunge kazi yake ni tofauti na ile ya uwakilishi eti kwamba imegeuka kuwa mhimizaji au mchangia maendeleo.
Mbunge akikutana na wananchi ni kwa mujibu wa kujua kero ili akamkamate waziri husik kule bungeni. Tafiti zaidi usipende tukumegee.