Rohombaya
JF-Expert Member
- Jul 4, 2011
- 13,055
- 10,339
Siku moja sheli moja ya Oil com hapa hapa Dar, nimeenda kujaza full tank, sasa sijui jamaa hakuwa mjuzi wa kuiba maana hadi tank linajaa mita inasoma lita 87, na nikiangalia gari yangu tank lake mwisho lita 70. Nilimuangalia afu nikamwambia we mwizi, akamind akaja juu akasema hajawahi kuiba toka azaliwe, nikasema niitie manager wako, akasema hayupo. Nikamwita mwenzake na jamaa flani alikuwa anapita nikasema naomba tu-drain mafuta yote kwenye tank afu tuangalie ni lita ngapi yamo pamoja na yaliyokuwamo karibu nusu tank. Nikawaambia kama mafuta yatafika hata lita 80 then nitalipa mara mbili kwa ajili ya usumbufu, jamaa ndo akashtuka ikabidi aanze kuniomba tuyamalize. Nikamkomalia mimi nilikuja na nusu tank, hivo nitalipia nusu tank ambayo ni lita 35 jamaa akawa anaomba kuwa pamoja na kuwa walinipiga lakini mafuta waliyoweka ni zaidi ya hapo, nikakomalia lita 35 kwa kuwa ni muongo na nikalipia hiyo nikachapa lapa. Lakini kiuhalisia taa ya mafuta ilishawaka, niliamua tu kuwakomesha na wao.
BP sinza ni hatari. Especially ukiweka mafuta mda wa usiku.Chukueni tahadhari
Pole wale ni hatari mno kuna siku minikifika nkawaambie waniwekee mafuta waset tu waiche mashine yenyewe bila kushika ooo hauifanyibkazi nikiiachia mafuta hayaingii nkamwambia basi nkasepa...Aisee sinza kijiweni kituo cha Puma yaani ni waizi sana nimejaza mafuta ya 30 elfu kwenye harrier yangu bado taa ya kuonesha mafuta hamna inawaka yaani nilibishana nao sana wakaniambia harrier inatank kubwa niliondoka ila roho iliniuma sana kesho yake nikaenda mlimani city sheli iliyoko kwenye kona pale sijui inaitwaje nikaweka ya 20 elfu tu mshale wa mafuta ukaenda zaidi ya robo tank. Ndipo nikaamini kituo cha puma sinza kijiweni ni waizi
Yani Nina wiki mbili nalalamika mbona mafuta yanaisha haraka sana lohhh yani had ilibidi niwe nacheck labda tanki linavuja..yani hali mbaya..nimechange vituo kama kumi, ila nilipojaza Victoria sijapata shida
Aisee sinza kijiweni kituo cha Puma yaani ni waizi sana nimejaza mafuta ya 30 elfu kwenye harrier yangu bado taa ya kuonesha mafuta hamna inawaka yaani nilibishana nao sana wakaniambia harrier inatank kubwa niliondoka ila roho iliniuma sana kesho yake nikaenda mlimani city sheli iliyoko kwenye kona pale sijui inaitwaje nikaweka ya 20 elfu tu mshale wa mafuta ukaenda zaidi ya robo tank. Ndipo nikaamini kituo cha puma sinza kijiweni ni waizi
Oil com wanaiba na hayo unayowekewa ni machafu...nilishauwa nozzles kwenye gx110. Gari ilikua fresh ila baada ya kuweka tu nusu tank..check engine light ikawaka.Oil com wamenila juzjuz yaan niliendesha kwa hasira sana
Niko pamoja na wewe kabisa juu ya uloyosemawataalamu wanadai kuwa kituo chochote Tanzania kama kinaendesha na TOTAL, GAPCO na ORIX kinaweza kuaminika, nasikia hata BP kabla haijabadilishwa ilikuwa vizuri sana lakini kwa sasa usithubutu. Hii inahusu vipimo sahihi na ubora wa mafuta yaani uchakachuaji.
Ni kweli hawaruhusu skuizi kwa kisingizio unaweza kumchoma mtu moto ikawa kesiKuna cku jini likaniishia mafuta mitaa ya mbezi,nikaomba kidumu kwa jamaa wa boda boda,nilipoenda petrol station na kidumu,nikaaambiwa meneja aruhusu kununua mafuta kwenye kidumu,ikabidi niwe mpole
Kama ilivyo pempers, kumbe kuna hugis, Molffx, sleep, nk, ila watu wanaita zote pempers.Hahaha! Mazoea tu hayo ya watanzania ila hakipo.Nadhani Shell walikuwa ndio wakwaza kuanza kuuza mafuta kwenye soko la retail, so watanzania wakajikuta wanazoea hilo jina na ikawa kawaida kwa watu kuita jina la kaampuni ya Shell kwa kila kituo.
Huyo dada ndio tabia yake ila kituo kimenunuliwa na ORYX pale kwa kopa cha ajabu yule dada bado wamemuajiri tena pale pale alishawahi kunibia mafuta yangu akaniharibia siku ni mwizi hatari.siku moja nipo na kirikuu yangu yule dada ananiambia sogea mbele nikamwambia aweke mafuta ya elfu kumi akaminyaaa weee nikaona ameweka mafuta ya elfu nane! nikampa elfu kumi nikamwambia nirudishie chenji yangu elfu mbili akashtuka akasema eti ameweka ya elfu kumi nikamwambia mbona nimekushuhudia umeweka ya elfu nane? kwa aibu yake akaongeza mafuta ya elfu mbili! hapo ilikuwa Oilcom ya zamani pale kwa kopa! haya juzi nimeenda na suzuki van yangu mpaka puma ya mwanamboka baada ya hapo gari ikawa inabadilika mlio halafu haina nguvu kumpelekea fundi leo kafanya uchunguzi wake kumbe mafuta ni machafu na yamechakachuliwa na maji! Roho imeniuma sana itanibidi nirudie enzi zangu za kununua mafuta kwenye dumu la lita ishirini na walipokuwa wananiona na dumu langu kama hawajaniona vile wanahudumia magari kwanza mpaka boda boda lakin mwenye kidumu unawekwa nyuma na msonyo juu!
Victoria na ENGEN ni waaminifu sana, ila hawa wenzetu wajanjawajanja inapaswa ukiwa unawekewa mafuta ushuke nje kabisa na usiruhusu awe anaminyaminya pump.Wezi wakubwa ni Oil com hilo halina ubishi kuna ile shell yao ya manzese ndiyo hatari zaidi,
Shell ambayo huwa najaza mafuta na roho huwa safi bila wasiwasi nawashauri nendeni shell za VICTORIA popote pale jamaa wapo vizuri sana kuanzia quantity hadi quality ya mafuta.
Naam ,mara zote hukataa.Dawa nikwenda na kidumu chako sheli baasi unapaki gari pembeni unachukua kidumu unanunua mafuta yako unajaza kwenye gari unasepa
nlikuwa na jamaa angu I see huwa nikipita hapo kila mara nakumbuka hasira zangu zinarenewpole sana mKuu. ulikuwa pekeako au na shemeji?
Kumbe oil com hawafai eeOil com wanaiba na hayo unayowekewa ni machafu...nilishauwa nozzles kwenye gx110. Gari ilikua fresh ila baada ya kuweka tu nusu tank..check engine light ikawaka.