Jatropha
JF-Expert Member
- Apr 9, 2009
- 1,151
- 199
Hivi karibuni Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali alitoa madai kuwa viongozi na watendaji wa Serikali wamekuwa wakiipuuza ofisi yake kiasi cha kupuuza ushauri wa kitaalamu unaotolewa na ofisi hiyo wenye lengo la kupunguza au kubana matumizi ya Serikali na kuongeza makusanyo ya Serikali ili kuipatia uwezo zaidi wa kuhudumia watanzania. Aliendelea kuwa viongozi na watendaji wa Serikali wamefikia hatua ya kuinyima ofisi yake ushirikiano kwa kuinyima nyaraka mbali mbali kwa lengo la kukwamisha ukaguzi wa fedha za umma hususan Shilingi Bilioni 48 katika mfuko wa kufufua uchumi ujulikanoa kama "Stimulus Package".
Katika kile kinachoonyesha kuwa tabia hiyo imekithiri kiasi cha kuwasababishia athari za kijamii na kiuchumi watanzania wa maeneo mabli mbali ya nchi hii, katika kikao cha bunge lililomalizika hivi karibuni Mhe John Mnyika amefichua sababu zinazopelekea wananchi wa jimbo lake la Ubungo kukosa huduma ya maji safi kuwa ni pamoja na DAWASCO kutotekeleza kikamilifu mapendekezo ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuanzia 2007/8 ambaye aliitaka kuwekeza katika upatikanaji wa maji safi. Soma kiambatanisho.
Kwa hakika wabunge wa CHADEMA wanaonyesha kwa dhati kuwa wanafahamu wajibu wao bungeni kwa mujibu wa Ibara ya 63 (3) inaeleza wajibu wa Mbunge ni "Kuishauri na Kuisimamia" Serikali.
Mhe John Mnyika tunaomba utueleze zaidi ili tuweze kufahamu zaidi sababuz zinzosababisha tukose maji safi.
Nini maoni yako
Katika kile kinachoonyesha kuwa tabia hiyo imekithiri kiasi cha kuwasababishia athari za kijamii na kiuchumi watanzania wa maeneo mabli mbali ya nchi hii, katika kikao cha bunge lililomalizika hivi karibuni Mhe John Mnyika amefichua sababu zinazopelekea wananchi wa jimbo lake la Ubungo kukosa huduma ya maji safi kuwa ni pamoja na DAWASCO kutotekeleza kikamilifu mapendekezo ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kuanzia 2007/8 ambaye aliitaka kuwekeza katika upatikanaji wa maji safi. Soma kiambatanisho.
Kwa hakika wabunge wa CHADEMA wanaonyesha kwa dhati kuwa wanafahamu wajibu wao bungeni kwa mujibu wa Ibara ya 63 (3) inaeleza wajibu wa Mbunge ni "Kuishauri na Kuisimamia" Serikali.
Mhe John Mnyika tunaomba utueleze zaidi ili tuweze kufahamu zaidi sababuz zinzosababisha tukose maji safi.
Nini maoni yako