Mnawaelewa wanunua hela?

Slim5

JF-Expert Member
Jan 7, 2014
28,074
37,542
Ushawahi kuiskia hii: "Tunanunua HELA MBOVU pamoja na DOLLAR"

Hii ni sauti inayosisika katika mijumuiko ya watu wengi, mf. vituo vya dala dala, sokoni, tena huwa wanutumia zile spika za koni. Wenzangu mnawaelewaje hawa jamaa!
 

Attachments

  • Hela zinauzwa.jpg
    Hela zinauzwa.jpg
    9.8 KB · Views: 46
Ushawahi kuiskia hii: "Tunanunua HELA MBOVU pamoja na DOLLAR"

Hii ni sauti inayosisika katika mijumuiko ya watu wengi, mf. vituo vya dala dala, sokoni, tena huwa wanutumia zile spika za koni. Wenzangu mnawaelewaje hawa jamaa!
Hao wananunua hela kwa nusu bei.

Kea mfano una shilingi elfu 1 ambayo ni mbovu yaani inakataliwa dukani au sehemu yoyote ile, unawapelekea wao wanakupa sh 500.
Wao wakisha inunua wanaipeleka bank ikabadilishwe
 
kwanza hiyo biashara hairuhusiwi kisheria banki tu zinaruhusiwa kubadilisha chenji na pesa mbovu na hii inachangia kushusha hata thamani ya pesa zetu kwa kifupi hao jamaa inaelekea wana watu wao BOT ambao wanashirikiana kucheza hiyo michezo kwa sababu ni vigumu sana ukienda benki kubadilishiwa pesa mbovu na hata BOT utasikia wanasema wamesimama kwa muda kubadilisha sasa unafikiri hao watu wanabadilishaje hizo pesa kama sio ufisadi mwingine
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom