Mnaongeleaje wizi wa mafuta sheli, yaani kujaza upepo?

Leo nimejaza victoria
Asee kujaza pale adi raha
Yaan ata kwa muonekano wale wa2 hawana habar na wizi
Pili unajaza fair kabisa adi roho inafrah
Yaan hawana ata chembe ya wizi
Ndo maana gar zinajaa pale kujaza
to victoria
 
Hii imeshanitokea mara mbili hapo Dodoma.. Mara ya kwanza nilikuwa natoka Mwanza kwenda Dar.. Kufika Dodoma nikajaziwa upepo.. Nilifika kwa shida sana Morogoro maana ilibidi nibanie mafuta na ilikuwa usiku.. Mara ya pili nilikuwa naenda Singida na nikajaziwa upepo Dodoma.. Mpaka nafika Singida saa saba ya usiku taa ya mafuta ilikuwa inawaka...
Mkubwa DAWA ni kujaza full tank yana mwagika unasoma mita kiasi gani unadaiwa unalipa.Na unachotakiwa kufanya ni kutafuta mtaji wa full tank first time, baada yahapo usisubirie hadi yaishe unakuwa unajaza kila unapo enda safari hutaibiwa Na Sheri yeyote
 
kuwa makini unapoingia sehemu ilipotoka bodaboda au bajaji,maranyingi hawa wanajaza mafuta hayazidi elfu tano kwahiyo wewe ukija ukitaka ya elfu ishirini wanapandishia kuanzia elfu tano mpaka elfu ishirini,unakuwa umeibiwa mafuta ya elfu tano.
 
dawa ni kujaza tank zima unakaa mwezi koz unajua kabisa gari inaingia lita ngapi,,,mengine yote mnajifariji ,,na unatakiwa kununua mafuta asubuh na mapema
 
Aisee sinza kijiweni kituo cha Puma yaani ni waizi sana nimejaza mafuta ya 30 elfu kwenye harrier yangu bado taa ya kuonesha mafuta hamna inawaka yaani nilibishana nao sana wakaniambia harrier inatank kubwa niliondoka ila roho iliniuma sana kesho yake nikaenda mlimani city sheli iliyoko kwenye kona pale sijui inaitwaje nikaweka ya 20 elfu tu mshale wa mafuta ukaenda zaidi ya robo tank. Ndipo nikaamini kituo cha puma sinza kijiweni ni waizi
mi walinambia geji yangu ni mbovu
 
BP Chuga ni shidaaa pia msisahau mkienda kuosha magari kodoeni macho kodo wanavuta petrol kwa mirija
Mm huwa namuita muosha gari tunapiga picha gauge ya mafuta na km, afu namuachia funguo nikirudi tunalinganisha na picha ndo namlipa.
 
Huu wizi upo sana hasa kwenye vituo vya oilcom, kuna sheli ya oilcom nilijaza siku moja mafuta ya elfu 30 taa haikuzima wakati siku zote huwa naweka ya elfu ishirini na taa inazima, ikabidi nimuone manager wao wakaniongezea mafuta cha ajabu hakuwakaripia wale waweka mafuta, nilijafanya kama afisa wa tra kumbe mkulima wa nyanya na vitunguu.
 
Jana oilcom ubungo wamenidukua, hii mara ya tatu sasa. Mashine yao inasoma kiasi nilicholipia ila mpaka nafika mjini gauge bado iko chini. Leo nmeenda shekilango Total kiasi kile kile cha jana gauge fasta imefika nusu. Sidhani ka nitakuwa na biashara na hawa jamaa tena.
 
Kiukweli Oilcom sijui wana shida gani? Mi juzi kuna kituo chao cha Boko magengeni niliweka ya 10000 ktk Opa jioni lakini nashangaa taa ya empty bado inawaka mpaka kesho yake asubuhi natoka home. Ninachofanya sasa hivi ni either kwenda na kidumu au kwenda kituo kingine kilichopo msikitini. lakini Oilcom washanichosha. Victoria service station wapo vizuri wana reputation nzuri sema tu hawajasambaa sana mjini ningekuwa ninatumia huduma zao tuu bila kuwa na shaka. Engen nao sioni kama wana shida.
 
Mm niona hapa mnalalamika tu sijaona anayethibitisha namna wizi unavyofanyika, anayejua jinsi wizi unavyofanyika atujuze. Pia kama unajua oilcom wanaiba kwanini unarudi tena kujaza mafuta hapo? Kama ni mwizi asusiwe.
 
Kwani ukiwekewa mafuta ya sh kadhaa unashindwa jua geji yako itapanda vp?
 
Mie kwakweli niko na sheli yangu maalum hapa uraian ndio naweka mafuta, karbia wafanyakaz wengi nmekuwa nao na wengine ni kaka zangu kabsa, ile mie bado dogo naoiga boli wananiona, napyenga kamas kwa stail ya nike wananiona so ndio ninao waamin zaid.. Kujaza sheli tofaut itokee bahat mbay tuu.. Wiz huu upo kuna sheli walikuwa hawatak kabsa kupima wese kwenye kidumu
Ukishaona kituo cha mafuta wanakataa kidumu, ujue mashine zao zimesetiwa kuiba
 
Aisee sinza kijiweni kituo cha Puma yaani ni waizi sana nimejaza mafuta ya 30 elfu kwenye harrier yangu bado taa ya kuonesha mafuta hamna inawaka yaani nilibishana nao sana wakaniambia harrier inatank kubwa niliondoka ila roho iliniuma sana kesho yake nikaenda mlimani city sheli iliyoko kwenye kona pale sijui inaitwaje nikaweka ya 20 elfu tu mshale wa mafuta ukaenda zaidi ya robo tank. Ndipo nikaamini kituo cha puma sinza kijiweni ni waizi
Pale mlimani city wapo vizuri sana. Sijajua kwa apa Kimara Baruti(Dar es salaam Tanzania). Wao Awapigi upepo kweli
 
Jinsi wanavyoiba....huwa hawazimi pump...na ufikapo hukuambia sogeza gari mbele ili usione kama pump inasoma zero zero.
Hakikisha pump inasoma zero zero kabla hajaanza kukuwekea mafuta
 
Back
Top Bottom