Serayamajimbo
Senior Member
- Apr 15, 2009
- 191
- 38
Mnyika amemjia juu Rais Kikwete na ikulu kuwa ndio chanzo cha mapungufu yote katika serikali. Akichangia bajeti ya hotuba ya ofisi ya rais amesema katiba imempa mamlaka makubwa na watumishi wote wengine wanafanya kazi kwa niaba yake hivyo wanapoharibu wa kuwajibika ni yeye.Mnyika amesema kuwa Rais amelidanganya taifa kuhusu mgawo wa umeme kwa kwa aliahidi mwezi aprili kuwa mwezi julai mitambo ya umeme ya MW 260 ingekuwa imeanza kazi.Amesema Rais anapaswa kuondoa ikulu wote wanaompa ushauri mbaya, pia amerudia tena kauli ya kuwataka Ngeleja na Malima wajiuzulu.Mnyika ametaka bilioni 135 ambazo bunge limejulishwa kuwa zitatumika na Ofisi ya rais kwa ajili ya matumizi ya kitaifa bila matumizi hayo kuelezwa kwa wabunge wala kuweka kwenye vitabu zifafanuliwe.Amesema kwamba fedha hizo ndizo zinazotumiwa na ikulu kufanya matumizi ya anasa ikiwemo safari nyingi za nje.Ameilipua pia ofisi ya rais kwa ufisadi uliofanyika wa malipo ya bilioni 3 kwa kampuni ya Twiga Chemicals kinyume na maamuzi na kutaka TAKUKURU na usalama wa taifa kuchukua hatua ikiwemo kuhusu rushwa katika miradi ya maji na ardhi jimboni Ubungo.Amekosoa mfumo wa bajeti ya Tanzania ambapo wabunge wanapewa vitabu vyenye kurasa chache vikiwa havielezi kwa undani matumizi ya ofisi ikiwemo ya Rais; na kuonyesha likitabu likubwa sana la bajeti ya Zambia.