Nimesikiliza vyombo vya habari vya kimataifa kama BBC na Deustch Velle,jamani hali ta Hospitali ya Taifa ni mbaya!Baadhi ya wagonjwa waliohojiwa wameelezea hali katika wodi hospitalini hapo ni mbaya kwani kuna wagonjwa waliofanyiwa upasuaji kabla ya mgomo hawaonwi na waganga.
Huku wengine wakipoteza uhai. Cha ajabu ni kwamba, ukiangalia taarifa za habari katika vyombo vyetu vya ndani ya nchi utasikia 'hali ni nzuri, huduma zinaendelea kutolewa kama kawaida'!
Na baadhi yao vimewanukuu baadhi ya wagonjwa wakithibitisha hilo. Tumwamini nani?
Huku wengine wakipoteza uhai. Cha ajabu ni kwamba, ukiangalia taarifa za habari katika vyombo vyetu vya ndani ya nchi utasikia 'hali ni nzuri, huduma zinaendelea kutolewa kama kawaida'!
Na baadhi yao vimewanukuu baadhi ya wagonjwa wakithibitisha hilo. Tumwamini nani?